< Numbers 26 >
1 Aftir that the blood of gilti men was sched out, the Lord seide to Moises and to Eleasar,
Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
2 preest, sone of Aaron, Noumbre ye al the summe of the sones of Israel, fro twenti yeer and aboue, bi her housis, and kynredis, alle men that mowen go forth to batels.
“Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
3 And so Moises and Eleasar, preest, spaken in the feeldi places of Moab, ouer Jordan, ayens Jerico, to hem that weren of twenti yeer and aboue,
Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
4 as the Lord comaundide; of whiche this is the noumbre.
“Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
5 Ruben, the firste gendrid of Israel; the sone of hym was Enoch, of whom was the meynee of Enochitis; and Phallu, of whom the meynee of Phalluytis; and Esrom,
Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
6 of whom the meynee of Esromytis; and Charmy, of whom the meynee of Charmytis.
kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
7 Thes weren the meynees of the generacioun of Ruben, of whiche meynees the noumbre was foundun thre and fourti thousand seuene hundrid and thretti.
Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
8 The sone of Phallu was Heliab;
Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
9 the sones of hym weren Namuel, and Dathan and Abiron. `These weren Dathan and Abiron, prynces of the puple, that riseden ayens Moises and Aaron, in the rebelte of Chore, whanne thei rebelliden ayens the Lord;
nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
10 and the erthe openyde his mouth, and deuouride Chore, while ful many men dieden, whanne the fier brente two hundrid men and fifti; and a greet myracle was maad,
Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
11 that whanne Chore perischide, hise sones perischiden not.
Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
12 The sones of Symeon bi her kynredis; Namuel, of hym was the meynee of Namuelitis; Jamyn, of hym was the meynee of Jamynytis; Jachin, of hym was the meynee of Jachynytis;
Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
13 Zare, of hym the meynee of Zarenytis; Saul, of hym the meynee of Saulitis.
kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
14 These weren the meynees of Symeon, of whiche all the noumbre was two and twenti thousynde and two hundrid.
Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
15 The sones of Gad bi her kynredis; Sephon, of hym the meynee of Sephonytis; Aggi, of hym the meynee of Aggitis; Sumy, of hym the meynee of Sumytis;
Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
16 Ozny, of hym the meynee of Oznytis; Heri, of hym the meynee of Hereytis;
kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
17 Arod, of hym the meynee of Aroditis; Ariel, of hym the meynee of Arielitis.
kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
18 These weren the meynees of Gad, of whiche al the noumbre was fourti thousynde and fyue hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
19 The sones of Juda weren Her and Onan, whiche bothe weren deed in the lond of Canaan.
Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
20 And the sones of Juda weren bi her kynredis; Sela, of whom the meynee of Selaitis; Phares, of whom the meynee of Pharesitis; Zare, of whom the meynee of Zareitis.
Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
21 Sotheli the sones of Phares weren Esrom, of whom the meynee of Esromytis; and Amul, of whom the meynee of Amulitis.
Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
22 These weren the meynees of Juda, of whiche al the noumbre was seuenty thousynde and fyue hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
23 The sones of Isachar bi her kynredis; Thola, of whom the meynee of Tholaitis; Phua, of whom the meynee of Phuitis;
Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
24 Jasub, of whom the meynee of Jasubitis; Semran, of whom the meynee of Semranytis.
kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
25 These weren the kynredis of Isachar, of whiche the noumbre was foure and sixti thousynd and three hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
26 The sones of Zabulon bi her kinredis; Sarad, of whom the meynee of Sareditis; Helon, of whom the meynee of Helonytis; Jalel, of whom the meynee of Jalelitis.
Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
27 These weren the kynredis of Zabulon, of whiche the noumbre was sixti thousynde and fyue hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
28 The sones of Joseph bi her kynredis weren Manasses and Effraym.
Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
29 Of Manasses was borun Machir, of whom the meynee of Machiritis. Machir gendride Galaad, of whom the meynee of Galaditis.
Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
30 Galaad hadde sones; Hizezer, of whom the meynee of Hizezeritis; and Helech, of whom the meynee of Helechitis;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
31 and Ariel, of whom the meynee of Arielitis; and Sechem, of whom the meynee of Sechemytis;
kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
32 and Semyda, of whom the meynee of Semydaitis; and Epher, of whom the meynee of Epheritis.
kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
33 Forsothe Epher was the fadir of Salphath, that hadde not sones, but oneli douytris; of whiche these weren the names; Maala, and Noha, and Egla, and Melcha, and Thersa.
