< Luke 5 >

1 And it was don, whanne the puple cam fast to Jhesu, to here the word of God, he stood bisidis the pool of Genasereth,
Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti, watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu,
2 and saiy two bootis stondynge bisidis the pool; and the fischeris weren go doun, and waischiden her nettis.
akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao.
3 And he wente vp in to a boot, that was Symoundis, and preiede hym to lede it a litil fro the loond; and he seet, and tauyte the puple out of the boot.
Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.
4 And as he ceesside to speke, he seide to Symount, Lede thou in to the depthe, and slake youre nettis to take fisch.
Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”
5 And Symount answeride, and seide to hym, Comaundoure, we traueliden al the nyyt, and token no thing, but in thi word Y schal leye out the net.
Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”
6 And whanne thei hadden do this thing, thei closiden togidir a greet multitude of fischis; and her net was brokun.
Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika.
7 And thei bikenyden to felawis, that weren in anothir boot, that thei schulden come, and helpe hem. And thei camen, and filliden bothe the bootis, so that thei weren almost drenchid.
Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.
8 And whanne Symount Petir saiy this thing, he felde doun to the knees of Jhesu, and seide, Lord, go fro me, for Y am a synful man.
Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!”
9 For he was on ech side astonyed, and alle that weren with hym, in the takyng of fischis whiche thei token.
Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata.
10 Sotheli in lijk maner James and Joon, the sones of Zebedee, that weren felowis of Symount Petre. And Jhesus seide to Symount, Nyle thou drede; now fro this tyme thou schalt take men.
Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
11 And whanne the bootis weren led vp to the loond, thei leften alle thingis, and thei sueden hym.
Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.
12 And it was don, whanne he was in oon of the citees, lo! a man ful of lepre; and seynge Jhesu felle doun on his face, and preyede hym, and seide, Lord, if thou wolt, thou maist make me clene.
Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”
13 And Jhesus held forth his hoond, and touchide hym, and seide, Y wole, be thou maad cleene. And anoon the lepre passide awei fro hym.
Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.
14 And Jhesus comaundide to hym, that he schulde seie to no man; But go, schewe thou thee to a preest, and offre for thi clensyng, as Moises bad, in to witnessyng to hem.
Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
15 And the word walkide aboute the more of hym; and myche puple camen togidere, to here, and to be heelid of her siknessis.
Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 And he wente in to desert, and preiede.
Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.
17 And it was don in oon of the daies, he sat, and tauyte; and there weren Farisees sittynge, and doctouris of the lawe, that camen of eche castel of Galilee, and of Judee, and of Jerusalem; and the vertu of the Lord was to heele sike men.
Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa.
18 And lo! men beren in a bed a man that was sijk in the palsye, and thei souyten to bere hym in, and sette bifor hym.
Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu.
19 And thei founden not in what partie thei schulden bere hym in, for the puple, `and thei wenten on the roof, and bi the sclattis thei leeten hym doun with the bed, in to the myddil, bifor Jhesus.
Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.
20 And whanne Jhesu saiy the feith of hem, he seide, Man, thi synnes ben foryouun to thee.
Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”
21 And the scribis and Farisees bigunnen to thenke, seiynge, Who is this, that spekith blasfemyes? who may foryyue synnes, but God aloone?
Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
22 And as Jhesus knewe the thouytis of hem, he answeride, and seide to hem, What thenken ye yuele thingis in youre hertes?
Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
23 What is liyter to seie, Synnes ben foryouun to thee, or to seie, Rise vp, and walke?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
24 But that ye wite, that mannus sone hath power in erthe to foryyue synnes, he seide to the sijk man in palesie, Y seie to thee, ryse vp, take thi bed, and go in to thin hous.
Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
25 And anoon he roos vp bifor hem, and took the bed in which he lay, and wente in to his hous, and magnyfiede God.
Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu.
26 And greet wondur took alle, and thei magnyfieden God; and thei weren fulfillid with greet drede, and seiden, For we han seyn merueilouse thingis to dai.
Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”
27 And after these thingis Jhesus wente out, and saiy a pupplican, Leuy bi name, sittynge at the tolbothe. And he seide to hym, Sue thou me;
Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
28 and whanne he hadde left alle thingis, he roos vp, and suede hym.
Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
29 And Leuy made to hym a greet feeste in his hous; and ther was a greet cumpanye of pupplicans, and of othere that weren with hem, sittynge at the mete.
Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
30 And Farisees and the scribis of hem grutchiden, and seiden to hise disciplis, Whi eten ye and drynken with pupplicans and synful men?
Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
31 And Jhesus answeride, and seide to hem, Thei that ben hoole han no nede to a leche, but thei that ben sijke;
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
32 for Y cam not to clepe iuste men, but synful men to penaunce.
Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
33 And thei seiden to hym, Whi the disciplis of Joon fasten ofte, and maken preieris, also and of Farisees, but thine eten and drynken?
Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”
34 To whiche he seide, Whether ye moun make the sones of the spouse to faste, while the spouse is with hem?
Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao?
35 But daies schulen come, whanne the spouse schal be takun a wei fro hem, and thanne thei schulen faste in tho daies.
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”
36 And he seide to hem also a liknesse; For no man takith a pece fro a newe cloth, and puttith it in to an oold clothing; ellis bothe he brekith the newe, and the pece of the newe acordith not to the elde.
Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa.
37 And no man puttith newe wyne in to oolde botels; ellis the newe wyn schal breke the botels, and the wyn schal be sched out, and the botels schulen perische.
Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika.
38 But newe wyne owith to be put in to newe botels, and bothe ben kept.
Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 And no man drynkynge the elde, wole anoon the newe; for he seith, The olde is the betere.
Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”

< Luke 5 >