< Leviticus 6 >
1 And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
Bwana alisema na Musa kumwabia,
2 'When any person doth sin, and hath committed a trespass against Jehovah, and hath lied to his fellow concerning a deposit, or concerning fellowship, or concerning violent robbery, or hath oppressed his fellow;
“Kama mtu akifanya dhambi na kuvunja amri kinyume na Bwana, kama kujihusisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani cha kutokuwa mwaminifu, au kama akidanganya au kuiba au amemdhurumu jirani.
3 or hath found a lost thing, and hath lied concerning it, and hath sworn to a falsehood, concerning one of all [these] which man doth, sinning in them:
Au akiokota kitu fulani ambacho jirani yake amepoteza na kusema uongo kuhusu hicho, na kuapa kwa uongo au kwa mambo kama haya ambayo watu wanaweza kutenda dhambi.
4 'Then it hath been, when he sinneth, and hath been guilty, that he hath returned the plunder which he hath taken violently away, or the thing which he hath got by oppression, or the deposit which hath been deposited with him, or the lost thing which he hath found;
Ndipo itakuwa hivi, kama ametenda dhambi na hatia, kwamba lazima akirudishe kwa vyovyote alichoiba au kudanganya au amedhurumu au kitu kilichopotea naye kukiokota.
5 or all that concerning which he sweareth falsely, he hath even repaid it in its principal, and its fifth he is adding to it; to him whose it [is] he giveth it in the day of his guilt-offering.
Au kama amedanganya kwa jambo lolote, lazima atakirudisha kamilina kuongezea sehemu ya tano kwa kumlipa anayedai, kwa siku ile anayopatikana na hatia.
6 'And his guilt-offering he bringeth in to Jehovah, a ram, a perfect one, out of the flock, at thy estimation, for a guilt-offering, unto the priest,
Ataleta sadka ya hatia kwa Bwana: kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi lake kulingana na thamani yake, kama sadaka ya hatia kwa kuhani.
7 and the priest hath made atonement for him before Jehovah, and it hath been forgiven him, concerning one thing of all that he doth, by being guilty therein.'
Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele ya Bwana, atakuwa amesamehewa kulingana na chochote kilicho mfanya kuwa na hatia.”
8 And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
Ndipo Bwana alisema na Musa kumwambia,
9 'Command Aaron and his sons, saying, This [is] a law of the burnt-offering (it [is] the burnt-offering, because of the burning on the altar all the night unto the morning, and the fire of the altar is burning on it, )
“Mwagize Haruni na wanawe, kusema, 'hii ni sheria ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa lazima iwe juu ya makaa ya madhabahu usiku wote hata asubuhi, na moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.
10 that the priest hath put on his long robe of fine linen, and his fine linen trousers he doth put on his flesh, and hath lifted up the ashes which the fire consumeth with the burnt-offering on the altar, and hath put them near the altar;
Kuhani atavaa nguo zake za kitani na atavaa nguo za kitani ndani yake. Atatoa majivu yaliyobaki baada ya moto kutekeza sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu, na ataweka majivu pembeni mwa madhabahu.
11 and he hath stripped off his garments, and hath put on other garments, and hath brought out the ashes unto the outside of the camp, unto a clean place.
Atavua mavazi haya na kuvaa mavazi mengine ili kuchukua majivu nje ya kambi na kupeleka mahali palipo safi.
12 'And the fire on the altar is burning on it, it is not quenched, and the priest hath burned on it wood morning by morning, and hath arranged on it the burnt-offering, and hath made perfume on it [with] the fat of the peace-offerings;
Moto katika madhabahu utaendelea kuwaka. Usizimike, na kuhani ataongeza kuni kila asubuhi. Atapanga juu yake sadaka ya kuteketezwa kama inavyotakiwa, na atateketeza juu yake mafuta ya sadaka ya amani.
13 fire is continually burning on the altar, it is not quenched.
Moto lazima utaendelea kuwaka katika madhabahu, kamwe usizimike.
14 'And this [is] a law of the present: sons of Aaron have brought it near before Jehovah unto the front of the altar,
Hii ni sheria ya sadaka ya nafaka. Wana wa Haruni watatoa mbele ya Bwana katika madhabahu.
15 and [one] hath lifted up of it with his hand from the flour of the present, and from its oil, and all the frankincense which [is] on the present, and hath made perfume on the altar, sweet fragrance — its memorial to Jehovah.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini wa sadaka ya nafaka na mafuta na ubani ambao uko juu ya sadaka ya nafaka, atateketeza juu ya madhabahu kuleta harufu nzuri ya shukrani ya kumpendeza Bwana.
