< Romans 6 >

1 Therfor what schulen we seie? Schulen we dwelle in synne, that grace be plenteuouse?
Tuseme nini basi? Je, tuendelee kutenda dhambi ili neema ipate kuongezeka?
2 God forbede. For hou schulen we that ben deed to synne, lyue yit ther ynne?
La hasha! Sisi tulioifia dhambi, tutawezaje kuendelea kuishi tena katika dhambi?
3 Whether, britheren, ye knowen not, that whiche euere we ben baptisid in Crist Jhesu, we ben baptisid in his deth?
Au hamjui ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
4 For we ben togidere biried with hym bi baptym `in to deth; that as Crist aroos fro deth bi the glorie of the fadir, so walke we in a newnesse of lijf.
Kwa hiyo tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa utukufu wa Baba, vivyo hivyo sisi nasi pia tupate kuenenda katika upya wa uzima.
5 For if we plauntid togidere ben maad to the licnesse of his deth, also we schulen be of the licnesse of his risyng ayen;
Kwa maana ikiwa tumeungana naye katika mauti yake, bila shaka tutaungana naye katika ufufuo wake.
6 witynge this thing, that oure olde man is crucified togidere, that the bodi of synne be distruyed, that we serue no more to synne.
Kwa maana twajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja naye ili ule mwili wa dhambi upate kuangamizwa, nasi tusiendelee kuwa tena watumwa wa dhambi.
7 For he that is deed, is iustefied fro synne.
Kwa maana mtu yeyote aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.
8 And if we ben deed with Crist, we bileuen that also we schulen lyue togidere with hym;
Basi ikiwa tulikufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba pia tutaishi pamoja naye.
9 witinge for Crist, rysynge ayen fro deth, now dieth not, deeth schal no more haue lordschip on hym.
Kwa maana tunajua kwamba Kristo, kwa sababu alifufuliwa kutoka kwa wafu, hawezi kufa tena; mauti haina tena mamlaka juu yake.
10 For that he was deed to synne, he was deed onys; but that he lyueth, he liueth to God.
Kifo alichokufa, aliifia dhambi mara moja tu, lakini uzima alio nao anamwishia Mungu.
11 So ye deme you silf to be deed to synne, but lyuynge to God in `Jhesu Crist oure Lord.
Vivyo hivyo, jihesabuni wafu katika dhambi lakini mlio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
12 Therfor regne not synne in youre deedli bodi, that ye obeische to hise coueityngis.
Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya.
13 Nether yyue ye youre membris armuris of wickidnesse to synne, but yyue ye you silf to God, as thei that lyuen of deed men, and youre membris armuris of riytwisnesse to God.
Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu kwake kama vyombo vya haki.
14 For synne schal not haue lordschipe on you; for ye ben not vndur the lawe, but vndur grace.
Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema.
15 What therfor? Schulen we do synne, for we ben not vndur the lawe, but vndur grace?
Ni nini basi? Je, tutende dhambi kwa kuwa hatuko chini ya sheria bali chini ya neema? La, hasha!
16 God forbede. Witen ye not, that to whom ye yyuen you seruauntis to obeie to, ye ben seruauntis of that thing, to which ye han obeschid, ether of synne to deth, ether of obedience to riytwisnesse?
Je, hamjui kwamba mnapojitoa kwa mtu yeyote kama watumwa watiifu, ninyi ni watumwa wa yule mnayemtii, aidha watumwa wa dhambi, ambayo matokeo yake ni mauti, au watumwa wa utii ambao matokeo yake ni haki?
17 But Y thanke God, that ye weren seruauntis of synne; but ye han obeischid of herte in to that fourme of techyng, in which ye ben bitakun.
Lakini Mungu ashukuriwe kwa kuwa ninyi ambao kwanza mlikuwa watumwa wa dhambi, mmekuwa watii kutoka moyoni kwa mafundisho mliyopewa.
18 And ye delyuered fro synne, ben maad seruauntis of riytwisnesse.
Nanyi, mkiisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mmekuwa watumwa wa haki.
19 Y seie that thing that is of man, for the vnstidefastnesse of youre fleisch. But as ye han youun youre membris to serue to vnclennesse, and to wickidnesse `in to wickidnesse, so now yyue ye youre membris to serue to riytwisnesse in to hoolynesse.
Ninasema kwa namna ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wenu wa hali ya asili. Kama vile mlivyokuwa mkivitoa viungo vya miili yenu kama watumwa wa mambo machafu na uovu uliokuwa ukiongezeka zaidi, hivyo sasa vitoeni viungo vyenu kama watumwa wa haki inayowaelekeza mpate kutakaswa.
20 For whanne ye weren seruauntis of synne, ye weren fre of riytfulnesse.
Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa hamtawaliwi na haki.
21 Therfor what fruyt hadden ye thanne in tho thingis, in whiche ye schamen now? For the ende of hem is deth.
Lakini mlipata faida gani kwa mambo hayo ambayo sasa mnayaonea aibu? Mwisho wa mambo hayo ni mauti.
22 But now ye delyuered fro synne, and maad seruauntis to God, han your fruyt in to holinesse, and the ende euerlastinge lijf. (aiōnios g166)
Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakatifu, ambao mwisho wake ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
23 For the wagis of synne is deth; the grace of God is euerlastynge lijf in Crist Jhesu our Lord. (aiōnios g166)
Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios g166)

< Romans 6 >