< Psalms 2 >

1 Whi gnastiden with teeth hethene men; and puplis thouyten veyn thingis?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 The kyngis of erthe stoden togidere; and princes camen togidere ayens the Lord, and ayens his Crist?
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 Breke we the bondis of hem; and cast we awei the yok of hem fro vs.
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 He that dwellith in heuenes schal scorne hem; and the Lord schal bimowe hem.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Thanne he schal speke to hem in his ire; and he schal disturble hem in his stronge veniaunce.
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 Forsothe Y am maad of hym a kyng on Syon, his hooli hil; prechynge his comaundement.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 The Lord seide to me, Thou art my sone; Y haue gendrid thee to dai.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Axe thou of me, and Y schal yyue to thee hethene men thin eritage; and thi possessioun the termes of erthe.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Thou schalt gouerne hem in an yrun yerde; and thou schalt breke hem as the vessel of a pottere.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 And now, ye kyngis, vndurstonde; ye that demen the erthe, be lerud.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Serue ye the Lord with drede; and make ye ful ioye to hym with tremblyng.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Take ye lore; lest the Lord be wrooth sumtyme, and lest ye perischen fro iust waie. Whanne his `ire brenneth out in schort tyme; blessed ben alle thei, that tristen in hym.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

< Psalms 2 >