< Ruth 4 >

1 Therfor Booz stiede to the yate, and sat there; and whanne he hadde seyn the kynesman passe forth, of whom the word was had, Booz seide to hym, Bowe thou a litil, and sitte here; and he clepide hym bi his name. And he turnede, and sat.
Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
2 Forsothe Booz took ten `men of the eldere men of the citee, and seide to hem, Sitte ye here.
Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
3 And while thei saten, Booz spak to the kynesman, Noemy, that turnede ayen fro the cuntrey of Moab, seelde the part of the feeld of oure brother Elymelech,
Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
4 which thing Y wolde that thou here; and Y wolde seie to thee bifor alle `men syttynge and grettere in birthe of my puple. If thou wolt haue in possessioun the feeld bi riyt of nyy kyn, bye thou, and `haue thou in possessioun; sotheli if it displesith thee, schewe thou this same thing to me, that Y wyte what Y `owe to do; for noon is niy in kyn, outakun thee which art the formere, and outakun me which am the secunde. And he answeride, Y schal bie the feeld.
Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
5 To whom Booz seide, Whanne thou hast bouyte the feeld of the `hond of the womman, thou owist `to take also Ruth of Moab, that was the wijf of the deed man, that thou reise the name of thi kynesman in his eritage.
Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
6 Which answeride, Y forsake the ryyt of nyy kyn; for Y owe not to do awei the eritage of my meynee; vse thou my priuelegie, which priuelegie Y knowleche me to wante gladli.
Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
7 Forsothe this was the custom bi eld tyme in Israel among kynesmen, that if a man yaf his riyt to anothir man, that the grauntyng were stidefast, the man vnlaase his scho, and yaf to his kynesman; this was the witnessyng of the yift in Israel.
(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
8 Therfor Booz seide to his kynesman, Take the scho fro thee; `which scho he vnlaside anoon fro his foot.
Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
9 And Booz seide to the grettere men in birthe and to al the puple, Ye ben witnessis to dai, that Y haue take in possessioun alle thingis that weren of Elymelech, and of Chelion, and of Maalon, bi the yifte of Noemy;
Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
10 and that Y haue take in to wedlok Ruth of Moab, the wijf of Maalon, that Y reise the name of the deed man in his erytage; lest his name be doon awey fro his meynee and britheren and puple. Ye, he seide, ben witnessis of this thing.
Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
11 Al the puple, that was in the yate, answeride, and the grettere men in birthe answeriden, We ben witnessis; the Lord make this womman, that entrith in to thin hows, as Rachel and Lia, that bildiden the hows of Israel, that sche be ensaumple of vertu in Effrata, and haue a solempne name in Bethleem;
Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
12 and thin hows be maad as the hows of Fares, whom Thamar childide to Judas, of the seed which the Lord schal yyue to thee of this damesel.
Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
13 Therfor Booz took Ruth, and took hir to wijf; and he entride to hir, and the Lord yaf to hir, that sche conseyuede, `and childide a sone.
Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
14 And wymmen seiden to Noemy, Blessid be the Lord, which `suffride not, that an eir failide to thi meynee, and his name were clepid in Israel;
Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
15 and that thou haue `a man, that schal coumforte thi soule, and nursche elde age. For a child is borun of thi douytir in lawe, `which child schal loue thee, and he is myche betere to thee, than if thou haddist seuene sones.
Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
16 And Noemy puttide the child resseyued in hir bosum; and sche dide the office of a nurische, and of a berere.
Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
17 Forsothe wymmen neiyboris thankiden hir, and seiden, A sone is borun to Noemy, and clepide his name Obeth. This is the fadir of Ysay, fadir of Dauid.
Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
18 These ben the generaciouns of Fares; Fares gendride Esrom;
Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
19 Esrom gendride Aram; Aram gendride Amynadab;
Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 Amynadab gendride Naason; Naason gendride Salmon; Salmon gendride Booz;
Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 Booz gendride Obeth;
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 Obeth gendride Isay; Isay gendride Dauid the kyng.
Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >