< Daniel 3 >
1 Nebuchadnezzar the king hath made an image of gold, its height sixty cubits, its breadth six cubits; he hath raised it up in the valley of Dura, in the province of Babylon;
Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
2 and Nebuchadnezzar the king hath sent to gather the satraps, the prefects, and the governors, the honourable judges, the treasurers, the counsellors, the sheriffs, and all the rulers of the province, to come to the dedication of the image that Nebuchadnezzar the king hath raised up.
Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
3 Then are gathered the satraps, the prefects, and the governors, the honourable judges, the treasurers, the counsellors, the sheriffs, and all the rulers of the province, to the dedication of the image that Nebuchadnezzar the king hath raised up: and they are standing before the image that Nebuchadnezzar hath raised up.
Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
4 And a crier is calling mightily: 'To you they are saying: O peoples, nations, and languages!
Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
5 at the time that ye hear the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, the symphony, and all kinds of music, ye fall down and do obeisance to the golden image that Nebuchadnezzar the king hath raised up:
Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
6 and whoso doth not fall down and do obeisance, in that hour he is cast into the midst of a burning fiery furnace.'
Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
7 Therefore at that time, when all the peoples are hearing the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, and all kinds of music, falling down are all the peoples, nations and languages, doing obeisance to the golden image that Nebuchadnezzar the king hath raised up.
Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
8 Therefore at that time drawn near have certain Chaldeans, and accused the Jews;
Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
9 they have answered, yea, they are saying to Nebuchadnezzar the king, 'O king, to the ages live!
Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
10 Thou, O king, hast made a decree that every man who doth hear the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, and the symphony, and all kinds of music, doth fall down and do obeisance to the golden image;
Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
11 and whoso doth not fall down and do obeisance, is cast into the midst of a burning fiery furnace.
na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
12 There are certain Jews whom thou hast appointed over the work of the province of Babylon — Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, these men have not made of thee, O king, [any] regard; thy gods they are not serving, and to the golden image thou hast raised up — are not making obeisance.'
Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
13 Then Nebuchadnezzar, in anger and fury, hath said to bring in Shadrach, Meshach, and Abed-Nego. Then these men have been brought in before the king.
Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
14 Nebuchadnezzar hath answered and said to them, 'Is [it] a laid plan, O Shadrach, Meshach, and Abed-Nego — my gods ye are not serving, and to the golden image that I have raised up ye are not doing obeisance?
naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 Now, lo, ye are ready, so that at the time that ye hear the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, and the symphony, and all kinds of music, ye fall down and do obeisance to the image that I have made! — and lo, ye do no obeisance — in that hour ye are cast into the midst of a burning fiery furnace; who is that God who doth deliver you out of my hands?'
Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
16 Shadrach, Meshach, and Abed-Nego have answered, yea, they are saying to the king Nebuchadnezzar, 'We have no need concerning this matter to answer thee.
Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
17 Lo, it is; our God whom we are serving, is able to deliver us from a burning fiery furnace; and from thy hand, O king, He doth deliver.
Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
18 And lo — not! be it known to thee, O king, that thy gods we are not serving, and to the golden image thou hast raised up we do no obeisance.'
Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
19 Then Nebuchadnezzar hath been full of fury, and the expression of his face hath been changed concerning Shadrach, Meshach, and Abed-Nego; he answered and said to heat the furnace seven times above that which it is seen to be heated;
Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
20 and to certain mighty men who [are] in his force he hath said to bind Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, to cast into the burning fiery furnace.
na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
21 Then these men have been bound in their coats, their tunics, and their turbans, and their clothing, and have been cast into the midst of the burning fiery furnace.
Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
22 Therefore, because that the word of the king is urgent, and the furnace heated exceedingly, those men who have taken up Shadrach, Meshach, and Abed-Nego — killed them hath the spark of the fire.
Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
23 And these three men, Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, have fallen down in the midst of the burning fiery furnace — bound.
Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
24 Then Nebuchadnezzar the king hath been astonished, and hath risen in haste; he hath answered and said to his counsellors, 'Have we not cast three men into the midst of the fire — bound?' They have answered and are saying to the king, 'Certainly, O king.'
Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
25 He answered and hath said, 'Lo, I am seeing four men loose, walking in the midst of the fire, and they have no hurt; and the appearance of the fourth [is] like to a son of the gods.'
Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
26 Then Nebuchadnezzar hath drawn near to the gate of the burning fiery furnace; he hath answered and said, 'Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, servants of God Most High come forth, yea, come;' then come forth do Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, from the midst of the fire;
Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
27 and gathered together, the satraps, the prefects, and the governors, and the counsellors of the king, are seeing these men, that the fire hath no power over their bodies, and the hair of their head hath not been singed, and their coats have not changed, and the smell of fire hath not passed on them.
Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
28 Nebuchadnezzar hath answered and hath said, 'Blessed [is] the God of Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, who hath sent His messenger, and hath delivered His servants who trusted on Him, and the word of the king changed, and gave up their bodies that they might not serve nor do obeisance to any god except to their own God.
Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
29 And by me a decree is made, that any people, nation, and language, that doth speak erroneously concerning the God of Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, pieces he is made, and its house is made a dunghill, because that there is no other god who is able thus to deliver.'
Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
30 Then the king hath caused Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, to prosper in the province of Babylon.
Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.