< Psalms 64 >

1 `In Ebrewe thus, To the victorie, the salm of Dauid. `In Jerom `thus, To the ouercomer, the song of Dauid. God, here thou my preier, whanne Y biseche; delyuere thou my soule fro the drede of the enemy.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
2 Thou hast defendid me fro the couent of yuele doers; fro the multitude of hem that worchen wickidnesse.
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 For thei scharpiden her tungis as a swerd, thei benten a bowe, a bittir thing;
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 for to schete in priuetees hym that is vnwemmed.
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
5 Sodeynli thei schulen schete hym, and thei schulen not drede; thei maden stidefast to hem silf a wickid word. Thei telden, that thei schulden hide snaris; thei seiden, Who schal se hem?
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 Thei souyten wickidnessis; thei souyten, and failiden in sekinge. A man neiyhe to deep herte;
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 and God schal be enhaunsid. The arowis of `litle men ben maad the woundis of hem;
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
8 and the tungis of hem ben maad sijk ayens hem. Alle men ben disturblid, that sien hem;
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
9 and ech man dredde. And thei telden the werkis of God; and vndurstoden the dedis of God.
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
10 The iust man schal be glad in the Lord, and schal hope in hym; and alle men of riytful herte schulen be preisid.
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

< Psalms 64 >