< Revelation 9 >

1 And the fyuethe aungel trumpide; and Y say, that a sterre hadde falle doun fro heuene in to erthe; and the keye of the pit of depnesse was youun to it. (Abyssos g12)
Kisha malaika wa tano alipiga tarumbeta yake. Niliona nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka kwenye dunia. Nyota ilipewa ufunguo wa shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
2 And it openede the pit of depnesse, and a smoke of the pit stiede vp, as the smoke of a greet furneis; and the sunne was derkid, and the eir, of the smoke of the pit. (Abyssos g12)
Alifungua shimo lisilo na kikomo, na moshi ukapanda juu kwa safu kutoka ndani ya shimo kama moshi kutoka katika tanuru kubwa. Jua na anga vilibadilika vikawa giza kwa sababu ya moshi uliotoka shimoni. (Abyssos g12)
3 And locustis wenten out of the smoke of the pit in to erthe; and power was youun to hem, as scorpiouns of the erthe han power.
Ndani ya moshi nzige walitoka kuja juu ya dunia, nao walipewa nguvu kama ile ya nge juu ya dunia.
4 And it was comaundid to hem, that thei schulden not hirte the gras of erthe, nether ony grene thing, nether ony tre, but oneli men, that han not the signe of God in her forhedis.
Waliambiwa kutokudhuru majani katika nchi au mmea wowote wa kijani au mti, isipokuwa tu watu ambao hawakuwa na muhuri wa Mungu katika paji za nyuso zao.
5 And it was youun to hem, that thei schulden not sle hem, but that thei schulden `be turmentid fyue monethis; and the turmentyng of hem, as the turmentyng of a scorpioun, whanne he smytith a man.
Hawakupewa ruhusa ya kuwaua hao watu, bali kuwatesa tu kwa miezi mitano. Uchungu wao ulikuwa kama ule wa kuumwa na nge amwumapo mtu.
6 And in tho daies men schulen seke deth, and thei schulen not fynde it; and thei schulen desire to die, and deth schal fle fro hem.
Katika siku hizo watu watatafuta kifo, lakini hawatakipata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
7 And the licnesse of locustis ben lijk horsis maad redi `in to batel; and on the heedis of hem as corouns lijk gold, and the facis of hem as the faces of men.
Nzige walifanana na farasi walioandaliwa kwa vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji ya dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8 And thei hadden heeris, as heeris of wymmen; and the teeth of hem weren as teeth of liouns.
Walikuwa na nywele kama za wanawake na meno yao yalikuwa kama ya simba.
9 And thei hadden haburiouns, as yren haburiouns, and the vois of her wengis as the vois of charis of many horsis rennynge `in to batel.
Walikuwa na vifua kama vifua vya chuma na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari mengi ya vita na farasi wakimbiao kwenda vitani.
10 And thei hadden tailis lijk scorpiouns, and prickis weren in the tailis of hem; and the myyt of hem was to noye men fyue monethis.
Walikuwa na mikia inayouma kama nge; katika mikia yao walikuwa na nguvu ya kudhuru watu kwa miezi mitano.
11 And thei hadden on hem a kyng, the aungel of depnesse, to whom the name bi Ebrew is Laabadon, but bi Greek Appollion, and bi Latyn `he hath a name `Extermynans, that is, a distriere. (Abyssos g12)
Walikuwa naye kama mfalme juu yao malaika wa shimo lisilokuwa na mwisho. Jina lake katika Kiebrania ni Abadoni, na katika Kiyunani ana jina Apolioni. (Abyssos g12)
12 O wo is passid, and lo! yit comen twei woes.
Ole ya kwanza imepita. Angalia! Baada ya hili kuna maafa mawili yaja.
13 Aftir these thingis also the sixte aungel trumpide; and Y herde a vois fro foure corneris of the goldun auter, that is bifore the iyen of God,
Malaika wa sita alipiga tarumbeta yake, na nikasikia sauti ikitoka katika pembe ya madhabahu ya dhahabu ambayo iko mbele za Mungu.
14 and seide to the sixte aungel that hadde a trumpe, Vnbynde thou foure aungels, that ben boundun in the greet flood Eufrates.
Sauti ilimwambia malaika wa sita aliyekuwa na tarumbeta, “Waachie malaika wanne ambao wamefungwa katika mto mkubwa Efrata.”
15 And the foure aungels weren vnboundun, whiche weren redi in to our, and dai, and monethe, and yeer, to sle the thridde part of men.
Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa kwa saa hiyo maalumu, siku hiyo, mwezi huo, na mwaka huo, waliachiwa wawaue theluthi ya wanadamu.
16 And the noumbre of the oost of horse men was twenti thousynde sithis ten thousynde. Y herde the noumbre of hem.
Idadi ya maaskari waliokuwa juu ya farasi ilikuwa 200, 000, 000. Nilisikia idadi yao.
17 And so Y say horsis in visioun; and thei that saten on hem hadden firy haburiouns, and of iacynt, and of brymstoon. And the heedis of the horsis weren as heedis of liouns; and fier, and smoke, and brymston, cometh forth of the mouth of hem.
Hivi ndivyo nilivyoona farasi katika maono yangu na wale waliopanda juu yao: Vifua vyao vilikuwa vyekundu kama moto, bluu iliyoiva na njano isiyoiva. Vichwa vya farasi vilifanana na vichwa vya simba, na midomoni mwao ulitoka moto, moshi na salfa.
18 Of these thre plagis the thridde part of men was slayn, of the fier, and of the smoke, and of the brymston, that camen out of the mouth of hem.
Theluthi ya wanadamu waliuawa na haya mapigo matatu: moto, moshi, na salfa iliyotoka katika midomo yao.
19 For the power of the horsis is in the mouth of hem, and in the tailis of hem; for the tailis of hem ben lyk to serpentis, hauynge heedis, and in hem thei noyen.
Kwa kuwa nguvu ya farasi ilikuwa katika midomo yao na katika mikia yao—kwa kuwa mikia yao ilikuwa kama nyoka, na walikuwa na vichwa ambavyo walitumia kuwatia majeraha wanadamu.
20 And the tothir men, that weren not slayn in these plagis, nether dyden penaunce of the werkis of her hondis, that thei worschipeden not deuelis, and simylacris of gold, and of siluer, and of bras, and of stoon, and of tre, whiche nethir mown se, nether heere, nether wandre;
Watu waliobaki, wale ambao walikuwa hawajauawa na mapigo haya, hawakutubia matendo yao waliyokuwa wamefanya, wala hawakuacha kuabudu mapepo na miungu ya dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti—vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia au kutembea.
21 and diden not penaunce of her mansleyngis, nether of her witchecraftis, nethir of her fornicacioun, nethir of her theftis, weren slayn.
Wala hawakutubia uuaji wao, uchawi wao, uasherati wao au njia zao za wizi.

< Revelation 9 >