< Matthew 26 >
1 And it was doon, whanne Jhesus hadde endid alle these wordis, he seide to hise disciplis,
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2 Ye witen, that aftir twei daies pask schal be maad, and mannus sone schal be bitakun to be crucified.
“Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe.”
3 Than the princes of prestis and the elder men of the puple were gaderid in to the halle of the prince of prestis, that was seid Cayfas,
Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4 and maden a counsel to holde Jhesu with gile, and sle him;
Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5 but thei seiden, Not in the haliday, lest perauenture noyse were maad in the puple.
Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6 And whanne Jhesus was in Betanye, in the hous of Symount leprous,
Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7 a womman that hadde a box of alabastre of precious oynement, cam to hym, and schedde out on the heed of hym restynge.
mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8 And disciplis seynge hadden dedeyn, and seiden, Wherto this loss? for it myyte be seld for myche,
Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Ya nini hasara hii?
9 and be youun to pore men.
Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha.”
10 But Jhesus knewe, and seide to hem, What ben ye heuy to this womman? for sche hath wrouyt in me a good werk.
Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11 For ye schulen euere haue pore men with you, but ye schulen not algatis haue me.
Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12 This womman sendynge this oynement in to my bodi, dide to birie me.
Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13 Treuli Y seie to you, where euer this gospel schal be prechid in al the world, it schal be seid, that sche dide this, in mynde of hym.
Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye.”
14 Thanne oon of the twelue, that was clepid Judas Scarioth, wente forth to the princis of prestis,
Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15 and seide to hem, What wolen ye yyue to me, and Y schal bitake hym to you? And thei ordeyneden to hym thretti pans of siluer.
akawaambia, “Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?” Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16 And fro that tyme he souyte oportunyte, to bitraye hym.
na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17 And in the firste dai of therf looues the disciplis camen to Jhesu, and seiden, Where wolt thou we make redi to thee, to ete paske?
Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, “Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?”
18 Jhesus seide, Go ye into the citee to `sum man, and seie to hym, The maistir seith, My tyme is nyy; at thee Y make paske with my disciplis.
Yeye akawajibu, “Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.”
19 And the disciplis diden, as Jhesus comaundide to hem; and thei maden the paske redi.
Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20 And whanne euentid was come, he sat to mete with hise twelue disciplis.
Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21 And he seide to hem, as thei eten, Treuli Y seie to you, that oon of you schal bitraye me.
Walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.”
22 And thei ful sori bigunnen ech bi hym silf to seie, Lord, whether `Y am?
Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, “Bwana! Je, ni mimi?”
23 And he answeride, and seide, He that puttith with me his hoond in the plater, schal bitraye me.
Yesu akajibu, “Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24 Forsothe mannus sone goith, as it is writun of hym; but wo to that man, bi whom mannus sone schal be bitrayed; it were good to hym, if that man hadde not be borun.
Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa.”
25 But Judas that bitraiede hym, answeride, seiynge, Maister, whether `Y am? Jhesus seide to hym, Thou hast seid.
Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, “Mwalimu! Je, ni mimi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
26 And while thei soupeden, Jhesus took breed, and blesside, and brak, and yaf to hise disciplis, and seide, Take ye, and ete; this is my body.
Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni mle; huu ni mwili wangu.”
27 And he took the cuppe, and dide thankyngis, and yaf to hem,
Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, “Nyweni nyote;
28 and seide, Drynke ye alle herof; this is my blood of the newe testament, which schal be sched for many, in to remissioun of synnes.
maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29 And Y seie to you, Y schal not drynke fro this tyme, of this fruyt of the vyne, in to that dai whanne Y schal drynke it newe with you, in the kyngdom of my fadir.
Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 And whanne the ympne was seid, thei wenten out in to the mount of Olyuete.
Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31 Thanne Jhesus seide to hem, Alle ye schulen suffre sclaundre in me, in this niyt; for it is writun, Y schal smyte the scheeperde, and the scheep of the flok schulen be scaterid.
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32 But aftir that Y schal rise ayen, Y schal go bifore you in to Galilee.
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya.”
33 Petre answeride, and seide to hym, Thouy alle schulen be sclaundrid in thee, Y schal neuer be sclaundrid.
Petro akamwambia Yesu “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe.”
34 Jhesus seide to him, Treuli Y seie to thee, for in this nyyt bifor the cok crowe, thries thou schalt denye me.
Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Peter seide to him, Yhe, thouy it bihoue that Y die with thee, Y schal not denye thee. Also alle the disciplis seiden.
Petro akamwambia, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Thanne Jhesus cam with hem in to a toun, that is seid Jessamanye. And he seide to his disciplis, Sitte ye here, the while Y go thider, and preye.
Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali.”
37 And whanne he hadde take Peter, and twei sones of Zebedee, he bigan to be heuy and sori.
Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38 Thanne he seide to hem, My soule is soreuful to the deeth; abide ye here, and wake ye with me.
Hapo akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”
39 And he yede forth a litil, and felde doun on his face, preiynge, and seiynge, My fader, if it is possible, passe this cuppe fro me; netheles not as Y wole, but as thou wolt.
Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: “Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe.”
