< Psalms 73 >
1 `The salm of Asaph. God of Israel is ful good; to hem that ben of riytful herte.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 But my feet weren moued almeest; my steppis weren sched out almeest.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 For Y louede feruentli on wickid men; seynge the pees of synneris.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 For biholdyng is not to the deth of hem; and stidefastnesse in the sikenesse of hem.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 Thei ben not in the trauel of men; and thei schulen not be betun with men.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Therfore pride helde hem; thei weren hilid with her wickidnesse and vnfeithfulnesse.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 The wickidnesse of hem cam forth as of fatnesse; thei yeden in to desire of herte.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Thei thouyten and spaken weiwardnesse; thei spaken wickidnesse an hiy.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Thei puttiden her mouth in to heuene; and her tunge passide in erthe.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Therfor my puple schal be conuertid here; and fulle daies schulen be foundun in hem.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 And thei seiden, How woot God; and whether kunnyng is an heiye, `that is, in heuene?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Lo! thilke synneris and hauynge aboundance in the world; helden richessis.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 And Y seide, Therfor without cause Y iustifiede myn herte; and waischide myn hoondis among innocentis.
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 And Y was betun al dai; and my chastisyng was in morutidis.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 If Y seide, Y schal telle thus; lo! Y repreuede the nacioun of thi sones.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 I gesside, that Y schulde knowe this; trauel is bifore me.
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Til Y entre in to the seyntuarie of God; and vndurstonde in the last thingis of hem.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Netheles for gilis thou hast put to hem; thou castidist hem doun, while thei weren reisid.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 Hou ben thei maad into desolacioun; thei failiden sodeynli, thei perischiden for her wickidnesse.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 As the dreem of men that risen; Lord, thou schalt dryue her ymage to nouyt in thi citee.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 For myn herte is enflaumed, and my reynes ben chaungid;
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 and Y am dryuun to nouyt, and Y wiste not.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 As a werk beeste Y am maad at thee; and Y am euere with thee.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Thou heldist my riythond, and in thi wille thou leddist me forth; and with glorie thou tokist me vp.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 For whi what is to me in heuene; and what wolde Y of thee on erthe?
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Mi fleische and myn herte failide; God of myn herte, and my part is God withouten ende.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 For lo! thei that drawen awei fer hem silf fro thee, `bi deedli synne, schulen perische; thou hast lost alle men that doen fornycacioun fro thee.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But it is good to me to cleue to God; and to sette myn hope in the Lord God. That Y telle alle thi prechyngis; in the yatis of the douyter of Syon.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.