< Job 11 >

1 And Zophar the Naamathite answereth and saith: —
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Is a multitude of words not answered? And is a man of lips justified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Thy devices make men keep silent, Thou scornest, and none is causing blushing!
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 And thou sayest, 'Pure [is] my discourse, And clean I have been in Thine eyes.'
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 And yet, O that God had spoken! And doth open His lips with thee.
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 And declare to thee secrets of wisdom, For counsel hath foldings. And know thou that God forgetteth for thee, [Some] of thine iniquity.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 By searching dost thou find out God? Unto perfection find out the Mighty One?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 Heights of the heavens! — what dost thou? Deeper than Sheol! — what knowest thou? (Sheol h7585)
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 Longer than earth [is] its measure, And broader than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If He pass on, and shut up, and assemble, Who then dost reverse it?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For he hath known men of vanity, And He seeth iniquity, And one doth not consider [it]!
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 And empty man is bold, And the colt of a wild ass man is born.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 If thou — thou hast prepared thy heart, And hast spread out unto Him thy hands,
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If iniquity [is] in thy hand, put it far off, And let not perverseness dwell in thy tents.
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 For then thou liftest up thy face from blemish, And thou hast been firm, and fearest not.
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 For thou dost forget misery, As waters passed away thou rememberest.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 And above the noon doth age rise, Thou fliest — as the morning thou art.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 And thou hast trusted because their is hope, And searched — in confidence thou liest down,
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 And thou hast rested, And none is causing trembling, And many have entreated thy face;
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 And the eyes of the wicked are consumed, And refuge hath perished from them, And their hope [is] a breathing out of soul!
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Job 11 >