40 And he cam to his disciplis, and foond hem slepynge. And he seide to Petir, So, whethir ye myyten not oon our wake with me?
Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41 Wake ye, and preye ye, that ye entre not in to temptacioun; for the spirit is redi, but the fleisch is sijk.
Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu.”
42 Eft the secounde tyme he wente, and preyede, seiynge, My fadir, if this cuppe may not passe, but Y drynke hym, thi wille be doon.
Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike.”
43 And eftsoone he cam, and foond hem slepynge; for her iyen weren heuyed.
Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44 And he lefte hem, and wente eftsoone, and preiede the thridde tyme, and seide the same word.
Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45 Thanne he cam to his disciplis, and seide to hem, Slepe ye now, and reste ye; loo! the our hath neiyed, and mannus sone schal be takun in to the hondis of synneris;
Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46 rise ye, go we; loo! he that schal take me, is nyy.
Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”
47 Yit the while he spak, lo! Judas, oon of the twelue, cam, and with hym a greet cumpeny, with swerdis and battis, sent fro the princis of prestis, and fro the eldre men of the puple.
Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48 And he that bitraiede hym, yaf to hem a tokene, and seide, Whom euer Y schal kisse, he it is; holde ye hym.
Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni.”
49 And anoon he cam to Jhesu, and seid, Haile, maister;
Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.
50 and he kisside hym. And Jhesus seide to hym, Freend, wherto art thou comun? Thanne thei camen niy, and leiden hoondis on Jhesu, and helden hym.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya ulichokuja kufanya.” Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51 And lo! oon of hem that weren with Jhesu, streiyte out his hoond, and drouy out his swerd; and he smoot the seruaunt of the prince of prestis, and kitte of his ere.
Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52 Thanne Jhesus seide to hym, Turne thi swerd in to his place; for alle that taken swerd, schulen perische bi swerd.
Hapo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53 Whether gessist thou, that Y may not preie my fadir, and he schal yyue to me now mo than twelue legiouns of aungels?
Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 Hou thanne schulen the scriptures be fulfilled? for so it bihoueth to be doon.
Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?”
55 In that our Jhesus seide to the puple, As to a theef ye han gon out, with swerdis and battis, to take me; dai bi dai Y sat among you, and tauyt in the temple, and ye helden me not.
Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, “Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56 But al this thing was don, that the scripturis of profetis schulden be fulfillid. Thanne alle the disciplis fledden, and leften hym.
Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57 And thei helden Jhesu, and ledden hym to Cayfas, the prince of prestis, where the scribis and the Farisees, and the eldre men of the puple weren comun togidere.
Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58 But Petir swede him afer, in to the halle of the prince of prestis; and he wente in, and sat with the seruauntis, to se the ende.
Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59 And the prince of prestis, and al the counsel souyten fals witnessing ayens Jhesu, that thei schulden take hym to deeth;
Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60 and thei founden not, whanne manye false witnessis weren comun. But at the laste, twei false witnessis camen,
lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61 and seiden, `This seide, Y may distruye the temple of God, and after the thridde dai bilde it ayen.
wakasema, “Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”
62 And the prince of prestis roos, and seide to hym, Answerist thou no thing to tho thingis, that these witnessen ayens thee?
Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
63 But Jhesus was stille. And the prince of prestis seide to hym, Y coniure thee bi lyuynge God, that thou seie to vs, if thou art Crist, the sone of God.
Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!”
64 Jhesus seide to him, Thou hast seid; netheles Y seie to you, `fro hennus forth ye schulen se mannus sone sittinge at the riythalf of the vertu of God, and comynge in the cloudis of heuene.
Yesu akamwambia, “Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Thanne the prince of prestis to-rente his clothis, and seide, He hath blasfemed; what yit han we nede to witnessis? lo! now ye han herd blasfemye; what semeth to you?
Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66 And thei answeriden, and seiden, He is gilti of deeth.
Ninyi mwaonaje?” Wao wakamjibu, “Anastahili kufa!”
67 Thanne thei speten `in to his face, and smyten hym with buffatis; and othere yauen strokis with the pawme of her hondis in his face,
Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68 and seide, Thou Crist, arede to vs, who is he that smoot thee?
wakasema, “Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!”
69 And Petir sat with outen in the halle; and a damysel cam to hym, and seide, Thou were with Jhesu of Galilee.
Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, “Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 And he denyede bifor alle men, and seide, Y woot not what thou seist.
Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”
71 And whanne he yede out at the yate, another damysel say hym, and seide to hem that weren there, And this was with Jhesu of Nazareth.
Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
72 And eftsoone he denyede with an ooth, For I knewe not the man.
Petro akakana tena kwa kiapo: “Simjui mtu huyo.”
73 And a litil aftir, thei that stooden camen, and seiden to Petir, Treuli thou art of hem; for thi speche makith thee knowun.
Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha.”
74 Thanne he bigan to warie and to swere, that he knewe not the man. And anoon the cok crewe.
Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, “Simjui mtu huyo!” Mara jogoo akawika.
75 And Petir bithouyte on the word of Jhesu, that he hadde seid, Bifore the cok crowe, thries thou schalt denye me. And he yede out, and wepte bitterli.
Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Basi, akatoka nje akalia sana.