< 2 Corinthians 10 >

1 And I, Paul, myself, do call upon you — through the meekness and gentleness of the Christ — who in presence, indeed [am] humble among you, and being absent, have courage toward you,
Basi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi!
2 and I beseech [you], that, being present, I may not have courage, with the confidence with which I reckon to be bold against certain reckoning us as walking according to the flesh;
Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu.
3 for walking in the flesh, not according to the flesh do we war,
Ingawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo.
4 for the weapons of our warfare [are] not fleshly, but powerful to God for bringing down of strongholds,
Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome,
5 reasonings bringing down, and every high thing lifted up against the knowledge of God, and bringing into captivity every thought to the obedience of the Christ,
tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo,
6 and being in readiness to avenge every disobedience, whenever your obedience may be fulfilled.
tena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.
7 The things in presence do ye see? if any one hath trusted in himself to be Christ's, this let him reckon again from himself, that according as he is Christ's, so also we [are] Christ's;
Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo.
8 for even if also anything more abundantly I shall boast concerning our authority, that the Lord gave us for building up, and not for casting you down, I shall not be ashamed;
Basi hata kama nikijisifu zaidi kidogo kuhusu mamlaka tuliyo nayo, ambayo Bwana alitupa ili kuwajenga wala si kuwabomoa, mimi sitaionea haya.
9 that I may not seem as if I would terrify you through the letters,
Sitaki nionekane kama ninayejaribu kuwatisha kwa nyaraka zangu.
10 'because the letters indeed — saith one — [are] weighty and strong, and the bodily presence weak, and the speech despicable.'
Kwa maana wanasema, “Nyaraka zake ni nzito na zenye nguvu, lakini ana kwa ana ni dhaifu na kuzungumza kwake ni kwa kudharauliwa.”
11 This one — let him reckon thus: that such as we are in word, through letters, being absent, such also, being present, [we are] in deed.
Watu kama hao wajue ya kuwa, yale tusemayo kwa barua tukiwa hatupo pamoja nanyi, ndivyo tulivyo na ndivyo tutakavyofanya tutakapokuwa pamoja nanyi.
12 For we do not make bold to rank or to compare ourselves with certain of those commending themselves, but they, among themselves measuring themselves, and comparing themselves with themselves, are not wise,
Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojitukuza wenyewe kuwa wao ni wa maana sana. Wanapojipima na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara.
13 and we in regard to the unmeasured things will not boast ourselves, but after the measure of the line that the God of measure did appoint to us — to reach even unto you;
Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ile Mungu aliyotuwekea, mipaka ambayo inawafikia hata ninyi.
14 for not as not reaching to you do we stretch ourselves overmuch, for even unto you did we come in the good news of the Christ,
Kwa maana hatukuwa tunavuka mipaka katika kujisifu kwetu, kama vile ambavyo ingekuwa kama hatukuwa tumekuja kwenu. Kwa maana sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuja kwenu na Injili ya Kristo.
15 not boasting of the things not measured, in other men's labours, and having hope — your faith increasing — in you to be enlarged, according to our line — into abundance,
Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi,
16 in the [places] beyond you to proclaim good news, not in another's line in regard to the things made ready, to boast;
ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine.
17 and he who is boasting — in the Lord let him boast;
Lakini, “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
18 for not he who is commending himself is approved, but he whom the Lord doth commend.
Kwa maana si yeye ajisifuye mwenyewe akubaliwaye, bali yeye ambaye Bwana humsifu.

< 2 Corinthians 10 >