< Psalms 17 >
1 The preier of Dauid. Lord, here thou my riytfulnesse; biholde thou my preier. Perseuye thou with eeris my preier; not maad in gileful lippis.
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 Mi doom come `forth of thi cheer; thin iyen se equite.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 Thou hast preued myn herte, and hast visitid in niyt; thou hast examynyd me bi fier, and wickidnesse is not foundun in me.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 That my mouth speke not the werkis of men; for the wordis of thi lippis Y haue kept harde weies.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 Make thou perfit my goyngis in thi pathis; that my steppis be not moued.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 I criede, for thou, God, herdist me; bowe doun thin eere to me, and here thou my wordis.
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Make wondurful thi mercies; that makist saaf `men hopynge in thee.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Kepe thou me as the appil of the iye; fro `men ayenstondynge thi riyt hond. Keuere thou me vndur the schadewe of thi wyngis;
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 fro the face of vnpitouse men, that han turmentid me. Myn enemyes han cumpassid my soule;
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 thei han closide togidere her fatnesse; the mouth of hem spak pride.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 Thei castiden me forth, and han cumpassid me now; thei ordeyneden to bowe doun her iyen in to erthe.
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 Thei, as a lioun maad redi to prey, han take me; and as the whelp of a lioun dwellynge in hid places.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Lord, rise thou vp, bifor come thou hym, and disseyue thou hym; delyuere thou my lijf fro the `vnpitouse,
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 delyuere thou thi swerd fro the enemyes of thin hond. Lord, departe thou hem fro a fewe men of `the lond in the lijf of hem; her wombe is fillid of thin hid thingis. Thei ben fillid with sones; and thei leften her relifis to her litle children.
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 But Y in riytfulnesse schal appere to thi siyt; Y schal be fillid, whanne thi glorie schal appere.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.