< 1 John 3 >

1 See ye what love the Father hath given to us, that children of God we may be called; because of this the world doth not know us, because it did not know Him;
Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2 beloved, now, children of God are we, and it was not yet manifested what we shall be, and we have known that if he may be manifested, like him we shall be, because we shall see him as he is;
Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3 and every one who is having this hope on him, doth purify himself, even as he is pure.
Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4 Every one who is doing the sin, the lawlessness also he doth do, and the sin is the lawlessness,
Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5 and ye have known that he was manifested that our sins he may take away, and sin is not in him;
Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6 every one who is remaining in him doth not sin; every one who is sinning, hath not seen him, nor known him.
Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7 Little children, let no one lead you astray; he who is doing the righteousness is righteous, even as he is righteous,
Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8 he who is doing the sin, of the devil he is, because from the beginning the devil doth sin; for this was the Son of God manifested, that he may break up the works of the devil;
Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9 every one who hath been begotten of God, sin he doth not, because his seed in him doth remain, and he is not able to sin, because of God he hath been begotten.
Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10 In this manifest are the children of God, and the children of the devil; every one who is not doing righteousness, is not of God, and he who is not loving his brother,
Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11 because this is the message that ye did hear from the beginning, that we may love one another,
Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12 not as Cain — of the evil one he was, and he did slay his brother, and wherefore did he slay him? because his works were evil, and those of his brother righteous.
Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13 Do not wonder, my brethren, if the world doth hate you;
Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14 we — we have known that we have passed out of the death to the life, because we love the brethren; he who is not loving the brother doth remain in the death.
Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15 Every one who is hating his brother — a man-killer he is, and ye have known that no man-killer hath life age-during in him remaining, (aiōnios g166)
Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios g166)
16 in this we have known the love, because he for us his life did lay down, and we ought for the brethren the lives to lay down;
Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17 and whoever may have the goods of the world, and may view his brother having need, and may shut up his bowels from him — how doth the love of God remain in him?
Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18 My little children, may we not love in word nor in tongue, but in word and in truth!
Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19 and in this we know that of the truth we are, and before Him we shall assure our hearts,
Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20 because if our heart may condemn — because greater is God than our heart, and He doth know all things.
Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21 Beloved, if our heart may not condemn us, we have boldness toward God,
Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22 and whatever we may ask, we receive from Him, because His commands we keep, and the things pleasing before Him we do,
na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23 and this is His command, that we may believe in the name of His Son Jesus Christ, and may love one another, even as He did give command to us,
Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24 and he who is keeping His commands, in Him he doth remain, and He in him; and in this we know that He doth remain in us, from the Spirit that He gave us.
Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.

< 1 John 3 >