< Psalms 30 >

1 The salm of song, for the halewyng of the hows of Dauid. Lord, Y schal enhaunse thee, for thou hast vp take me; and thou delitidist not myn enemyes on me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Mi Lord God, Y criede to thee; and thou madist me hool.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Lord, thou leddist out my soule fro helle; thou sauedist me fro hem that goen doun into the lake. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Ye seyntis of the Lord, synge to the Lord; and knowleche ye to the mynde of his hoolynesse.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 For ire is in his indignacioun; and lijf is in his wille. Wepyng schal dwelle at euentid; and gladnesse at the morewtid.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Forsothe Y seide in my plentee; Y schal not be moued with outen ende.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Lord, in thi wille; thou hast youe vertu to my fairnesse. Thou turnedist awei thi face fro me; and Y am maad disturblid.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Lord, Y schal crye to thee; and Y schal preye to my God.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 What profit is in my blood; while Y go doun in to corrupcioun? Whether dust schal knouleche to thee; ethir schal telle thi treuthe?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 The Lord herde, and hadde merci on me; the Lord is maad myn helpere.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Thou hast turned my weilyng in to ioye to me; thou hast to-rent my sak, and hast cumpassid me with gladnesse.
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 That my glorie synge to thee, and Y be not compunct; my Lord God, Y schal knouleche to thee with outen ende.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Psalms 30 >