< Luke 19 >
1 And Jhesus `goynge yn, walkide thorou Jericho.
Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
2 And lo! a man, Sache bi name, and this was a prince of pupplicans, and he was riche.
Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
3 And he souyte to se Jhesu, who he was, and he myyte not, for the puple, for he was litil in stature.
Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
4 And he ran bifore, and stiyede in to a sicomoure tree, to se hym; for he was to passe fro thennus.
Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
5 And Jhesus biheld vp, whanne he cam to the place, and saiy hym, and seide to hym, Sache, haste thee, and come doun, for to dai Y mot dwelle in thin hous.
Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
6 And he hiyynge cam doun, and ioiynge resseyuede hym.
Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
7 And whanne alle men sayn, thei grutchiden seiynge, For he hadde turned to a synful man.
Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
8 But Sache stood, and seide to the Lord, Lo! Lord, Y yyue the half of my good to pore men; and if Y haue ony thing defraudid ony man, Y yelde foure so myche.
Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
9 Jhesus seith to hym, For to dai heelthe is maad to this hous, for that he is Abrahams sone;
Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
10 for mannus sone cam to seke, and make saaf that thing that perischide.
Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
11 Whanne thei herden these thingis, he addide, and seide a parable, for that he was nyy Jerusalem, `and for thei gessiden, that anoon the kyngdom of God schulde be schewid.
Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
12 Therfor he seide, A worthi man wente in to a fer cuntre, to take to hym a kyngdom, and to turne ayen.
Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
13 And whanne hise ten seruauntis weren clepid, he yaf to hem ten besauntis; and seide to hem, Chaffare ye, til Y come.
Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
14 But hise citeseyns hatiden hym, and senten a messanger aftir hym, and seiden, We wolen not, that he regne on vs.
“Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
15 And it was don, that he turnede ayen, whan he hadde take the kyngdom; and he comaundide hise seruauntis to be clepid, to whiche he hadde yyue monei, to wite, hou myche ech hadde wonne bi chaffaryng.
“Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
16 And the firste cam, and seide, Lord, thi besaunt hath wonne ten besauntis.
“Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
17 He seide to hym, Wel be, thou good seruaunt; for in litil thing thou hast be trewe, thou schalt be hauynge power on ten citees.
“Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
18 And the tother cam, and seide, Lord, thi besaunt hath maad fyue besauntis.
“Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
19 And to this he seide, And be thou on fyue citees.
“Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
20 And the thridde cam, and seide, Lord, lo! thi besaunt, that Y hadde, put vp in a sudarie.
“Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
21 For Y dredde thee, for thou art `a sterne man; thou takist awey that that thou settidist not, and thou repist that that thou hast not sowun.
Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
22 He seith to hym, Wickid seruaunt, of thi mouth Y deme thee. Wistist thou, that Y am `a sterne man, takynge awei that thing that Y settide not, and repyng ethat thing that Y sewe not?
“Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
23 and whi hast thou not youun my money to the bord, and Y comynge schulde haue axid it with vsuris?
kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
24 And he seide to men stondynge nyy, Take ye awei fro hym the besaunt, and yyue ye to hym that hath ten beyauntis:
“Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
25 And thei seiden to hym, Lord, he hath ten besauntis.
“Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
26 And Y seie to you, to ech man that hath, it schal be youun, and he schal encreese; but fro him that hath not, also that thing that he hath, schal be takun of hym.
“Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
27 Netheles brynge ye hidur tho myn enemyes, that wolden not that Y regnede on hem, and sle ye bifor me.
Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
28 And whanne these thingis weren seid, he wente bifore, and yede vp to Jerusalem.
Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
29 And it was don, whanne Jhesus cam nyy to Bethfage and Betanye, at the mount, that is clepid of Olyuete, he sente hise twei disciplis, and seide,
Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
30 Go ye in to the castel, that is ayens you; in to which as ye entren, ye schulen fynde a colt of an asse tied, on which neuer man sat; vntye ye hym, and brynge ye to me.
“Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
31 And if ony man axe you, whi ye vntien, thus ye schulen seie to hym, For the Lord desirith his werk.
Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
32 And thei that weren sent, wenten forth, and fonden as he seide to hem, a colt stondynge.
Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 And whanne thei vntieden the colt, the lordis of hym seiden to hem, What vntien ye the colt?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
34 And thei seiden, For the Lord hath nede to hym.
Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 And thei ledden hym to Jhesu; and thei castynge her clothis on the colt, setten Jhesu on hym.
Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
36 And whanne he wente, thei strowiden her clothis in the weie.
Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And whanne he cam nyy to the comyng doun of the mount of Olyuete, al the puple that cam doun bygunnen to ioye, and to herie God with greet vois on alle the vertues, that thei hadden sayn,
Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
38 and seiden, Blessid be the king, that cometh in the name of the Lord; pees in heuene, and glorie in hiye thingis.
“Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
39 And sum of the Farisees of the puple seiden to hym, Maister, blame thi disciplis.
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
40 And he seide to hem, Y seie to you, for if these ben stille, stoonus schulen crye.
Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
41 And whanne he neiyede, `he seiy the citee,
Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
42 and wepte on it, and seide, For if thou haddist knowun, thou schuldist wepe also; for in this dai the thingis ben in pees to thee, but now thei ben hid fro thin iyen.
akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 But daies schulen come in thee, and thin enemyes schulen enuyroun thee with a pale, and thei schulen go aboute thee, and make thee streit on alle sidis,
Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
44 and caste thee doun to the erthe, and thi sones that ben in thee; and thei schulen not leeue in thee a stoon on a stoon, for thou hast not knowun the tyme of thi visitacioun.
Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
45 And he entride in to the temple, and bigan to caste out men sellynge ther inne and biynge,
Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
46 and seide to hem, It is writun, That myn hous is an hous of preyer, but ye han maad it a den of theues.
Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
47 And he was techynge euerydai in the temple. And the princis of prestis, and the scribis, and the princis of the puple souyten to lese hym;
Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
48 and thei founden not, what thei schulden do to hym, for al the puple was ocupied, and herde hym.
Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.