< Psalms 108 >

1 The song of `the salm of Dauid. Min herte is redi, God, myn herte is redi; Y schal singe, and Y schal seie salm in my glorie.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 My glorie, ryse thou vp, sautrie and harp, rise thou vp; Y schal rise vp eerli.
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 Lord, Y schal knouleche to thee among puplis; and Y schal seie salm to thee among naciouns.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 For whi, God, thi merci is greet on heuenes; and thi treuthe is til to the cloudis.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 God, be thou enhaunsid aboue heuenes; and thi glorie ouer al erthe.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 That thi derlingis be delyuerid, make thou saaf with thi riythond, and here me; God spak in his hooli.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 I schal make ful out ioye, and Y schal departe Siccimam; and Y schal mete the grete valei of tabernaclis.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Galaad is myn, and Manasses is myn; and Effraym is the vptaking of myn heed. Juda is my king; Moab is the caudron of myn hope.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 In to Ydume Y schal stretche forth my scho; aliens ben maad frendis to me.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Who schal lede me forth in to a stronge citee; who schal lede me forth til in to Idume?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Whether not thou, God, that hast put vs awei; and, God, schalt thou not go out in oure vertues?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Yyue thou help to vs of tribulacioun; for the heelthe of man is veyn.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 We schulen make vertu in God; and he schal bringe oure enemyes to nouyt.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Psalms 108 >