< Proverbs 12 >

1 He that loueth chastisyng, loueth kunnyng; but he that hatith blamyngis, is vnwijs.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 He that is good, schal drawe to hym silf grace of the Lord; but he that tristith in hise thouytis, doith wickidli.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 A man schal not be maad strong by wyckidnesse; and the root of iust men schal not be moued.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 A diligent womman is a coroun to hir hosebond; and rot is in the boonys of that womman, that doith thingis worthi of confusioun.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 The thouytis of iust men ben domes; and the counselis of wickid men ben gileful.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 The wordis of wickid men setten tresoun to blood; the mouth of iust men schal delyuere hem.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 Turne thou wickid men, and thei schulen not be; but the housis of iust men schulen dwelle perfitli.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 A man schal be knowun bi his teching; but he that is veyn and hertles, schal be open to dispising.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Betere is a pore man, and sufficient to him silf, than a gloriouse man, and nedi of breed.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 A iust man knowith the soulis of hise werk beestis; but the entrailis of wickid men ben cruel.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 He that worchith his lond, schal be fillid with looues; but he that sueth idilnesse, is moost fool. He that is swete, lyueth in temperaunces; and in hise monestyngis he forsakith dispisyngis.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 The desir of a wickid man is the memorial of worste thingis; but the roote of iust men schal encreesse.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 For the synnes of lippis `falling doun neiyeth to an yuel man; but a iust man schal scape fro angwisch.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 Of the fruyt of his mouth ech man schal be fillid with goodis; and bi the werkis of hise hondis it schal be yoldun to him.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 The weie of a fool is riytful in hise iyen; but he that is wijs, herith counsels.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 A fool schewith anoon his ire; but he that dissymelith wrongis, is wijs.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 He that spekith that, that he knowith, is a iuge of riytfulnesse; but he that lieth, is a gileful witnesse.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 A man is that bihetith, and he is prickid as with the swerd of conscience; but the tunge of wise men is helthe.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 The lippe of treuthe schal be stidfast with outen ende; but he that is a sudeyn witnesse, makith redi the tunge of leesyng.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 Gile is in the herte of hem that thenken yuels; but ioye sueth hem, that maken counsels of pees.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 What euere bifallith to a iust man, it schal not make hym sori; but wickid men schulen be fillid with yuel.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 False lippis is abhominacioun to the Lord; but thei that don feithfuli, plesen him.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 A fel man hilith kunnyng; and the herte of vnwise men stirith foli.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 The hond of stronge men schal haue lordschip; but the hond that is slow, schal serue to tributis.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Morenynge in the herte of a iust man schal make hym meke; and he schal be maad glad bi a good word.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 He that dispisith harm for a frend, is a iust man; but the weie of wickid men schal disseyue hem.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 A gileful man schal not fynde wynnyng; and the substaunce of man schal be the prijs of gold.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 Lijf is in the path of riytfulnesse; but the wrong weie leedith to deeth.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Proverbs 12 >