< Nehemiah 8 >

1 And the seuenthe monethe `was comun vndur Esdras and Neemye; sotheli the sones of Israel weren in her cytees. And al the puple was gaderid togydere as o man, to the street which is bifor the yate of watris. And thei seiden to Esdras, the scribe, that he schulde brynge the book of the lawe of Moises, which the Lord hadde comaundid to Israel.
watu wote wakakusanyika kama mtu mmoja kwenye uwanja mbele ya Lango la Maji. Wakamwambia Ezra mwandishi alete Kitabu cha Sheria ya Mose, ambacho Bwana aliamuru kwa ajili ya Israeli.
2 Therfor Esdras, the preest, brouyte the lawe bifor the multitude of men and of wymmen, and bifor alle that myyten vndurstonde, `in the firste day of the seuenth monethe.
Basi katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba, kuhani Ezra akaleta Sheria mbele ya kusanyiko, ambamo walikuwamo wanaume, wanawake na watu wote walioweza kufahamu.
3 And he redde in it opynli in the street that was bifor the yate of watris, fro the morewtid `til to myddai, in the siyt of men and of wymmen and of wise men; and the eeris of al the puple weren reisid to the book.
Akaisoma kwa sauti kubwa tangu mapambazuko mpaka adhuhuri, akiwa ameuelekea uwanja uliokuwa mbele ya Lango la Maji mbele ya wanaume, wanawake na wengine ambao waliweza kufahamu. Watu wote wakasikiliza kwa makini kile Kitabu cha Sheria.
4 Forsothe Esdras the writere stood on the grees of tree, which he hadde maad to speke theron; and Mathatie, and Semma, and Ananye, and Vrie, and Elchie, and Maasie stoden bisidis hym at his riyt half; and Phadaie, Mysael, and Melchie, Assum, and Aseph, Dana, and Zacharie, and Mosollam stoden at the left half.
Mwandishi Ezra alikuwa amesimama juu ya jukwaa la miti lililojengwa kwa kusudi hilo. Karibu naye upande wa kuume alisimama Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya. Upande wake wa kushoto walikuwepo Pedaya, Mishaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu.
5 And Esdras openyde the book bifor al the puple; for he apperide ouer al the puple; and whanne he hadde openyd the book, al the puple stood.
Ezra akakifungua kile kitabu. Watu wote waliweza kumwona kwa sababu alikuwa amesimama juu zaidi, naye alipokifungua watu wote wakasimama.
6 And Esdras blesside the Lord God with greet vois; and al the puple answeride, Amen, Amen, reisynge her hondis. And thei weren bowid, and thei worschipiden God, lowli on the erthe.
Ezra akamsifu Bwana, Mungu mkuu, nao watu wote wakainua mikono yao na kuitikia, “Amen! Amen!” Kisha wakasujudu na kumwabudu Bwana hali nyuso zao zikigusa ardhi.
7 Forsothe Josue, and Baany, and Serebie, Jamyn, Acub, Septhai, Odia, Maasie, Celitha, Ayarie, Jozabeth, Anan, Phallaie, dekenes, maden silence in the puple for to here the lawe. Sotheli the puple stood in her degree.
Watu wakiwa wamesimama pale, Walawi wafuatao waliwafunza ile Sheria: Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya.
8 And thei redden in the book of Goddis lawe distinctli, `ether atreet, and opynli to vndurstonde; `and thei vndurstoden, whanne it was red.
Walisoma kutoka kile Kitabu cha Sheria ya Mungu, wakiifafanua na kuwapa maelezo ili watu waweze kufahamu kile kilichokuwa kikisomwa.
9 Forsothe Neemye seide, he is Athersata, and Esdras, the preest and writere, and the dekenes, expownynge to al the puple, It is a dai halewid to `oure Lord God; nyle ye morne, and nyle ye wepe. For al the puple wepte, whanne it herde the wordis of the lawe.
Ndipo Nehemia aliyekuwa mtawala, Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia wote, “Siku hii ni takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msiomboleze wala msilie.” Kwa kuwa watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya ile Sheria.
