< Job 38 >
1 And Jehovah answereth Job out of the whirlwind, and saith: —
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Who [is] this — darkening counsel, By words without knowledge?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Gird, I pray thee, as a man, thy loins, And I ask thee, and cause thou Me to know.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Where wast thou when I founded earth? Declare, if thou hast known understanding.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Who placed its measures — if thou knowest? Or who hath stretched out upon it a line?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 On what have its sockets been sunk? Or who hath cast its corner-stone?
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 In the singing together of stars of morning, And all sons of God shout for joy,
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 And He shutteth up with doors the sea, In its coming forth, from the womb it goeth out.
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 In My making a cloud its clothing, And thick darkness its swaddling band,
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 And I measure over it My statute, And place bar and doors,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 And say, 'Hitherto come thou, and add not, And a command is placed On the pride of thy billows.'
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Hast thou commanded morning since thy days? Causest thou the dawn to know its place?
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 To take hold on the skirts of the earth, And the wicked are shaken out of it,
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 It turneth itself as clay of a seal And they station themselves as clothed.
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 And withheld from the wicked is their light, And the arm lifted up is broken.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Hast thou come in to springs of the sea? And in searching the deep Hast thou walked up and down?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Revealed to thee were the gates of death? And the gates of death-shade dost thou see?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Thou hast understanding, Even unto the broad places of earth! Declare — if thou hast known it all.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Where [is] this — the way light dwelleth? And darkness, where [is] this — its place?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 That thou dost take it unto its boundary, And that thou dost understand The paths of its house.
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Thou hast known — for then thou art born And the number of thy days [are] many!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Hast thou come in unto the treasure of snow? Yea, the treasures of hail dost thou see?
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 That I have kept back for a time of distress, For a day of conflict and battle.
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Where [is] this, the way light is apportioned? It scattereth an east wind over the earth.
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Who hath divided for the flood a conduit? And a way for the lightning of the voices?
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 To cause [it] to rain on a land — no man, A wilderness — no man in it.
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 To satisfy a desolate and waste place, And to cause to shoot up The produce of the tender grass?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Hath the rain a father? Or who hath begotten the drops of dew?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 From whose belly came forth the ice? And the hoar-frost of the heavens, Who hath begotten it?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 As a stone waters are hidden, And the face of the deep is captured.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Dost thou bind sweet influences of Kimah? Or the attractions of Kesil dost thou open?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Dost thou bring out Mazzaroth in its season? And Aysh for her sons dost thou comfort?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Hast thou known the statutes of heaven? Or dost thou appoint Its dominion in the earth?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Dost thou lift up to the cloud thy voice, And abundance of water doth cover thee?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Dost thou send out lightnings, and they go And say unto thee, 'Behold us?'
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Who hath put in the inward parts wisdom? Or who hath given To the covered part understanding?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Who doth number the clouds by wisdom? And the bottles of the heavens, Who doth cause to lie down,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 In the hardening of dust into hardness, And clods cleave together?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Dost thou hunt for a lion prey? And the desire of young lions fulfil?
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 When they bow down in dens — Abide in a thicket for a covert?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Who doth prepare for a raven his provision, When his young ones cry unto God? They wander without food.
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?