< Matthew 16 >

1 And the Farisees and the Saducees camen to hym temptynge, and preieden hym to schewe hem a tokene fro heuene.
Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
2 And he answeride, and seide to hem, Whanne the euentid is comun, ye seien, It schal be clere, for heuene is rodi;
Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’
3 and the morewtid, To dai tempest, for heuene schyneth heueli.
Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.
4 Thanne ye kunne deme the face of heuene, but ye moun not wite the tokenes of tymes. An yuel generacioun and auoutresse sekith a tokene; and a tokene schal not be youun to it, but the tokene of Jonas, the profete. And whanne he hadde left hem, he wente forth.
Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.
5 And whanne his disciplis camen ouer the see, thei foryaten to take looues.
Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
6 And he seide to hem, Biholde ye, and be war of the soure dowy of Farisees and Saducees.
Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
7 And thei thouyten among hem, and seiden, For we han not take looues.
Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”
8 But Jhesus witynge seide to hem, What thenken ye among you of litel feith, for ye han not looues?
Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?
9 Yit `vndurstonden not ye, nether han mynde of fyue looues in to fyue thousynde of men, and hou many cofyns ye token?
Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
10 nether of seuene looues in to foure thousynde of men, and hou many lepis ye token?
Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
11 Whi vndurstonden ye not, for Y seide not to you of breed, Be ye war of the sourdowy of Farisees and of Saducees?
Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”
12 Thanne thei vndurstooden, that he seide not to be war of sourdowy of looues, but of the techyng of Farisees and Saducees.
Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
13 And Jhesus cam in to the parties of Cesarie of Filip, and axide hise disciplis, and seide, Whom seien men to be mannus sone?
Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”
14 And thei seiden, Summe Joon Baptist; othere Elie; and othere Jeremye, or oon of the prophetis.
Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
15 Jhesus seide to hem, But whom seien ye me to be?
Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”
16 Symount Petre answeride, and seide, Thou art Crist, the sone of God lyuynge.
Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
17 Jhesus answeride, and seide to him, Blessid art thou, Symount Bariona; for fleisch and blood schewide not to thee, but my fadir that is in heuenes.
Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.
18 And Y seie to thee, that thou art Petre, and on this stoon Y schal bilde my chirche, and the yatis of helle schulen not haue miyt ayens it. (Hadēs g86)
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs g86)
19 And to thee Y shal yyue the keies of the kingdom of heuenes; and what euer thou shalt bynde on erthe, schal be boundun also in heuenes; and what euer thou schalt vnbynde on erthe, schal be vnbounden also in heuenes.
Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
20 Thanne he comaundide to hise disciplis, that thei schulden seie to no man, that he was Crist.
Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
21 Fro that tyme Jhesus bigan to schewe to hise disciplis, that it bihofte hym go to Jerusalem, and suffre many thingis, of the eldere men, and of scribis, and princis of prestis; and be slayn, and the thridde dai to rise ayen.
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.
22 And Petre took hym, and bigan to blame him, and seide, Fer be it fro thee, Lord; this thing schal not be to thee.
Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”
23 And he turnede, and seide to Petre, Sathanas, go after me; thou art a sclaundre to me; for thou sauerist not tho thingis that ben of God, but tho thingis that ben of men.
Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
24 Thanne Jhesus seide to his disciplis, If ony man wole come after me, denye he hym silf, and take his cros, and sue me; for he that wole make his lijf saaf,
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
25 shal leese it; and he that schal leese his lijf for me, schal fynde it.
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
26 For what profitith it to a man, if he wynne al the world, and suffre peiryng of his soule? or what chaunging schal a man yyue for his soule?
Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
27 For mannes sone schal come in glorie of his fader, with his aungels, and thanne he schal yelde to ech man after his werkis.
Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
28 Treuli Y seie to you, `ther ben summe of hem that stonden here, whiche schulen not taste deth, til thei seen mannus sone comynge in his kyngdom.
Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”

< Matthew 16 >