< Nehemiah 12 >

1 Sotheli these weren prestis and dekenes, that stieden with Zorobabel, the sone of Salatiel, and with Josue; Saraie, Jeremye,
Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Esdras, Amarie, Melluch, Accus,
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Sechenye, Reum, Merymucth,
Shekania, Rehumu, Meremothi,
4 Addo, Jethon, Myomyn,
Ido, Ginethoni, Abiya,
5 Abia, Meldaa, Belga, Semeie, and Joarib,
Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Adaie, Sellum, Amoe, Elceia, and Jadie;
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 these weren the princes of prestis `and her britheren, in the daies of Josue.
Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
8 Certis dekenes; Jesua, Bennuy, Cedynyel, Serabie, Juda, Mathanye, `weren ouer the ympnes, `thei and her britheren;
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 and Bezechie, and Ezanny, and the britheren of hem, ech man in his office.
Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 Sotheli Josue gendride Joachym, and Joachym gendride Eliasib, and Eliasib gendride Joiada,
Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 and Joiada gendride Jonathan, and Jonathan gendride Jeddaia.
Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 Forsothe in the daies of Joachym weren prestis, and princis of meynees of prestis, Saraie, Amarie, Jeremye, Ananye, Esdre,
Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 Mosollam, Amarie, Johannam,
wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 Mylico, Jonathan, Sebenye,
wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
15 Joseph, Aram, Edua,
wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 Maraioth, Elchie, Addaie, Zacharie, Genthon,
wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 Mosollam, Abie, Zecherie, Myamyn, and Moadie,
wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
18 Phelti, Belge, Sannya, Semeie,
wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 Jonathan, Joarib, Mathanye, Jodaie, Azi,
wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 Sellaye, Mochebor, Helchie,
wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 Asebie, Idaie, Nathanael.
wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 Dekenes in the daies of Eliasib, and of Joiada, and of Jonam, and of Jedda, weren writun princes of meynees, `and prestis in the rewme of Darius of Persis.
Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
23 The sones of Leuy, princes of meynees, weren writun in the book of wordis of daies, and `til to the daies of Jonathan, sone of Eliasib.
Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 `And the princes of dekenes weren Asebie, Serebie, and Jesue, the sone of Cedynyel; and the britheren of hem bi her whiles, that thei schulden herie and knowleche bi the comaundement of kyng Dauid, the man of God, and thei schulden kepe euenli bi ordre.
Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 Mathanye, and Bethbecie, and Obedie, Mosollam, Thelmon, Accub, weren keperis of the yatis, and of the porchis bifor the yatis.
Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 These weren in the daies of Joachym, sone of Josue, sone of Josedech, and in the daies of Neemye, duyk, and of Esdras, the prest and writere.
Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 Forsothe in the halewyng of the wal of Jerusalem thei souyten dekenes of alle her places, to bryng hem in to Jerusalem, and to make the halewyng in gladnesse, in the doyng of thankyngis, and in song, and in cymbalis, and in sautrees, and in harpis.
Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 Sotheli the sones of syngeris weren gaderid bothe fro the feeldi places aboute Jerusalem, and fro the townes of Nethophati,
Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 and fro the hows of Galgal, and fro the cuntreis of Gebez, and of Amanech; for syngeris hadden bildid townes to hem silf in the cumpas of Jerusalem.
kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 And prestis and dekenes weren clensid, and thei clensiden the puple, and the yatis, and the wal.
Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 Forsothe Y made the princes of Juda to stie on the wal, and Y ordeynede twei greete queris of men heriynge; and thei yeden to the riyt side on the wal, to the yate of the dunghil.
Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 And Osaie yede aftir hem, and the half part of prynces of Juda,
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 and Azarie, Esdras, and Mosollam,
pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
34 Juda, and Beniamyn, and Semeye, and Jeremye `yeden aftir hem.
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
35 And of the sones of prestis syngynge in trumpis; Zacharie, the sone of Jonathan, the sone of Semeie, the sone of Mathanye, the sone of Machaie, the sone of Zeccur, the sone of Asaph.
pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 And hise britheren; Semeie, and Azarel, Malalai, Galalai, Maai, Nathanael, and Juda, and Amany, in the instrumentis of song of Dauid, the man of God; and Esdras, the wrytere, bifor hem, in the yate of the welle.
pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 And thei stieden ayens hem in the greis of the citee of Dauid, in the stiyng of the wal, on the hows of Dauid, and `til to the yate of watris at the eest.
Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 And the secounde queer of men tellynge thankyngis yede euene ayens, and Y aftir hym; and the half part of the puple was on the wal, and on the tour of ouenys, and `til to the broddeste wal;
Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
39 and on the yate of Effraym, and on the elde yate, and on the yate of fischis, and on the toure of Ananeel, and on the tour of Emath, and thei camen `til to the yate of the floc;
juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 and thei stoden in the yate of kepyng. And twei queeris of men heriynge stoden in the hows of God, and Y and the half part of magistratis with me.
Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 And the prestis, Eliachym, Maasie, Myamyn, Mychea, Helioneai, Zacharie, Ananye, in trumpis;
na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 and Maasie, and Senea, and Eleazar, and Azi, and Johannan, and Melchia, and Elam, and Ezer; and the syngeris sungen clereli, and Jezraie, the souereyn.
na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 And thei offriden in that dai grete sacrifices, and weren glad; `for God `hadde maad hem glad with grete gladnesse. But also her wyues and lawful childre weren ioiful, and the gladnesse of Jerusalem was herd fer.
Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 Also thei noumbriden in that dai men ouer the keping places of tresour, to moiste sacrifices, and to the firste fruytis, and to tithis, that the princes of the citee schulden brynge in bi hem, `in the fairenesse of doyng of thankyngis, prestis and dekenes; for Juda was glad in prestis and dekenes present.
Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 And thei kepten the kepyng of her God, the kepyng of clensyng; and syngeris, and porteris, bi the comaundement of Dauid and of Salomon, his sone;
Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
46 for in the daies of Dauid and of Asaph fro the bigynnyng princes of syngeris weren ordeyned, heriyng in song, and knoulechynge to God.
Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 And al Israel, in the daies of Zorobabel, and in the daies of Neemye, yauen partis to syngeris and to porteris bi alle `the daies; and thei halewiden dekenes, and the dekenes halewiden the sones of Aaron.
Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

< Nehemiah 12 >