10 And he seide to hem, Go ye, and `ete ye fatte thingis, and drynke ye wiyn `maad swete with hony, and sende ye partis to hem, that maden not redi to hem silf, for it is an hooli dai of the Lord; `nyle ye be sory, for the ioye of the Lord is youre strengthe.
Nehemia akasema, “Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Bwana. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”
11 Sotheli the dekenes maden silence in al the puple, and seiden, Be ye stille, for it is an hooli dai, and `nyle ye make sorewe.
Walawi wakawatuliza watu wote wakisema, “Kuweni watulivu, kwa kuwa hii ni siku takatifu. Msihuzunike.”
12 Therfor al the puple yede for to ete, and drynke, and to sende partis, and `to make greet gladnesse; for thei vndurstoden the wordis, whiche he hadde tauyt hem.
Kisha watu wote wakaondoka kwenda kula na kunywa, na kupeana sehemu ya chakula, na wakaadhimisha kwa furaha kubwa, kwa sababu sasa walifahamu maneno yale waliyokuwa wameelezwa.
13 And in the secound dai the princes of meynees, alle the puplis, prestis, and dekenes, weren gaderid togidere to Esdras, the writere, that he schulde expowne to hem the wordis of the lawe.
Katika siku ya pili ya mwezi, wakuu wa mbari zote, pamoja na makuhani na Walawi, walikusanyika wakimzunguka Ezra mwandishi ili wapate kusikiliza kwa makini maneno ya Sheria.
14 And thei foundun writun in the lawe, that the Lord comaundide `in the hond of Moyses, that the sones of Israel dwelle in tabernaclis in the solempne dai, in the seuenthe moneth;
Wakakuta imeandikwa katika ile Sheria, ambayo Bwana aliiamuru kupitia kwa Mose, kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba,
15 and that thei preche, and pupplische a vois in alle her citees, and in Jerusalem; and seie, Go ye out in to the hil, and brynge ye bowis of olyue, and bowis of the faireste tree, the bowis of a myrte tree, and the braunchis of a palm tree, and the bowis of a `tree ful of wode, that tabernaclis be maad, as it is writun.
na kwamba walipaswa kutangaza neno hili na kulieneza katika miji yao na katika Yerusalemu wakisema: “Enendeni katika nchi ya mlima na kuleta matawi kutoka miti ya mizeituni, mizeituni mwitu, mihadasi, mitende na miti ya kivuli, ili kutengeneza vibanda,” kama ilivyoandikwa.
16 And al the puple yede out, and thei brouyten, and maden to hem silf tabernaclis, `ech man in `his hows roof, and in her stretis, `ether foryerdis, and in the large placis of Goddis hows, and in the street of the yate of watris, and in the street of the yate of Effraym.
Basi watu wakaenda na kuleta matawi, nao wakajijengea vibanda juu ya paa za nyumba zao, katika nyua zao, katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja karibu na Lango la Maji na uwanja wa Lango la Efraimu.
17 Therfor al the chirche of hem, that camen ayen fro caytifte, made tabernaclis, and thei dwelliden in tabernaclis. For the sones of Israel hadden not do siche thingis fro the daies of Josue, sone of Nun, `til to that dai; and ful greet gladnesse was.
Jamii yote ya watu waliorudi kutoka utumwani wakajenga vibanda na kuishi ndani yake. Tangu wakati wa Yoshua mwana wa Nuni mpaka siku ile, Waisraeli hawakuwahi kuiadhimisha namna hii. Furaha yao ilikuwa kubwa sana.
18 Forsothe Esdras radde in the book of Goddis lawe bi alle daies, fro the firste dai `til to the laste dai; and thei maden solempnytee bi seuene daies, and in the eiyte day thei maden a gaderyng of siluer, `bi the custom.
Siku baada ya siku, kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho, Ezra alisoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakaiadhimisha sikukuu ile kwa siku saba, nayo siku ya nane, kufuatana na maagizo, kulikuwa na kusanyiko maalum.

< Nehemiah 8 >