< 2 Kings 17 >

1 In the twelfth year of Ahaz king of Judah reigned hath Hoshea son of Elah in Samaria, over Israel — nine years,
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
2 and he doth the evil thing in the eyes of Jehovah, only, not as the kings of Israel who were before him;
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
3 against him came up Shalmaneser king of Asshur, and Hoshea is to him a servant, and doth render to him a present.
Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
4 And the king of Asshur findeth in Hoshea a conspiracy, in that he hath sent messengers unto So king of Egypt, and hath not caused a present to go up to the king of Asshur, as year by year, and the king of Asshur restraineth him, and bindeth him in a house of restraint.
Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
5 And the king of Asshur goeth up into all the land, and he goeth up to Samaria, and layeth siege against it three years;
Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
6 in the ninth year of Hoshea hath the king of Asshur captured Samaria, and removeth Israel to Asshur, and causeth them to dwell in Halah, and in Habor, [by] the river Gozan, and [in] the cities of the Medes.
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
7 And it cometh to pass, because the sons of Israel have sinned against Jehovah their God — who bringeth them up out of the land of Egypt, from under the hand of Pharaoh king of Egypt — and fear other gods,
Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
8 and walk in the statutes of the nations that Jehovah dispossessed from the presence of the sons of Israel, and of the kings of Israel that they made;
na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
9 and the sons of Israel do covertly things that [are] not right against Jehovah their God, and build for them high places in all their cities, from a tower of the watchers unto the fenced city,
Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
10 and set up for them standing-pillars and shrines on every high height, and under every green tree,
Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
11 and make perfume there in all high places, like the nations that Jehovah removed from their presence, and do evil things to provoke Jehovah,
Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
12 and serve the idols, of which Jehovah said to them, 'Ye do not do this thing;'
Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
13 And Jehovah testifieth against Israel, and against Judah, by the hand of every prophet, and every seer, saying, 'Turn back from your evil ways, and keep My commands, My statutes, according to all the law that I commanded your fathers, and that I sent unto you by the hand of My servants the prophets;'
Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
14 and they have not hearkened, and harden their neck, like the neck of their fathers, who did not remain stedfast in Jehovah their God,
Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
15 and reject His statutes and His covenant that He made with their fathers, and His testimonies that He testified against them, and go after the vain thing, and become vain, and after the nations that are round about them, of whom Jehovah commanded them not to do like them;
Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
16 And they forsake all the commands of Jehovah their God, and make to them a molten image — two calves, and make a shrine, and bow themselves to all the host of the heavens, and serve Baal,
Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
17 and cause their sons and their daughters to pass over through fire, and divine divinations, and use enchantments, and sell themselves to do the evil thing in the eyes of Jehovah, to provoke Him;
Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
18 That Jehovah sheweth himself very angry against Israel, and turneth them aside from His presence; none hath been left, only the tribe of Judah by itself.
Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
19 Also Judah hath not kept the commands of Jehovah their God, and they walk in the statutes of Israel that they had made.
na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
20 And Jehovah kicketh against all the seed of Israel, and afflicteth them, and giveth them into the hand of spoilers, till that He hath cast them out of His presence,
Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
21 for He hath rent Israel from the house of David, and they make Jeroboam son of Nebat king, and Jeroboam driveth Israel from after Jehovah, and hath caused them to sin a great sin,
Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
22 and the sons of Israel walk in all the sins of Jeroboam that he did, they have not turned aside therefrom,
Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
23 till that Jehovah hath turned Israel aside from His presence, as He spake by the hand of all His servants the prophets, and Israel is removed from off its land to Asshur, unto this day.
hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
24 And the king of Asshur bringeth in from Babylon and from Cutha, and from Ava, and from Hamath, and Sepharvaim, and causeth [them] to dwell in the cities of Samaria instead of the sons of Israel, and they possess Samaria, and dwell in its cities;
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
25 and it cometh to pass, at the commencement of their dwelling there, they have not feared Jehovah, and Jehovah doth send among them the lions, and they are destroying among them.
Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
26 And they speak to the king of Asshur, saying, 'The nations that thou hast removed, and dost place in the cities of Samaria, have not known the custom of the God of the land, and He sendeth among them the lions, and lo, they are destroying them, as they do not know the custom of the God of the land.'
Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
27 And the king of Asshur commandeth, saying, 'Cause to go thither one of the priests whom ye removed thence, and they go and dwell there, and he doth teach them the custom of the God of the land.'
Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
28 And one of the priests whom they removed from Samaria cometh in, and dwelleth in Beth-El, and he is teaching them how they do fear Jehovah,
Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
29 and they are making each nation its gods, and place [them] in the houses of the high places that the Samaritans have made, each nation in their cities where they are dwelling.
Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
30 And the men of Babylon have made Succoth-Benoth, and the men of Cuth have made Nergal, and the men of Hamath have made Ashima,
Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
31 and the Avites have made Nibhaz and Tartak, and the Sepharvites are burning their sons with fire to Adrammelech and Anammelech, gods of Sepharvim.
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
32 And they are fearing Jehovah, and make to themselves from their extremities priests of high places, and they are acting for them in the house of the high places.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
33 Jehovah they are fearing, and their gods they are serving, according to the custom of the nations whence they removed them.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
34 Unto this day they are doing according to the former customs — they are not fearing Jehovah, and are not doing according to their statutes, and according to their ordinances, and according to the law, and according to the command, that Jehovah commanded the sons of Jacob whose name He made Israel,
Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
35 and Jehovah maketh with them a covenant, and chargeth them, saying, 'Ye do not fear other gods, nor bow yourselves to them, nor serve them, nor sacrifice to them,
Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
36 but Jehovah who brought you up out of the land of Egypt with great power, and with a stretched-out arm, Him ye do fear, and to Him ye bow yourselves, and to Him ye do sacrifice;
Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
37 and the statutes, and the judgments, and the law, and the command, that He wrote for you, ye observe to do all the days, and ye do not fear other gods;
Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
38 and the covenant that I have made with you ye do not forget, and ye do not fear other gods;
Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
39 but Jehovah your God ye do fear, and He doth deliver you out of the hand of all your enemies;'
Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
40 and they have not hearkened, but according to their former custom they are doing,
Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
41 and these nations are fearing Jehovah, and their graven images they have served, both their sons and their sons' sons; as their fathers did, they are doing unto this day.
Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.

< 2 Kings 17 >