< Revelation 14 >
1 And Y sai, and lo! lomb stood on the mount of Sion, and with hym an hundrid thousynde and foure and fourti thousynde, hauynge his name, and the name of his fadir writun in her forhedis.
Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
2 And Y herde a vois fro heuene, as the vois of many watris, and as the vois of a greet thundur; and the vois which is herd, was as of many harperis harpinge in her harpis.
Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
3 And thei sungun as a newe song bifor the seete of God, and bifore the foure beestis, and senyouris. And no man miyte seie the song, but thei an hundrid thousynde and foure and fourti thousynde, that ben bouyt fro the erthe.
Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
4 These it ben, that ben not defoulid with wymmen; for thei ben virgyns. These suen the lomb, whidir euer he schal go; these ben bouyt of alle men, the firste fruytis to God, and to the lomb;
Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
5 and in the mouth of hem lesyng is not foundun; for thei ben with out wem bifor the trone of God.
Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
6 And Y say another aungel, fliynge bi the myddil of heuene, hauynge an euerlastinge gospel, that he schulde preche to men sittynge on erthe, and on ech folk, and lynage, and langage, and puple; (aiōnios )
Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios )
7 and seide with a greet vois, Drede ye the Lord, and yyue ye to hym onour, for the our of his dom cometh; and worschipe ye hym, that made heuene and erthe, the see, and alle thingis that ben in hem, and the wellis of watris.
Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
8 And anothir aungel suede, seiynge, Thilke greet Babiloyne fel doun, fel doun, which yaf drinke to alle folkis of the wyn of wraththe of her fornycacioun.
Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
9 And the thridde aungel suede hem, and seide with a greet vois, If ony man worschipe the beeste, and the ymage of it, and takith the carecter in his forheed, ether in his hoond,
Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
10 this schal drynke of the wyn of Goddis wraththe, that is meynd with clere wyn in the cuppe of his wraththe, and schal be turmentid with fier and brymston, in the siyt of hooli aungels, and bifore the siyt of the lomb.
yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
11 And the smoke of her turmentis schal stie vp in to the worldis of worldis; nether thei han reste dai and niyt, whiche worschipiden the beeste and his ymage, and yf ony man take the carect of his name. (aiōn )
Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn )
12 Here is the pacience of seyntis, whiche kepen the maundementis of God, and the feith of Jhesu.
Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
13 And Y herde a vois fro heuene, seiynge to me, Write thou, Blessid ben deed men, that dien in the Lord; fro hennus forth now the spirit seith, that thei reste of her traueilis; for the werkis of hem suen hem.
Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
14 And Y say, and lo! a white cloude, and aboue the cloude a sittere, lijk the sone of man, hauynge in his heed a goldun coroun, and in his hond a scharp sikil.
Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
15 And another aungel wente out of the temple, and criede with greet vois to hym that sat on the cloude, Sende thi sikil, and repe, for the our cometh, that it be ropun; for the corn of the erthe is ripe.
Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
16 And he that sat on the cloude, sente his sikil in to the erthe, and rap the erthe.
Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
17 And another aungel wente out of the temple, that is in heuene, and he also hadde a scharp sikile.
Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
18 And another aungel wente out fro the auter, that hadde power on fier and water; and he criede with a greet vois to hym that hadde the scharp sikil, and seide, Sende thi scharp sikil, and kitte awei the clustris of the vynyerd of the erthe, for the grapis of it ben ripe.
Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
19 And the aungel sente his sikil in to the erthe, and gaderide grapis of the vynyerd of the erthe, and sente into the greet lake of Goddis wraththe.
Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
20 And the lake was troddun without the citee, and the blood wente out of the lake til to the `bridels of horsis, bi furlongis a thousynd and six hundrid.
Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.