< Luke 23 >

1 And al the multitude of hem arysen, and ledden hym to Pilat.
Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
2 And thei bigunnen to accuse hym, and seiden, We han foundun this turnynge vpsodoun oure folk, and forbedynge tributis to be youun to the emperour, and seiynge that hym silf is Crist and kyng.
Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
3 And Pilat axide hym, and seide, Art thou kyng of Jewis? And he answeride, and seide, Thou seist.
Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
4 And Pilat seide to the princis of prestis, and to the puple, Y fynde no thing of cause in this man.
Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
5 And thei woxen stronger, and seiden, He moueth the puple, techynge thorou al Judee, bigynnynge fro Galile til hidir.
Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
6 And Pilat herynge Galile axide, if he were a man of Galile.
Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
7 And whanne he knewe that he was of the powere of Eroude, he sente hym to Eroude; which was at Jerusalem in tho daies.
Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
8 And whanne Eroude siy Jhesu, he ioyede ful myche; for long tyme he coueitide to se hym, for he herde many thingis of hym, and hopide to see sum tokene `to be don of hym.
Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
9 And he axide hym in many wordis; and he answeride no thing to hym.
Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
10 And the princis of preestis and the scribis stoden, stidfastli accusynge hym.
Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 But Eroude with his oost dispiside hym, and scornede hym, and clothide with a white cloth, and sente hym ayen to Pilat.
Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
12 And Eroude and Pilat weren maad freendis fro that dai; for bifor thei weren enemyes togidre.
Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
13 And Pilat clepide togider the princis of prestis and the maiestratis of the puple, and seide to hem,
Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
14 Ye han brouyt to me this man, as turnynge awey the puple, and lo! Y axynge bifor you fynde no cause in this man of these thingis, in whiche ye accusen hym;
akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
15 nether Eroude, for he hath sent hym ayen to vs, and lo! no thing worthi of deth is don to hym.
Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
16 And therfor Y schal amende hym, and delyuere hym.
Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
17 But he moste nede delyuer to hem oon bi the feest dai.
Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
18 And al the puple criede togidir, and seide, Do `awei hym, and delyuer to vs Barabas;
Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
19 which was sent `in to prisoun for disturblyng maad in the cite, and for mansleynge.
(Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
20 And eftsoone Pilat spak to hem, and wolde delyuer Jhesu.
Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
21 And thei vndurcrieden, and seiden, Crucifie, crucifie hym.
Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
22 And the thridde tyme he seide to hem, For what yuel hath this don? Y fynde no cause of deeth in hym; therfor Y schal chastise hym, and Y schal delyuer.
Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
23 And thei contynueden with greet voicis axynge, that he schulde be crucified; and the voicis of hem woxen stronge.
Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
24 And Pilat demyde her axyng to be don.
Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
25 And he delyueride to hem hym, that for mansleyng and sedicioun was sent in to prisoun, whom thei axiden; but he bitook Jhesu to her wille.
Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
26 And whanne thei ledden hym, thei token a man, Symon of Syrenen, comynge fro the toun, and thei leiden on hym the cross to bere aftir Jhesu.
Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
27 And there suede hym myche puple, and wymmen that weiliden, and bymorneden hym.
Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
28 And Jhesus turnede to hem, and seide, Douytris of Jerusalem, nyle ye wepe on me, but wepe ye on youre silf and on youre sones.
Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
29 For lo! daies schulen come, in whiche it schal be seid, Blessid be bareyn wymmen, and wombis that han not borun children, and the tetis that han not youun souke.
Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
30 Thanne thei schulen bigynne to seie to mounteyns, Falle ye doun on vs, and to smale hillis, Keuere ye vs.
Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
31 For if in a greene tre thei don these thingis, what schal be don in a drie?
Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
32 Also othere twei wickid men weren led with hym, to be slayn.
Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
33 And `aftir that thei camen in to a place, that is clepid of Caluerie, there thei crucifieden hym, and the theues, oon on the riyt half, and `the tother on the left half.
Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
34 But Jhesus seide, Fadir, foryyue hem, for thei witen not what thei doon.
Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
35 And thei departiden his clothis, and kesten lottis. And the puple stood abidynge; and the princis scorneden hym with hem, and seiden, Othere men he maad saaf; make he hym silf saaf, if this be Crist, the chosun of God.
Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
36 And the knyytis neiyeden, and scorneden hym, and profreden vynegre to hym,
Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
37 and seiden, If thou art king of Jewis, make thee saaf.
na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 And the superscripcioun was writun ouer hym with Greke lettris, and of Latyn, and of Ebreu, This is the kyng of Jewis.
Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
39 And oon of these theues that hangiden, blasfemyde hym, and seide, If thou art Crist, make thi silf saaf and vs.
Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
40 But `the tothir answerynge, blamyde hym, and seide, Nether thou dredist God, that art in the same dampnacioun?
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
41 And treuli we iustli, for we han resseiued worthi thingis to werkis; but this dide no thing of yuel.
Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
42 And he seide to Jhesu, Lord, haue mynde of me, whanne thou comest `in to thi kyngdom.
Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
43 And Jhesus seide to hym, Treuli Y seie to thee, this dai thou schalt be with me in paradise.
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
44 And it was almest the sixte our, and derknessis weren maad in al the erthe `in to the nynthe our.
Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
45 And the sun was maad derk, and the veile of the temple was to-rent atwo.
kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
46 And Jhesus criynge with a greet vois, seide, Fadir, in to thin hoondis Y bitake my spirit. And he seiynge these thingis, yaf vp the goost.
Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
47 And the centurien seynge that thing that was don, glorifiede God, and seide, Verili this man was iust.
Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
48 And al the puple of hem that weren there togidir at this spectacle, and sayn tho thingis that weren don, smyten her brestis, and turneden ayen.
Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
49 But alle his knowun stoden afer, and wymmen that sueden hym fro Galile, seynge these thingis.
Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
50 And lo! a man, Joseph bi name, of Aramathie, a cite of Judee, that was a decurien, a good man and a iust,
Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
51 this man concentide not to the counseil and to the dedis of hem; and he abood the kyngdom of God.
lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
52 This Joseph cam to Pilat, and axide the bodi of Jhesu,
Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 and took it doun, and wlappide it in a cleene lynen cloth, and leide hym in a graue hewun, in which not yit ony man hadde be leid.
Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
54 And the dai was the euen of the halidai, and the sabat bigan to schyne.
Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
55 And the wymmen suynge, that camen with hym fro Galile, sayn the graue, and hou his bodi was leid.
Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
56 And thei turneden ayen, and maden redi swete smellynge spicis, and oynementis; but in the sabat thei restiden, aftir the comaundement.
Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.

< Luke 23 >