< Mark 4 >

1 And eft Jhesus bigan to teche at the see; and myche puple was gaderid to hym, so that he wente in to a boot, and sat in the see, and al the puple was aboute the see on the loond.
Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.
2 And he tauyte hem in parablis many thingis. And he seide to hem in his techyng,
Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:
3 Here ye. Lo! a man sowynge goith out to sowe.
“Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
4 And the while he sowith, summe seed felde aboute the weie, and briddis of heuene camen, and eeten it.
Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
5 Othere felde doun on stony places, where it had not myche erthe; and anoon it spronge vp, for it had not depnesse of erthe.
Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
6 And whanne the sunne roos vp, it welewide for heete, and it driede vp, for it hadde no roote.
Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
7 And othere felde doun in to thornes, and thornes sprongen vp, and strangliden it, and it yaf not fruyt.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.
8 And other felde doun in to good loond, and yaf fruyt, springynge vp, and wexynge; and oon brouyte thretti foold, and oon sixti fold, and oon an hundrid fold.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”
9 And he seide, He that hath eeris of heryng, here he.
Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
10 And whanne he was bi hym silf, tho twelue that weren with hym axiden hym to expowne the parable.
Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.
11 And he seide to hem, To you it is youun to knowe the priuete of the kyngdom of God. But to hem that ben with outforth, alle thingis be maad in parablis, that thei seynge se,
Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,
12 and se not, and thei herynge here and vnderstonde not; lest sum tyme thei be conuertid, and synnes be foryouun to hem.
ili, “‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’”
13 And he seide to hem, Knowe not ye this parable? and hou ye schulen knowe alle parablis?
Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?
14 He that sowith, sowith a word.
Yule mpanzi hupanda neno.
15 But these it ben that ben aboute the weie, where the word is sowun; and whanne thei han herd, anoon cometh Satanas, and takith awei the word that is sowun in her hertis.
Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.
16 And in lijk maner ben these that ben sowun on stony placis, whiche whanne thei han herd the word, anoon thei taken it with ioye;
Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.
17 and thei han not roote in hem silf, but thei ben lastynge a litil tyme; aftirward whanne tribulacioun risith, and persecucioun for the word, anoon thei ben sclaundrid.
Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.
18 And ther ben othir that ben sowun in thornes; these it ben that heren the word,
Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;
19 and disese of the world, and disseit of ritchessis, and othir charge of coueytise entrith, and stranglith the word, and it is maad with out fruyt. (aiōn g165)
lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn g165)
20 And these it ben that ben sowun on good lond, whiche heren the word, and taken, and maken fruyt, oon thritti fold, oon sixti fold, and oon an hundrid fold.
Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”
21 And he seide to hem, Wher a lanterne cometh, that it be put vndur a buschel, or vndur a bed? nay, but that it be put on a candilstike?
Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?
22 Ther is no thing hid, that schal not be maad opyn; nethir ony thing is pryuey, that schal not come in to opyn.
Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni.
23 If ony man haue eeris of heryng, here he.
Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
24 And he seide to hem, Se ye what ye heren. In what mesure ye meten, it schal be metun to you ayen, and be cast to you.
Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi.
25 For it schal be youun to hym that hath, and it schal be takun awei fro him that hath not, also that that he hath.
Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”
26 And he seide, So the kingdom of God is, as if a man caste seede in to the erthe,
Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani.
27 and he sleepe, and it rise up niyt and dai, and brynge forth seede, and wexe faste, while he woot not.
Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo.
28 For the erthe makith fruyt, first the gras, aftirward the ere, and aftir ful fruyt in the ere.
Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.
29 And whanne of it silf it hath brouyt forth fruyt, anoon he sendith a sikil, for repyng tyme is come.
Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”
30 And he seide, To what thing schulen we likne the kyngdom of God? or to what parable schulen we comparisoun it?
Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza?
31 As a corne of seneuei, which whanne it is sowun in the erthe, is lesse than alle seedis that ben in the erthe;
Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini.
32 and whanne it is sprongun up, it waxith in to a tre, and is maad gretter than alle erbis; and it makith grete braunchis, so that briddis of heuene moun dwelle vndur the schadewe therof.
Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”
33 And in many suche parablis he spak to hem the word, as thei myyten here;
Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa.
34 and he spak not to hem with out parable. But he expownede to hise disciplis alle thingis bi hemsilf.
Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.
35 And he seide to hem in that dai, whanne euenyng was come, Passe we ayenward.
Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.”
36 And thei leften the puple, and token hym, so that he was in a boot; and othere bootys weren with hym.
Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye.
37 And a greet storm of wynde was maad, and keste wawis in to the boot, so that the boot was ful.
Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji.
38 And he was in the hyndir part of the boot, and slepte on a pilewe. And thei reisen hym, and seien to hym, Maistir, perteyneth it not to thee, that we perischen?
Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”
39 And he roos vp, and manasside the wynde, and seide to the see, Be stille, wexe doumbe. And the wynde ceesside, and greet pesiblenesse was maad.
Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.
40 And he seide to hem, What dreden ye? `Ye han no feith yit?
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”
41 And thei dredden with greet drede, and seiden `ech to other, Who, gessist thou, is this? for the wynde and the see obeschen to hym.
Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”

< Mark 4 >