< Titus 1 >
1 Poul, the seruaunt of God, and apostle of Jhesu Crist, bi the feith of the chosun of God, and bi the knowing of the treuthe, whiche is aftir pitee,
Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
2 in to the hope of euerlastinge lijf, which lijf God that lieth not, bihiyte bifore tymes of the world; (aiōnios )
ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati, (aiōnios )
3 but he hath schewid in hise tymes his word in preching, that is bitakun to me bi the comaundement of `God oure sauyour,
na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
4 to Tite, most dereworthe sone bi the comyn feith, grace and pees of God the fadir, and of Crist Jhesu, oure sauyour.
Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
5 For cause of this thing Y lefte thee at Crete, that thou amende tho thingis that failen, and ordeyne preestis bi citees, as also Y disposide to thee.
Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
6 If ony man is withoute cryme, an hosebonde of o wijf, and hath feithful sones, not in accusacioun of letcherie, or not suget.
mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
7 For it bihoueth a bischop to be without cryme, a dispendour of God, not proud, not wrathful, not drunkelew, not smytere, not coueytouse of foul wynnyng;
Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
8 but holdinge hospitalite, benygne, prudent, sobre, iust,
Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
9 hooli, contynent, takinge that trewe word, that is aftir doctryn; that he be miyti to amoneste in hoolsum techyng, and to repreue hem that ayenseien.
Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
10 For ther ben many vnobedient, and veyn spekeris, and disseyueris, moost thei that ben of circumcisyoun,
Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
11 whiche it bihoueth to be repreued; whiche subuerten alle housis, techinge whiche thingis it bihoueth not, for the loue of foul wynnyng.
Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
12 And oon of hem, her propre profete, seide, Men of Crete ben euere more lyeris, yuele beestis, of slowe wombe.
Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: “Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!”
13 This witnessyng is trewe. For what cause blame hem sore, that thei be hool in feith,
Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
14 not yyuynge tent to fablis of Jewis, and to maundementis of men, that turnen awei hem fro treuthe.
Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
15 And alle thingis ben clene to clene men; but to vnclene men and to vnfeithful no thing is clene, for the soule and conscience of hem ben maad vnclene.
Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
16 Thei knoulechen that thei knowen God, but bi dedis thei denyen; whanne thei ben abhominable, and vnbileueful, and repreuable to al good werk.
Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.