< 1 Chronicles 27 >

1 And the sons of Israel, after their number, heads of the fathers, and princes of the thousands and of the hundreds, and their officers, those serving the king in any matter of the courses, that are coming in and going out month by month, throughout all months of the year — [are] in each course twenty and four thousand.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Over the first course, for the first month, [is] Jashobeam son of Zabdiel, and on his course [are] twenty and four thousand;
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 of the sons of Perez [is] the head of all princes of the hosts for the first month.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 And over the course of the second month [is] Dodai the Ahohite, and his course, and Mikloth [is] the president, and on his course [are] twenty and four thousand.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 Head of the third host, for the third month, [is] Benaiah son of Jehoiada, the head priest, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 This Benaiah [is] a mighty one of the thirty, and over the thirty, and [in] his course [is] Ammizabad his son.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 The fourth, for the fourth month, [is] Asahel brother of Joab, and Zebadiah his son after him, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 The fifth, for the fifth month, [is] the prince Shamhuth the Izrahite, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 The sixth, for the sixth month, [is] Ira son of Ikkesh the Tekoite, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 The seventh, for the seventh month, [is] Helez the Pelonite, of the sons of Ephraim, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 The eighth, for the eighth month, [is] Sibbecai the Hushathite, of the Zarhite, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 The ninth, for the ninth month, [is] Abiezer the Antothite, of the Benjamite, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 The tenth, for the tenth month, [is] Maharai the Netophathite, of the Zarhite, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 Eleventh, for the eleventh month, [is] Benaiah the Pirathonite, of the sons of Ephraim, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 The twelfth, for the twelfth month, [is] Heldai the Netophathite, of Othniel, and on his course [are] twenty and four thousand.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 And over the tribes of Israel: Of the Reubenite, a leader [is] Eliezer son of Zichri; of the Simeonite, Shephatiah son of Maachah;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 of the Levite, Hashabiah son of Kemuel; of the Aaronite, Zadok;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 of Judah, Elihu, of the brethren of David; of Issachar, Omri son of Michael;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 of Zebulun, Ishmaiah son of Obadiah; of Naphtali, Jerimoth son of Azriel;
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 of the sons of Ephraim, Hoshea son of Azaziah; of the half of the tribe of Manasseh, Joel son of Pedaiah;
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 of the half of Manasseh in Gilead, Iddo son of Zechariah; of Benjamin, Jaasiel son of Abner; of Dan, Azareel son of Jeroham:
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 these [are] heads of the tribes of Israel.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 And David hath not taken up their number from a son of twenty years and under, for Jehovah said to multiply Israel as the stars of the heavens.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Joab son of Zeruiah hath begun to number — and hath not finished — and there is for this wrath against Israel, and the number hath not gone up in the account of the Chronicles of king David.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 And over the treasures of the king [is] Azmaveth son of Adiel; and over the treasures in the field, in the cities, and in the villages, and in the towers, [is] Jehonathan son of Uzziah;
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 and over workmen of the field for the service of the ground [is] Ezri son of Chelub;
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 and over the vineyards [is] Shimei the Ramathite; and over what [is] in the vineyards for the treasures of wine [is] Zabdi the Shiphmite;
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 and over the olives, and the sycamores, that [are] in the low country, [is] Baal-Hanan the Gederite; and over the treasures of oil [is] Joash;
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 and over the herds that are feeding in Sharon [is] Shitrai the Sharonite; and over the herds in the valleys [is] Shaphat son of Adlai;
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 and over the camels [is] Obil the Ishmeelite; and over the asses [is] Jehdeiah the Meronothite;
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 and over the flock [is] Jaziz the Hagerite; all these [are] heads of the substance that king David hath.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 And Jonathan, uncle of David, [is] counsellor, a man of understanding, he is also a scribe; and Jehiel son of Hachmoni [is] with the sons of the king;
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 and Ahithophel [is] counsellor to the king; and Hushai the Archite [is] the friend of the king;
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 and after Ahithophel [is] Jehoiada son of Benaiah, and Abiathar; and the head of the host of the king [is] Joab.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

< 1 Chronicles 27 >