< Psalms 88 >

1 The song of salm, to the sones of Chore, to victorie on Mahalat, for to answere, the lernyng of Heman Ezraite. Lord God of myn helthe; Y criede in dai and nyyt bifore thee.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 Mi preier entre bifore thi siyt; bowe doun thin eere to my preier.
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 For my soule is fillid with yuels; and my lijf neiyede to helle. (Sheol h7585)
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
4 I am gessid with hem that goon doun in to the lake; Y am maad as a man with outen help,
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 and fre among deed men. As men woundid slepinge in sepulcris, of whiche men noon is myndeful aftir; and thei ben put awei fro thin hond.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 Thei han put me in the lower lake; in derke places, and in the schadewe of deth.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Thi strong veniaunce is confermed on me; and thou hast brouyt in alle thi wawis on me.
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 Thou hast maad fer fro me my knowun; thei han set me abhomynacioun to hem silf. I am takun, and Y yede not out;
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 myn iyen weren sijk for pouert. Lord, Y criede to thee; al dai Y spredde abrood myn hondis to thee.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 Whethir thou schalt do merueils to deed men; ether leechis schulen reise, and thei schulen knouleche to thee?
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 Whether ony man in sepulcre schal telle thi merci; and thi treuthe in perdicioun?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 Whether thi merueilis schulen be knowun in derknessis; and thi riytfulnesse in the lond of foryetyng?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 And, Lord, Y criede to thee; and erli my preier schal bifor come to thee.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 Lord, whi puttist thou awei my preier; turnest awei thi face fro me?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 I am pore, and in traueils fro my yongthe; sotheli Y am enhaunsid, and Y am maad low, and disturblid.
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 Thi wraththis passiden on me; and thi dredis disturbliden me.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 Thei cumpassiden me as watir al dai; thei cumpassiden me togidere.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 Thou madist fer fro me a frend and neiybore; and my knowun fro wretchidnesse.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

< Psalms 88 >