< Psalms 34 >

1 To Dauid, whanne he chaungide his mouth bifor Abymalech, and he `droof out Dauid, `and he yede forth. I schal blesse the Lord in al tyme; euere his heriyng is in my mouth.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Mi soule schal be preisid in the Lord; mylde men here, and be glad.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Magnyfie ye the Lord with me; and enhaunse we his name into it silf.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 I souyte the Lord, and he herde me; and he delyueride me fro alle my tribulaciouns.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Neiye ye to him, and be ye liytned; and youre faces schulen not be schent.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 This pore man criede, and the Lord herde hym; and sauyde hym fro alle hise tribulaciouns.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 The aungel of the Lord sendith in the cumpas of men dredynge hym; and he schal delyuere hem.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Taaste ye, and se, for the Lord is swete; blessid is the man, that hopith in hym.
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Alle ye hooli men of the Lord, drede hym; for no nedynesse is to men dredynge hym.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Riche men weren nedi, and weren hungri; but men that seken the Lord schulen not faile of al good.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Come, ye sones, here ye me; Y schal teche you the drede of the Lord.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Who is a man, that wole lijf; loueth to se good daies?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Forbede thi tunge fro yuel; and thi lippis speke not gile.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Turne thou awei fro yuel, and do good; seke thou pees, and perfitli sue thou it.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 The iyen of the Lord ben on iust men; and hise eeren ben to her preiers.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 But the cheer of the Lord is on men doynge yuels; that he leese the mynde of hem fro erthe.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Just men cryeden, and the Lord herde hem; and delyueride hem fro alle her tribulaciouns.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 The Lord is nyy hem that ben of troblid herte; and he schal saue meke men in spirit.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Many tribulaciouns ben of iust men; and the Lord schal delyuere hem fro alle these.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 The Lord kepith alle the boonys of hem; oon of tho schal not be brokun.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 The deth of synneris is werst; and thei that haten a iust man schulen trespasse.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 The Lord schal ayenbie the soulis of hise seruauntis; and alle, that hopen in him, schulen not trespasse.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalms 34 >