< Matthew 19 >

1 And it was don, whanne Jhesus hadde endid these wordis, he passide fro Galilee, and cam in to the coostis of Judee ouer Jordan.
Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ngʼambo ya Mto Yordani.
2 And myche puple suede him, and he heelide hem there.
Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.
3 And Farisees camen to him, temptynge him, and seiden, Whether it be leueful to a man to leeue his wijf, for ony cause?
Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”
4 Which answeride, and seide to hem, Han ye not red, for he that made men at the bigynnyng, made hem male and female?
Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke,
5 And he seide, For this thing a man schal leeue fadir and modir, and he schal draw to his wijf; and thei schulen be tweyne in o fleisch.
naye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?
6 And so thei ben not now tweyne, but o fleisch. Therfor a man departe not that thing that God hath ioyned.
Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
7 Thei seien to hym, What thanne comaundide Moises, to yyue a libel of forsakyng, and to leeue of?
Wakamuuliza, “Kwa nini basi Mose aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?”
8 And he seide to hem, For Moises, for the hardnesse of youre herte, suffride you leeue youre wyues; but fro the bigynnyng it was not so.
Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.
9 And Y seie to you, that who euer leeueth his wijf, but for fornycacioun, and weddith another, doith letcherie; and he that weddith the forsakun wijf, doith letcherie.
Mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati naye akaoa mke mwingine, anazini. Naye amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia anazini.”
10 His disciplis seien to him, If the cause of a man with a wijf is so, it spedith not to be weddid.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali mtu asioe!”
11 And he seide to hem, Not alle men taken this word; but to whiche it is youun.
Yesu akawaambia, “Si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu.
12 For ther ben geldingis, whiche ben thus born of the modris wombe; and ther ben geldyngis, that ben maad of men; and there ben geldyngis, that han geldid hem silf, for the kyngdom of heuenes. He that may take, `take he.
Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”
13 Thanne litle children weren brouyte to hym, that he schulde putte hondis to hem, and preie.
Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wale waliowaleta.
14 And the disciplis blamyden hem. But Jhesus seide to hem, Suffre ye that litle children come to me, and nyle ye forbede hem; for of siche is the kyngdom of heuenes.
Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio kama hawa.”
15 And whanne he hadde put to hem hondis, he wente fro thennus.
Naye akaweka mikono yake juu yao, na akaondoka huko.
16 And lo! oon cam, and seide to hym, Good maister, what good schal Y do, that Y haue euerlastynge lijf? (aiōnios g166)
Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
17 Which seith to hym, What axist thou me of good thing? There is o good God. But if thou wolt entre to lijf, kepe the comaundementis.
Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza habari ya mema? Aliye mwema ni Mmoja tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”
18 He seith to hym, Whiche? And Jhesus seide, Thou schalt not do mansleying, thou schalt not do auowtrie, thou schalt not do thefte, thou schalt not seie fals witnessying;
Yule mtu akamuuliza, “Amri zipi?” Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
19 worschipe thi fadir and thi modir, and, thou schalt loue thi neiybore as thi silf.
waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.”
20 The yonge man seith to hym, Y haue kept alle these thingis fro my youthe, what yit failith to me?
Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?”
21 Jhesus seith to hym, If thou wolt be perfite, go, and sille alle thingis that thou hast, and yyue to pore men, and thou schalt haue tresoure in heuene; and come, and sue me.
Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 And whanne the yong man hadde herd these wordis, he wente awei sorewful, for he hadde many possessiouns.
Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 And Jhesus seide to hise disciplis, Y seie to you treuthe, for a riche man of hard schal entre in to the kyngdom of heuenes.
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Amin, nawaambia, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni.
24 And eftsoone Y seie to you, it is liyter a camel to passe thorou a needlis iye, thanne a riche man to entre in to the kyngdom of heuens.
Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
25 Whanne these thingis weren herd, the disciplis wondriden greetli, and seiden, Who thanne may be saaf?
Wanafunzi wake waliposikia haya, walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
26 Jhesus bihelde, and seide to hem, Anentis men this thing is impossible; but anentis God alle thingis ben possible.
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
27 Thanne Petre answeride, and seide to hym, Lo! we han forsake alle thingis, and we han suede thee; what thanne schal be to vs?
Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata! Tutapata nini basi?”
28 Jhesus seide to hem, Truli I seie to you, that ye that han forsake alle thingis, and han sued me, in the regeneracioun whanne mannus sone schal sitte in the sete of his maieste, ye schulen sitte on twelue setis, demynge the twelue kynredis of Israel.
Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, wakati wa kufanywa upya vitu vyote, Mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake kitukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
29 And euery man that forsakith hous, britheren or sistren, fadir or modir, wijf ethir children, or feeldis, for my name, he schal take an hundrid foold, and schal welde euerlastynge lijf. (aiōnios g166)
Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. (aiōnios g166)
30 But manye schulen be, the firste the laste, and the laste the firste.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.

< Matthew 19 >