< Nahum 2 >

1 He stiede up, that schal scatere bifore thee, that schal kepe bisechyng; biholde thou the weie, coumforte leendis, strengthe thou vertu greetli.
Yule ambaye atakuharibu vipande vipande anakuja dhidi yako. Linda kuta za mji, linda barabara, jitieni nguvu ninyi wenyewe, yakusanyeni majeshi yenu.
2 For as the Lord yeldide the pride of Jacob, so the pride of Israel; for distrieris scateriden hem, and distrieden the generaciouns of hem.
Maana Yehova anarejesha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli, ingawa wateka nyara waliwaharibu na kuharibu matawi ya zabibu zao.
3 The scheld of stronge men of hym ben firi, men of the oost ben in rede clothis; raynes of fire of chare, in the dai of his makyng redi; and the leederis therof ben asleep.
Ngao za mashujaa wake ni nyekundu, na watu hodari wamevaa nguo nyekundu; magari ya vita yameandaliwa yanang'ara kwenye vyuma vyake wakati wa mchana, na mikuki ya mivinje inarushwa hewani.
4 In weies thei ben troblid togidere, cartis of foure horsis ben hurtlid togidere in stretis; the siyte of hem as laumpis, as leitis rennynge aboute.
Magari ya vita yapo kasi kwenye mitaa; yanakimbia mbele na nyuma katika mitaa. Yapo kama kurunzi, na yanakimbia kama radi.
5 He schal bithenke of his stronge men, thei schulen falle in her weies; and swiftli thei schulen stie on the wallis therof, and schadewyng place schal be maad redi.
Yule ambaye atakuvunja vipande vipande anawaita maafisa wake; wanajikwaa kila mmoja kwa mwingine katika kutembea kwao; wanaharakisha kuushambulia ukuta wa mji. Ngao kubwa imetayarishwa kujikinga na hawa washambuliaji.
6 Yatis of floodis ben openyd, and the temple is brokun doun to erthe.
Malango kwenye mito yamelazishwa kufunguka, na jumba la mfalme linaanguka kwenye uharibifu.
7 And a knyyt is led awei caitif, and the handmaidis therof schulen be dryuun sorewynge as culueris, grutchynge in her hertis.
Husabu amevuliwa mavazi yake na amachukuliwa; watumishi wake wa kike wanaomboleza kama njiwa, wanavipiga vifua vyao.
8 And Nynyue, as a cisterne of watris the watris therof; forsothe thei fledden; stonde ye, stonde ye, and there is not that schal turne ayen.
Ninawi ni kama bwawa la maji linalovuja, watu wake kwa pamoja wanakimbia kama maji yanayotiririka. Wengine wanasema, “Simama, simama,” lakini hakuna anayegeuka nyuma.
9 Rauysche ye siluer, rauysche ye gold; and there is noon ende of richessis, of alle desirable vessels.
Chukua nyara ya fedha, kuchua nyara ya dhahabu, maana hakuna mwisho wake, kwa fahari ya vitu vyote vizuri vya Ninawi.
10 It is distried, and kit, and to-rent, and herte failynge, and vnknyttinge of smale knees, and failynge in alle reynes; and the face of alle ben as blacnesse of a pot.
Ninawi ipo tupu na imeharibiwa. Moyo wa kila mtu unayeyuka, magoti ya kila mmoja yanagongana pamoja, na uchungu upo kwa kila mmoja; sura zao wote zimepauka.
11 Where is the dwellyng of liouns, and lesewis of whelpis of liouns? To whiche citee the lioun yede, that the whelp of the lioun schulde entre thidur, and there is not that schal make aferd.
Sasa liko wapi pango la simba, sehemu ambapo simba wadogo hula chakula, sehemu ambapo simba dume na simba jike walitembea, pamoja wana-simba, ambapo hawakuogopa kitu chochote?
12 The lioun took ynow to hise whelpis, and slowy to his lionessis; and fillide her dennes with prei, and his couche with raueyn.
Simba alirarua mawindo yake vipande vipande kwa ajili ya watoto wake; aliwanyonga mawindo wake kwa ajili ya wake zake, na kulijaza pango lake mawindo, makao yake kwa mizoga iliyoraruliwa.
13 Lo! Y to thee, seith the Lord God of oostis; and Y schal brenne thi cartis of foure horsis til to the hiyeste, and swerd schal ete thi smale liouns; and Y schal distrie thi prei fro the lond, and the vois of thi messangeris schulen no more be herd.
“Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi. Nitayachoma magari yenu ya vita katika moshi, na upanga utateketeza simba wenu vijana. Nitazuia nyara zenu kutoka kwenye nchi yangu, na sauti za wajumbe wenu hazitasikika tena.”

< Nahum 2 >