< Genesis 44 >

1 And he commandeth him who [is] over his house, saying, 'Fill the bags of the men [with] food, as they are able to bear, and put the money of each in the mouth of his bag;
Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
2 and my cup, the silver cup, thou dost put in the mouth of the bag of the young one, and his corn-money;' and he doth according to the word of Joseph which he hath spoken.
Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
3 The morning is bright, and the men have been sent away, they and their asses —
Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
4 they have gone out of the city — they have not gone far off — and Joseph hath said to him who [is] over his house, 'Rise, pursue after the men; and thou hast overtaken them, and thou hast said unto them, Why have ye recompensed evil for good?
Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
5 Is not this that with which my lord drinketh? and he observeth diligently with it; ye have done evil [in] that which ye have done.'
Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
6 And he overtaketh them, and speaketh unto them these words,
Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
7 and they say unto him, 'Why doth my lord speak according to these words? far be it from thy servants to do according to this word;
Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
8 lo, the money which we found in the mouth of our bags we brought back unto thee from the land of Canaan, and how do we steal from the house of thy lord silver or gold?
Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
9 with whomsoever of thy servants it is found, he hath died, and we also are to my lord for servants.'
Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
10 And he saith, 'Now, also, according to your words, so it [is]; he with whom it is found becometh my servant, and ye are acquitted;'
Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
11 and they hasten and take down each his bag to the earth, and each openeth his bag;
Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
12 and he searcheth — at the eldest he hath begun, and at the youngest he hath completed — and the cup is found in the bag of Benjamin;
Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
13 and they rend their garments, and each ladeth his ass, and they turn back to the city.
Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
14 And Judah — his brethren also — cometh in unto the house of Joseph, and he is yet there, and they fall before him to the earth;
Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
15 and Joseph saith to them, 'What [is] this deed that ye have done? have ye not known that a man like me doth diligently observe?'
Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
16 And Judah saith, 'What do we say to my lord? what do we speak? and what — do we justify ourselves? God hath found out the iniquity of thy servants; lo, we [are] servants to my lord, both we, and he in whose hand the cup hath been found;'
Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
17 and he saith, 'Far be it from me to do this; the man in whose hand the cup hath been found, he becometh my servant; and ye, go ye up in peace unto your father.'
Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
18 And Judah cometh nigh unto him, and saith, 'O, my lord, let thy servant speak, I pray thee, a word in the ears of my lord, and let not thine anger burn against thy servant — for thou art as Pharaoh.
Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
19 My lord hath asked his servants, saying, Have ye a father or brother?
Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
20 and we say unto my lord, We have a father, an aged one, and a child of old age, a little one; and his brother died, and he is left alone of his mother, and his father hath loved him.
Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
21 'And thou sayest unto thy servants, Bring him down unto me, and I set mine eye upon him;
“Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
22 and we say unto my lord, The youth is not able to leave his father, when he hath left his father, then he hath died;
Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
23 and thou sayest unto thy servants, If your young brother come not down with you, ye add not to see my face.
Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
24 'And it cometh to pass, that we have come up unto thy servant my father, that we declare to him the words of my lord;
Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
25 and our father saith, Turn back, buy for us a little food,
“Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
26 and we say, We are not able to go down; if our young brother is with us, then we have gone down; for we are not able to see the man's face, and our young brother not with us.
Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
27 'And thy servant my father saith unto us, Ye — ye have known that two did my wife bare to me,
“Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
28 and the one goeth out from me, and I say, Surely he is torn — torn! and I have not seen him since;
Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
29 when ye have taken also this from my presence, and mischief hath met him, then ye have brought down my grey hairs with evil to sheol. (Sheol h7585)
Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
30 'And now, at my coming in unto thy servant my father, and the youth not with us (and his soul is bound up in his soul),
“Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
31 then it hath come to pass when he seeth that the youth is not, that he hath died, and thy servants have brought down the grey hairs of thy servant our father with sorrow to sheol; (Sheol h7585)
akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
32 for thy servant obtained the youth by surety from my father, saying, If I bring him not in unto thee — then I have sinned against my father all the days.
Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
33 'And now, let thy servant, I pray thee, abide instead of the youth a servant to my lord, and the youth goeth up with his brethren,
“Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
34 for how do I go up unto my father, and the youth not with me? lest I look on the evil which doth find my father.'
Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”

< Genesis 44 >