< Job 21 >
1 And Job answereth and saith: —
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Hear ye diligently my word, And this is your consolation.
“Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
3 Bear with me, and I speak, And after my speaking — ye may deride.
Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
4 I — to man [is] my complaint? and if [so], wherefore May not my temper become short?
Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
5 Turn unto me, and be astonished, And put hand to mouth.
Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
6 Yea, if I have remembered, then I have been troubled. And my flesh hath taken fright.
Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
7 Wherefore do the wicked live? They have become old, Yea, they have been mighty in wealth.
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
8 Their seed is established, Before their face with them, And their offspring before their eyes.
Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
9 Their houses [are] peace without fear, Nor [is] a rod of God upon them.
Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10 His bullock hath eaten corn, and doth not loath. His cow bringeth forth safely, And doth not miscarry.
Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
11 They send forth as a flock their sucklings, And their children skip,
Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
12 They lift [themselves] up at timbrel and harp, And rejoice at the sound of an organ.
Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
13 They wear out in good their days, And in a moment [to] Sheol go down. (Sheol )
Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
14 And they say to God, 'Turn aside from us, And the knowledge of Thy ways We have not desired.
Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
15 What [is] the Mighty One that we serve Him? And what do we profit when we meet with Him?'
Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
16 Lo, not in their hand [is] their good, (The counsel of the wicked Hath been far from me.)
Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
17 How oft is the lamp of the wicked extinguished, And come on them doth their calamity? Pangs He apportioneth in His anger.
Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
18 They are as straw before wind, And as chaff a hurricane hath stolen away,
Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
19 God layeth up for his sons his sorrow, He giveth recompense unto him — and he knoweth.
Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
20 His own eyes see his destruction, And of the wrath of the Mighty he drinketh.
Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
21 For what [is] his delight in his house after him, And the number of his months cut off?
Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
22 To God doth [one] teach knowledge, And He the high doth judge?
Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
23 This [one] dieth in his perfect strength, Wholly at ease and quiet.
Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
24 His breasts have been full of milk, And marrow his bones doth moisten.
Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
25 And this [one] dieth with a bitter soul, And have not eaten with gladness.
Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
26 Together — on the dust they lie down, And the worm doth cover them over.
Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
27 Lo, I have known your thoughts, And the devices against me ye do wrongfully.
Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
28 For ye say, 'Where [is] the house of the noble? And where the tent — The tabernacles of the wicked?'
Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
29 Have ye not asked those passing by the way? And their signs do ye not know?
Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
30 That to a day of calamity is the wicked spared. To a day of wrath they are brought.
kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
31 Who doth declare to his face his way? And [for] that which he hath done, Who doth give recompence to him?
Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
32 And he — to the graves he is brought. And over the heap a watch is kept.
Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
33 Sweet to him have been the clods of the valley, And after him every man he draweth, And before him there is no numbering.
Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
34 And how do ye comfort me [with] vanity, And in your answers hath been left trespass?
Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”