< 2 Kings 11 >
1 And Athaliah [is] mother of Ahaziah, and she hath seen that her son [is] dead, and she riseth, and destroyeth all the seed of the kingdom;
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme.
2 and Jehosheba daughter of king Joram, sister of Ahaziah, taketh Joash son of Ahaziah, and stealeth him out of the midst of the sons of the king who are put to death, him and his nurse, in the inner part of the bed-chambers, and they hide him from the presence of Athaliah, and he hath not been put to death,
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa.
3 and he is with her, in the house of Jehovah, hiding himself, six years, and Athaliah is reigning over the land.
Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
4 And in the seventh year hath Jehoiada sent and taketh the heads of the hundreds, of the executioners and of the runners, and bringeth them in unto him, to the house of Jehovah, and maketh with them a covenant, and causeth them to swear in the house of Jehovah, and sheweth them the son of the king,
Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari, na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme.
5 and commandeth them, saying, 'This [is] the thing that ye do; The third of you [are] going in on the sabbath, and keepers of the charge of the house of the king,
Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme,
6 and the third [is] at the gate of Sur, and the third at the gate behind the runners, and ye have kept the charge of the house pulled down;
theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu,
7 and two parts of you, all going out on the sabbath — they have kept the charge of the house of Jehovah about the king,
nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme.
8 and ye have compassed the king round about, each with his weapons in his hand, and he who is coming unto the ranges is put to death; and be ye with the king in his going out and in his coming in.'
Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
9 And the heads of the hundreds do according to all that Jehoiada the priest commanded, and take each his men going in on the sabbath, with those going out on the sabbath, and come in unto Jehoiada the priest,
Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada.
10 and the priest giveth to the heads of the hundreds the spears and the shields that king David had, that [are] in the house of Jehovah.
Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana.
11 And the runners stand, each with his weapons in his hand, from the right shoulder of the house unto the left shoulder of the house, by the altar and by the house, by the king round about;
Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
12 and he bringeth out the son of the king, and putteth on him the crown, and the testimony, and they make him king, and anoint him, and smite the hand, and say, 'Let the king live.'
Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
13 And Athaliah heareth the voice of the runners [and] of the people, and she cometh in unto the people, to the house of Jehovah,
Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana.
14 and looketh, and lo, the king is standing by the pillar, according to the ordinance, and the heads, and the trumpets, [are] by the king, and all the people of the land are rejoicing, and blowing with trumpets, and Athaliah rendeth her garments, and calleth, 'Conspiracy! conspiracy!'
Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”
15 And Jehoiada the priest commandeth the heads of the hundreds, inspectors of the force, and saith unto them, 'Bring her out unto the outside of the ranges, and him who is going after her, put to death by the sword:' for the priest had said, 'Let her not be put to death in the house of Jehovah.'
Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.”
16 And they make for her sides, and she entereth the way of the entering in of the horses to the house of the king, and is put to death there.
Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.
17 And Jehoiada maketh the covenant between Jehovah and the king and the people, to be for a people to Jehovah, and between the king and the people.
Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu.
18 And all the people of the land go in to the house of Baal, and break it down, its altars and its images they have thoroughly broken, and Mattan priest of Baal they have slain before the altars; and the priest setteth inspectors over the house of Jehovah,
Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana.
19 and taketh the heads of the hundreds, and the executioners, and the runners, and all the people of the land, and they bring down the king from the house of Jehovah, and come by the way of the gate of the runners, to the house of the king, and he sitteth on the throne of the kings.
Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi,
20 And all the people of the land rejoice, and the city [is] quiet, and Athaliah they have put to death by the sword in the house of the king;
nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.
21 a son of seven years is Jehoash in his reigning.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.