< Proverbs 11 >

1 A gileful balaunce is abhominacioun anentis God; and an euene weiyte is his wille.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 Where pride is, there also dispising schal be; but where meeknesse is, there also is wisdom.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 The simplenesse of iust men schal dresse hem; and the disseyuyng of weiward men schal destrie hem.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4 Richessis schulen not profite in the dai of veniaunce; but riytfulnesse schal delyuere fro deth.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 The riytfulnesse of a simple man schal dresse his weie; and a wickid man schal falle in his wickidnesse.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 The riytfulnesse of riytful men schal delyuere hem; and wickid men schulen be takun in her aspiyngis.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 Whanne a wickid man is deed, noon hope schal be ferther; and abidyng of bisy men schal perische.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 A iust man is delyuered from angwisch; and a wickid man schal be youun for hym.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 A feynere bi mouth disseyueth his freend; but iust men schulen be deliuered bi kunnyng.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 A citee schal be enhaunsid in the goodis of iust men; and preysyng schal be in the perdicioun of wickid men.
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 A citee schal be enhaunsid bi blessing of iust men; and it schal be distried bi the mouth of wickid men.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 He that dispisith his freend, is nedi in herte; but a prudent man schal be stille.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 He that goith gilefuli, schewith priuetees; but he that is feithful, helith the priuetee of a freend.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Where a gouernour is not, the puple schal falle; but helthe `of the puple is, where ben many counsels.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 He that makith feith for a straunger, schal be turmentid with yuel; but he that eschewith snaris, schal be sikur.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 A graciouse womman schal fynde glorie; and stronge men schulen haue richessis.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 A merciful man doith wel to his soule; but he that is cruel, castith awei, yhe, kynnesmen.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 A wickid man makith vnstable werk; but feithful mede is to hym, that sowith riytfulnesse.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 Merci schal make redi lijf; and the suyng of yuels `schal make redi deth.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 A schrewid herte is abhomynable to the Lord; and his wille is in hem, that goen symply.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 Thouy hond be in the hond, an yuel man schal not be innocent; but the seed of iust men schal be sauyd.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 A goldun `sercle, ether ryng, in the `nose thrillis of a sowe, a womman fair and fool.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 The desir of iust men is al good; abiding of wickid men is woodnesse.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 Sum men departen her owne thingis, and ben maad richere; other men rauyschen thingis, that ben not hern, and ben euere in nedynesse.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 A soule that blessith, schal be maad fat; and he that fillith, schal be fillid also.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 He that hidith wheete `in tyme, schal be cursid among the puplis; but blessyng schal come on the heed of silleris.
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 Wel he risith eerli, that sekith good thingis; but he that is a serchere of yuels, schal be oppressid of tho.
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 He that tristith in hise richessis, schal falle; but iust men schulen buriowne as a greene leef.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 He that disturblith his hows, schal haue wyndis in possessioun; and he that is a fool, schal serue a wijs man.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 The fruyt of a riytful man is the tre of lijf; and he that takith soulis, is a wijs man.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 If a iust man receyueth in erthe, how miche more an vnfeithful man, and synnere.
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

< Proverbs 11 >