< Luke 14 >
1 And it was don, whanne he hadde entrid in to the hous of a prince of Farisees, in the sabat, to ete breed, thei aspieden hym.
Ikawa siku moja Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo siku ya Sabato, watu walikuwa wakimchunguza kwa bidii.
2 And lo! a man sijk in the dropesie was bifor hym.
Papo hapo mbele yake palikuwa na mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba mwili.
3 And Jhesus answerynge spak to the wise men of lawe, and to the Farisees, and seide, Whethir it is leeueful to heele in the sabat?
Yesu akawauliza wale Mafarisayo na walimu wa sheria, “Je, ni halali kuponya watu siku ya Sabato au la?”
4 And thei helden pees. And Jhesus took, and heelide hym, and let hym go.
Wakakaa kimya. Hivyo Yesu akamshika yule mgonjwa mkono na kumponya, akamruhusu aende zake.
5 And he answeride to hem, and seide, Whos asse or oxe of you schal falle in to a pit, and `he schal not anoon drawe hym out in the dai of the sabat?
Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ngʼombe wake aliyetumbukia katika kisima siku ya Sabato, je, hamtamvuta mara moja na kumtoa?”
6 And thei myyten not answere to hym to these thingis.
Nao hawakuwa na la kusema.
7 He seide also a parable to men bodun to a feeste, and biheld hou thei chesen the first sittyng placis, and seide to hem,
Alipoona jinsi wageni walivyokuwa wanachagua mahali pa heshima wakati wa kula, akawaambia mfano huu:
8 Whanne thou art bodun to bridalis, sitte not `at the mete in the firste place; lest perauenture a worthier than thou be bodun of hym,
“Mtu akikualika arusini, usikae mahali pa mgeni wa heshima kwa kuwa inawezekana amealikwa mtu mheshimiwa kuliko wewe.
9 and lest he come that clepide thee and hym, and seie to thee, Yyue place to this, and thanne thou schalt bigynne with schame to holde the lowest place.
Kama mkifanya hivyo yule aliyewaalika ninyi wawili atakuja na kukuambia, ‘Mpishe huyu mtu kiti chako.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kukaa katika nafasi ya chini kabisa.
10 But whanne thou art bedun to a feste, go, and sitte doun in the laste place, that whanne he cometh, that bad thee to the feeste, he seie to thee, Freend, come hiyer. Thanne worschip schal be to thee, bifor men that sitten at the mete.
Badala yake, unapoalikwa, chagua nafasi ya chini, ili yule mwenyeji wako atakapokuona atakuja na kukuambia, ‘Rafiki yangu, nenda kwenye nafasi iliyo bora zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wenzako wote.
11 For ech that enhaunsith hym, schal be lowid; and he that meketh hym, schal be hiyed.
Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”
12 And he seide to hym, that hadde bodun hym to the feeste, Whanne thou makist a mete, or a soper, nyle thou clepe thi freendis, nether thi britheren, nethir cosyns, nethir neiyboris, ne riche men; lest perauenture thei bidde thee ayen to the feeste, and it be yolde ayen to thee.
Kisha Yesu akamwambia yule aliyewaalika, “Uandaapo karamu ya chakula cha mchana au cha jioni, usialike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako walio matajiri tu. Ukifanya hivyo, wao nao wanaweza kukualika kwao, nawe ukawa umelipwa kile ulichofanya na kupata thawabu yako.
13 But whanne thou makist a feeste, clepe pore men,
Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu,
14 feble, crokid, and blynde, and thou schalt be blessid; for thei han not wherof to yelde thee, for it schal be yoldun to thee in the risyng ayen of iust men.
nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.”
15 And whanne oon of hem that saten togider at the mete hadde herd these thingis, he seide to hym, Blessid is he, that schal ete breed in the rewme of God.
Mmoja wa wale waliokuwa pamoja naye mezani aliposikia hivi akamwambia Yesu, “Amebarikiwa mtu yule atakayekula katika karamu ya Ufalme wa Mungu!”
16 And he seide to hym, A man made a greet soper, and clepide many.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anaandaa karamu kubwa, akaalika watu wengi.
17 And he sent his seruaunt in the our of soper, to seie to men that weren bodun to the feeste, that thei schulden come, for now alle thingis ben redi.
Wakati wa karamu ulipofika, akamtuma mtumishi wake akawaambie wale walioalikwa, ‘Karibuni, kila kitu ki tayari sasa.’
18 And alle bigunnen togidir to excusen hem. The firste seide, Y haue bouyt a toun, and Y haue nede to go out, and se it; Y preye thee, haue me excusid.