16 'And the remnant of it do Aaron and his sons eat; [with] unleavened things it is eaten, in the holy place, in the court of the tent of meeting they do eat it.
Haruni na wanae watakula sadaka inayobaki, italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu. Watakula katika ua ya hema ya kukutania.
17 It is not baken [with] any thing fermented, their portion I have given it, out of My fire-offerings; it [is] most holy, like the sin-offering, and like the guilt-offering.
Haitaokwa pamoja na chachu. Nimewapa kama sehemu ya sadaka yangu itolewayo kwa moto, ni takatifu sana, kama sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
18 Every male among the sons of Aaron doth eat it — a statute age-during to your generations, out of the fire-offerings of Jehovah: all that cometh against them is holy.'
Kwa nyakati zote zijazo kupitia watu wa kizazi chako, mwanaume yeyote mzaliwa kutoka kwa Haruni aweza kula ni sehemu yake, ichukuliwayo katika sadaka ya Bwana kwa moto. Yeyote anayeigusa atakuwa mtakatifu.”
19 And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
Bwana aliongea tena na Musa kumwambia,
20 'This [is] an offering of Aaron and of his sons, which they bring near to Jehovah in the day of his being anointed; a tenth of the ephah of flour [for] a continual present, half of it in the morning, and half of it in the evening;
“Hii ni sadaka ya Haruni na wanawe ambayo watatoa kwa Bwana katika siku ambayo kila mwana atawekwa wakfu: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama kawaida sadaka ya nafaka nusu yake asubuhi na nusu yake jioni.
21 on a girdel with oil it is made — fried thou dost bring it in; baked pieces of the present thou dost bring near, a sweet fragrance to Jehovah.
Itatengenezwa na mafuta katika kikaango, utaileta ikiwa imeandaliwa imeokwa katika vipande utatoa sadaka ya nafaka ili kuleta harufu nzuri kwa Bwana.
22 'And the priest who is anointed in his stead, from among his sons, doth make it, — a statute age-during of Jehovah: it is completely perfumed;
Mwana wa Kuhani Mkuu atakayekuwa Kuhani Mkuu mpya kutoka miongoni mwa wanawe ataitoa. Kama amri ya milele, yote itateketezwa kwa Bwana.
23 and every present of a priest is a whole burnt-offering; it is not eaten.'
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itatekezwa yote. Haitaliwa kamwe.”
24 And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
Bwana alisema tena Musa, kumwambia,
25 'Speak unto Aaron and unto his sons, saying, This [is] a law of the sin-offering: in the place where the burnt-offering is slaughtered is the sin-offering slaughtered before Jehovah; it [is] most holy.
“Sema na Haruni na watoto wake kwamba, 'Hii ni sheria ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi lazima kuchinjwa mahali pa sadaka ya kuteketezwa itachinjwa mbeleya Bwana. Ni takatifu sana.
26 'The priest who is making atonement with it doth eat it, in the holy place it is eaten, in the court of the tent of meeting;
Kuhani atakayeitoa kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila. Italiwa mahali patakatifu katika ua wa hema ya kukutania.
27 all that cometh against its flesh is holy, and when [any] of its blood is sprinkled on the garment, that on which it is sprinkled thou dost wash in the holy place;
Yeyote atakayeigusa nyama yake atakuwa ni mtakatifu na kama damu itadondokea mavazi yatafuliwa mahali palipodondokewa, mahali patakatifu.
28 and an earthen vessel in which it is boiled is broken, and if in a brass vessel it is boiled, then it is scoured and rinsed with water.
Lakini chungu kikipikiwa kitavunjwa, kama imepikiwa katika chombo cha shaba, lazima kitasuguliwa na kusafishwa kwa maji.
29 'Every male among the priests doth eat it — it [is] most holy;
Mwanaume yeyote miongoni mwa makuhani anaweza kula nyama hiyo kwa sababu ni takatifu sana.
30 and no sin-offering, [any] of whose blood is brought in unto the tent of meeting to make atonement in the sanctuary is eaten; with fire it is burnt.
Na hakuna sadaka ya dhambi italiwa ambayo damu yake imeletwa katika hema ya kukutania kufanya upatanisho katika mahali patakatifu. Ni lazima iteketezwe.