(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
34 These weren the meynees of Manasse, and the noumbre of hem was two and fifty thousynde and seuene hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
35 Forsothe the sones of Effraym bi her kynredis weren these; Suthala, of whom the meynee of Suthalaitis; Bether, of whom the meynee of Betherytis; Tehen, of whom the meynee of Thehenytis.
Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
36 Forsothe the sone of Suthala was Heram, of whom the meynee of Heramytis.
Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
37 These weren the kynredis `of the sones of Effraym, of whiche the noumbre was two and thretti thousynde and fyue hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
38 These weren the sones of Joseph, bi her meynees. The sones of Beniamyn in her kynredis; Bale, of whom the meynee of Baleytis; Azbel, of whom the meynee of Azbelitis; Ahiram, of whom the meynee of Ahiramitis;
Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
39 Suphan, of whom the meynee of Suphanitis; Huphan, of whom the meynee of Huphanitis.
kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
40 The sones of Bale, Hered and Noeman; of Hered, the meyne of Hereditis; of Noeman, the meynee of Noemanitis.
Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
41 Thes weren the sones of Beniamyn bi her kynredis, of whiche the noumbre was fyue and fourti thousynde and sixe hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
42 The sones of Dan bi her kynredis; Suphan, of whom the meynee of Suphanytis. These weren the kynredis of Dan bi her meynees;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
43 alle weren Suphanytis, of whiche the noumbre was foure and sixti thousynde and foure hundrid.
Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
44 The sones of Aser bi her kynredis; Jemma, of whom the meynee of Jemmaytis; Jesuy, of whom the meynee of Jesuytis; Brie, of whom the meynee of Brieitis.
Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
45 The sones of Brie; Haber, of whom the meynee of Haberitis; and Melchiel, of whom the meynee of Melchielitis.
kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
46 Sotheli the name of `the douytir of Azer was Zara.
(Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
47 These weren the kynredis of the sones of Aser, and the noumbre of hem was foure and fifti thousynde and foure hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
48 The sones of Neptalym bi her kynredis; Jesehel, of whom the meynee of Jeselitis; Guny, of whom the meynee of Gunytis;
Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
49 Jeser, of whom the meynee of Jeserytis; Sellem, of whom the meynee of Sellemytis.
kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
50 Thes weren the kynredis of the sones of Neptalym bi her meynees, of whiche the noumbre was fyue and fourti thousynde and foure hundrid.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
51 This is the summe of the sones of Israel, that weren noumbrid, sixe hundrid thousynde and a thousynde seuene hundrid and thretti.
Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
52 And the Lord spak to Moises, and seide,
Bwana akamwambia Mose,
53 The lond schal be departid to these, bi the noumbre of names in to her possessiouns;
“Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
54 thou schalt yyue the grettere part to mo men, and the lesse part to fewere men; possessioun schal be youun to alle bi hem silf, as thei ben noumbrid now;
Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
55 so oneli that lot departe the lond to lynagis and meynees.
Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
56 What euer thing bifallith bi lot, ethir mo ether fewere men take this.
Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
57 Also this is the noumbre of the sones of Leuy bi her meynees; Gerson, of whom the meynee of Gersonytis; Caath, of whom the meynee of Caathitis; Merary, of whom the meynee of Meraritis.
Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
58 These weren the meynees of Leuy; the meynee of Lobny, the meynee of Ebron, the meynee of Mooli, the meynee of Musi, the meynee of Chori. And sotheli Caath gendride Amram,
Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
59 which hadde a wijf, Jocabeth, douyter of Leuy, which douyter was borun to hym in Egipt. This Jocabeth gendride to hir hosebonde `Amram sones, Aaron, and Moyses, and Marie, `the sister of hem.
jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
60 Nadab, and Abyu, and Eleazar, and Ithamar weren bigetun of Aaron;
Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
61 of whiche Nadab and Abyu weren deed, whanne thei hadden offrid alien fier bifor the Lord.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
62 And alle that weren noumbrid weren thre and twenti thousynde of male kynde, fro o monethe and aboue, whiche weren not noumbrid among the sones of Israel, nether possessioun was youun to hem with othir men.
Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
63 This is the noumbre of the sones of Israel, that weren discryued of Moises and Eleasar, preest, in the feeldi places of Moab, ouer Jordan, ayen Jerico;
Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
64 among whiche noon of hem was that weren noumbrid bifor of Moises and Aaron, in the deseert of Synay;
Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
65 for the Lord bifore seide, that alle schulden die in `the wildirnesse; and noon of hem dwellide, no but Caleph, `the sone of Jephone, and Josue, the sone of Nun.
Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.