“Lakini wote, kila mmoja, wakaanza kutoa udhuru: Wa kwanza akasema, ‘Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali niwie radhi.’
19 And the tother seide, Y haue bouyt fyue yockis of oxun, and Y go to preue hem; Y preye thee, haue me excusid.
“Mwingine akasema, ‘Ndipo tu nimenunua jozi tano za ngʼombe wa kulimia, nami ninakwenda kuwajaribu, tafadhali niwie radhi.’
20 And an othir seide, Y haue weddid a wijf; and therfor Y may not come.
Naye mwingine akasema, ‘Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.’
21 And the seruaunt turnede ayen, and tolde these thingis to his lord. Thanne the hosebonde man was wrooth, and seide to his seruaunt, Go out swithe in to the grete stretis and smal stretis of the citee, and brynge ynne hidir pore men, and feble, blynde, and crokid.
“Yule mtumishi akarudi, akampa bwana wake taarifa. Ndipo yule mwenye nyumba akakasirika, akamwagiza yule mtumishi wake, akisema, ‘Nenda upesi kwenye mitaa na vichochoro vya mjini uwalete maskini, vilema, vipofu na viwete.’
22 And the seruaunt seide, Lord, it is don, as thou hast comaundid, and yit there is a void place.
“Yule mtumishi akamwambia, ‘Bwana, yale uliyoniagiza nimefanya, lakini bado ipo nafasi.’
23 And the lord seide to the seruaunt, Go out in to weies and heggis, and constreine men to entre, that myn hous be fulfillid.
“Ndipo yule bwana akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda kwenye barabara na vijia vilivyoko nje ya mji na uwalazimishe watu waingie ili nyumba yangu ipate kujaa.
24 For Y seie to you, that noon of tho men that ben clepid, schal taaste my soper.
Kwa maana nawaambia, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeionja karamu yangu.’”
25 And myche puple wenten with hym; and he turnede, and seide to hem,
Umati mkubwa wa watu ulikuwa ukisafiri pamoja na Yesu, naye akageuka, akawaambia,
26 If ony man cometh to me, and hatith not his fadir, and modir, and wijf, and sones, and britheren, and sistris, and yit his owne lijf, he may not be my disciple.
“Mtu yeyote anayekuja kwangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto wake, ndugu zake na dada zake, naam, hata maisha yake mwenyewe.
27 And he that berith not his cross, and cometh aftir me, may not be my disciple.
Yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28 For who of you willynge to bilde a toure, whether he `first sitte not, and countith the spensis that ben nedeful, if he haue to perfourme?
“Ni nani miongoni mwenu ambaye kama anataka kujenga nyumba, hakai kwanza chini na kufanya makisio ya gharama aone kama ana fedha za kutosha kukamilisha?
29 Lest aftir that he hath set the foundement, and mowe not perfourme, alle that seen, bigynnen to scorne hym, and seie, For this man bigan to bilde,
La sivyo, akiisha kuweka msingi, naye akiwa hana uwezo wa kuikamilisha, wote waionao wataanza kumdhihaki,
30 and myyte not make an ende.
wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kukamilisha.’
31 Or what kyng that wole go to do a bataile ayens anothir kyng, whether he sittith not first, and bithenkith, if he may with ten thousynde go ayens hym that cometh ayens hym with twenti thousynde?
“Au ni mfalme gani atokaye kwenda kupigana vita na mfalme mwingine, ambaye hakai chini kwanza na kufikiri iwapo akiwa na jeshi la watu 10,000 ataweza kupigana na yule anayekuja na jeshi la watu 20,000?
32 Ellis yit while he is afer, he sendynge a messanger, preieth tho thingis that ben of pees.
Kama hawezi, basi wakati yule mwingine akiwa bado yuko mbali, yeye hutuma ujumbe wa watu na kuomba masharti ya amani.
33 So therfor ech of you, that forsakith not alle thingis that he hath, may not be my disciple.
Vivyo hivyo, yeyote miongoni mwenu ambaye hawezi kuacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
34 Salt is good; but if salt vanysche, in what thing schal it be sauerid?
“Chumvi ni nzuri, lakini chumvi ikiwa imepoteza ladha yake, itafanywaje ili iweze kukolea tena?
35 Nethir in erthe, nethir in donghille it is profitable, but it schal be cast out. He that hath eeris of herynge, here he.
Haifai ardhi wala kwa lundo la mbolea, bali hutupwa nje. “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”