< Psalms 113 >
1 Alleluya. Children, preise ye the Lord; preise ye the name of the Lord.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 The name of the Lord be blessid; fro this tyme now and til in to the world.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 Fro the risyng of the sunne til to the goyng doun; the name of the Lord is worthi to be preisid.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 The Lord is hiy aboue alle folkis; and his glorie is aboue heuenes.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is as oure Lord God, that dwellith in hiye thingis;
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 and biholdith meke thingis in heuene and in erthe?
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 Reisynge a nedi man fro the erthe; and enhaunsinge a pore man fro drit.
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 That he sette hym with princes; with the princes of his puple.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Which makith a bareyn womman dwelle in the hous; a glad modir of sones.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.