< Proverbs 26 >

1 As snow in somer, and reyn in heruest; so glorie is vnsemeli to a fool.
Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 For whi as a brid fliynge ouer to hiy thingis, and a sparowe goynge in to vncerteyn; so cursing brouyt forth with out resonable cause schal come aboue in to sum man.
Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 Beting to an hors, and a bernacle to an asse; and a yerde in the bak of vnprudent men.
Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 Answere thou not to a fool bi his foli, lest thou be maad lijk hym.
Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Answere thou a fool bi his fooli, lest he seme to him silf to be wijs.
Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 An haltinge man in feet, and drinkinge wickidnesse, he that sendith wordis by a fonned messanger.
Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 As an haltinge man hath faire leggis in veyn; so a parable is vnsemeli in the mouth of foolis.
Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 As he that casteth a stoon in to an heep of mercurie; so he that yyueth onour to an vnwijs man.
Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 As if a thorn growith in the hond of a drunkun man; so a parable in the mouth of foolis.
Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10 Doom determyneth causis; and he that settith silence to a fool, swagith iris.
Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11 As a dogge that turneth ayen to his spuyng; so is an vnprudent man, that rehersith his fooli.
Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12 Thou hast seyn a man seme wijs to hym silf; an vnkunnyng man schal haue hope more than he.
Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13 A slow man seith, A lioun is in the weie, a liounnesse is in the foot pathis.
Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14 As a dore is turned in his hengis; so a slow man in his bed.
Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
15 A slow man hidith hise hondis vndur his armpit; and he trauelith, if he turneth tho to his mouth.
Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
16 A slow man semeth wysere to hym silf, than seuene men spekynge sentensis.
Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
17 As he that takith a dogge bi the eeris; so he that passith, and is vnpacient, and is meddlid with the chiding of anothir man.
Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18 As he is gilti, that sendith speris and arowis in to deth;
Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19 so a man that anoieth gilefuli his frend, and whanne he is takun, he schal seie, Y dide pleiynge.
ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 Whanne trees failen, the fier schal be quenchid; and whanne a priuy bacbitere is withdrawun, stryues resten.
Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21 As deed coolis at quic coolis, and trees at the fier; so a wrathful man reisith chidyngis.
Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22 The wordis of a pryuei bacbitere ben as symple; and tho comen til to the ynneste thingis of the herte.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23 As if thou wolt ourne a vessel of erthe with foul siluer; so ben bolnynge lippis felouschipid with `the werste herte.
Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24 An enemy is vndirstondun bi hise lippis, whanne he tretith giles in the herte.
Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
25 Whanne he `makith low his vois, bileue thou not to hym; for seuene wickidnessis ben in his herte.
Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
26 The malice of hym that hilith hatrede gilefuli, schal be schewid in a counsel.
Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
27 He that delueth a diche, schal falle in to it; and if a man walewith a stoon, it schal turne ayen to hym.
Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
28 A fals tunge loueth not treuth; and a slidir mouth worchith fallyngis.
Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.

< Proverbs 26 >