< Psalms 41 >

1 For victorie, the song of Dauid. Blessid is he that vndurstondith `on a nedi man and pore; the Lord schal delyuere hym in the yuel dai.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 The Lord kepe hym, and quykene hym, and make hym blesful in the lond; and bitake not hym in to the wille of his enemyes.
Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 The Lord bere help to hym on the bed of his sorewe; thou hast ofte turned al his bed stre in his sijknesse.
Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
4 I seide, Lord, haue thou mercy on me; heele thou my soule, for Y synnede ayens thee.
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5 Myn enemyes seiden yuels to me; Whanne schal he die, and his name schal perische?
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6 And if he entride for to se, he spak veyn thingis; his herte gaderide wickidnesse to hym silf.
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7 He yede with out forth; and spak to the same thing. Alle myn enemyes bacbitiden pryuyli ayens me; ayens me thei thouyten yuels to me.
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8 Thei ordeineden an yuel word ayens me; Whether he that slepith, schal not leie to, that he rise ayen?
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9 For whi the man of my pees, in whom Y hopide, he that eet my looues; made greet disseit on me.
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
10 But thou, Lord, haue merci on me, and reise me ayen; and Y schal yelde to hem.
Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11 In this thing Y knew, that thou woldist me; for myn enemye schal not haue ioye on me.
Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12 Forsothe thou hast take me vp for ynnocence; and hast confermed me in thi siyt with outen ende.
Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
13 Blessid be the Lord God of Israel, fro the world and in to the world; be it doon, be it doon.
Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.

< Psalms 41 >