< Numbers 18 >

1 And the Lord seide to Aaron, Thou, and thi sones, and the hows of thi fadir with thee, schulen bere the wickidnesse of the seyntuarie; and thou and thi sones togidere schulen suffre the synnes of youre preesthod.
Bwana akamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, na wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.
2 But also take thou with thee thi britheren of the lynage of Leuy, and the power of thi fadir, and be thei redi, that thei mynystre to thee. Forsothe thou and thi sones schulen mynystre in the tabernacle of witnessyng;
Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.
3 and the dekenes schulen wake at thi comaundementis, and at alle werkis of the tabernacle; so oneli that thei neiye not to the vessels of seyntuarie, and to the autir, lest bothe thei dien, and ye perischen togidere.
Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.
4 Forsothe be thei with thee, and wake thei in the kepyngis of the tabernacle, and in alle the cerymonyes therof. An alien schal not be meddlid with you.
Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.
5 Wake ye in the kepyng of the seyntuarie, and in the seruyce of the auter, lest indignacioun rise on the sones of Israel.
“Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.
6 Lo! Y haue youun `to you youre britheren, dekenes, fro the myddis of the sones of Israel, and Y haue youe a fre yifte to the Lord, that thei serue in the seruyces of his tabernacle.
Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwa Bwana ili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.
7 Forsothe thou and thi sones, kepe youre preesthod; and alle thingis that perteynen to the ournyng of the auter, and ben with ynne the veil, schulen be mynystrid bi preestis; if ony straunger neiyeth, he schal be slayn.
Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine yeyote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”
8 The Lord spak to Aaron, Lo! Y haue youe to thee the kepyng of my firste fruytis; Y haue youe to thee and to thi sones alle thingis, that ben halewid of the sones of Israel, for preestis office euerlastynge lawful thingis.
Kisha Bwana akamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.
9 Therfor thou schalt take these thingis of tho thingis that ben halewid, and ben offrid to the Lord; ech offryng, and sacrifice, and what euer thing is yoldun to me for synne and for trespas, and cometh in to hooli of hooli thingis, schal be thin and thi sones.
Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka kwa matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka, au za dhambi, au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.
10 Thou schalt ete it in the seyntuarie; malis oneli schulen ete therof, for it is halewid to the Lord.
Mtaila kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume ataila. Ni lazima mtaiheshimu kama takatifu.
11 Forsothe Y haue youe to thee, and to thi sones and douytris, bi euerlastynge riyt, the firste fruytis whiche the sones of Israel a vowen and offren; he that is clene in thin hous, schal ete tho.
“Hiki pia ni chako: chochote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kuinuliwa za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.
12 Y yaf to thee al the merowe of oile, and of wyn, and of wheete, what euer thing of the firste fruytis thei schulen offre to the Lord.
“Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote, na divai mpya iliyo bora kuliko zote na nafaka wanazompa Bwana kama malimbuko katika mavuno yao.
13 Alle the bigynnyngis of fruytis whiche the erthe bryngith forth, and ben brouyt to the Lord, schulen falle in to thin vsis; he that is cleene in thin hous, schal ete of tho.
Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamletea Bwana yatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.
14 Al thing which the sones of Israel yelden bi avow, schal be thin.
“Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwa Bwana ni chenu.
15 What euer thing `schal breke out first of the wombe of al fleisch, which fleisch thei offren to the Lord, whether it is of men, ethir of beestis, it schal be of thi riyt; so oneli that thou take prijs for the firste gendrid child of man, and that thou make ech beeste which is vncleene to be bouyt ayen;
Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwa Bwana ni wenu. Lakini ni lazima mtamkomboa kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.
16 whos ayenbiyng schal be aftir o monethe, for fyue siclis of siluer, bi the weiyte of seyntuarie; a sicle hath xx. halpens.
Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tano za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.
17 Forsothe thou schalt not make the firste gendrid of oxe, and of scheep, and of goet, to be ayen bouyt, for tho ben halewid to the Lord; oneli thou schalt schede the blood of tho on the auter, and thou schalt brenne the ynnere fatnesse in to swettist odour to the Lord.
“Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
18 Forsothe the fleischis schulen falle in to thin vss, as the brest halewid and the riyt schuldur, schulen be thine.
Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kuinuliwa na paja la mguu wa kulia.
19 Y yaf to the and to thi sones and douytris, bi euerlastynge riyt, alle the firste fruytis of seyntuarie, whiche the sones of Israel offren to the Lord; it is euerlastynge couenant of salt bifor the Lord, to thee, and to thi sones.
Chochote kitakachotengwa kutoka sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtolea Bwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele za Bwana kwako na watoto wako.”
20 And the Lord seide to Aaron, Ye schulen not welde ony thing in the lond of hem, nether ye schulen haue part among hem; Y am thi part and erytage, in the myddis of the sones of Israel.
Bwana akamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wowote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.
21 Forsothe Y yaf to the sones of Leuy alle the tithis of Israel in to possessioun, for the seruyce bi whyche thei seruen me in the tabernacle of boond of pees;
“Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.
22 that the sones of Israel neiye no more to the `tabernacle of boond of pees, nether do dedli synne.
Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.
23 To the sones aloone of Leuy, seruynge me in the tabernacle, and berynge the `synnes of the puple, it schal be a lawful thing euerlastynge in youre generaciouns.
Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wowote miongoni mwa Waisraeli.
24 Thei schulen welde noon other thing, and thei schulen be apeied with the offryng of tithis, whiche Y departide in to vsis and necessaries of hem.
Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwa Bwana kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’”
25 And the Lord spak to Moises and seide,
Bwana akamwambia Mose,
26 Comaunde thou, and denounse to the dekenes, Whanne ye han take tithis of the sones of Israel, whiche Y yaf to you, offre ye the firste fruytis of tho to the Lord, that is, the tenthe part of the dyme,
“Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwa Bwana, iwe zaka ya hiyo zaka.
27 that it be arettid to you in to offryng of the firste fruytis, as wel of corn flooris as of pressis;
Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.
28 and of alle thingis of whiche ye taken tithis, offre ye the firste fruytis to the Lord, and yyue ye to Aaron, preest.
Kwa njia hii, ninyi pia mtatoa sadaka kwa Bwana kutoka zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu ya Bwana kwa Aroni, kuhani.
29 Alle thingis whiche ye schulen offre of tithis, and schulen departe in to the yiftis of the Lord, schulen be the beste, and alle chosun thingis.
Ni lazima mtoe kama sehemu ya Bwana iliyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’
30 And thou schalt seye to hem, If ye offren to the Lord alle the clere and betere thingis of tithis, it schal be arettid to you, as if ye yauen the firste fruitis of the corn floor and presse.
“Waambie Walawi: ‘Mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.
31 And ye schulen ete tho tithis in alle youre placis, as wel ye as youre meynees, for it is the prijs for the seruyce, in whiche ye seruen in the tabernacle of witnessyng.
Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali popote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.
32 And ye schulen not do synne on this thing, `and resserue noble thingis and fat to you, lest ye defoulen the offryngis of the sones of Israel, and ye dien.
Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’”

< Numbers 18 >