< Numbers 25 >

1 Forsothe in that tyme Israel dwellide in Sechym; and the puple dide fornycacioun with the douytris of Moab;
Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
2 whiche douytris clepiden hem to her sacrifices, and thei eten, and worschipiden the goddis of tho douytris;
ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
3 and Israel made sacrifice to Belphegor. And the Lord was wrooth,
Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
4 and seide to Moises, Take thou alle the princes of the puple, and hange hem ayens the sunne in iebatis, that my wodnesse, `that is stronge veniaunce, be turned awai fro Israel.
Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
5 And Moises seide to the iugis of Israel, Ech man sle his neiyboris, that maden sacrifice to Belphagor.
Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
6 And, lo! oon of the sones of Israel entride bifor his britheren to `an hoore of Madian, in the siyt of Moises, and al the cumpeny of the sones of Israel, whiche wepten bifor the yatis of the tabernacle.
Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
7 And whanne Phynees, the sone of Eleazar, sone of Aaron, preest, hadde seyn this, he roos fro the myddis of the multitude; and whanne he hadde take a swerd,
Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
8 he entride aftir the man of Israel in to the `hoore hows, and stikide thorou both togidere, that is, the man and the womman, in the places of gendryng. And the veniaunce ceesside fro the sones of Israel,
akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
9 and foure and twenti thousand of men weren slayn.
Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
10 And the Lord seide to Moises,
Bwana akamwambia Mose,
11 Fynees, the sone of Eleazar, sone of Aaron, preest, turnede away myn yre fro the sones of Israel; for he was stirid ayens hem bi my feruent loue, that Y my silf schulde not do awai the sones of Israel in my greet hete, `ether strong veniaunce.
“Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
12 Therfor speke thou to hym, Lo! Y yyue to hym the pees of my couenaunt,
Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
13 and it schal be an euerlastynge couenaunt of preesthod, as wel to hym silf as to his seed; for he louyde feruentli for his God, and he clenside the greet trespas of the sones of Israel.
Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
14 Forsothe the name of the man of Israel, that was slayn with the womman of Madian, was Zambri, the sone of Salu, duyk of the kynrede and lynage of Symeon.
Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
15 Forsothe the womman of Madian that was slayn togidere, was clepid Cobri, the douyter of Sur, the nobleste prince of Madianytis.
Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
16 And the Lord spak to Moises and seide,
Bwana akamwambia Mose,
17 `Madianytis feele you enemyes, and smyte ye hem;
“Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
18 for also thei diden enemyliche ayens you, and disseyueden thorow tresouns, bi the idol of Phegor, and bi `the douyter of Corbri, duyk of Madian, her sister, which douyter was sleyn in the dai of veniaunce, for the sacrilege of Phegor.
kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”

< Numbers 25 >