< Luke 1 >

1 Forsothe for manye men enforceden to ordeyne the tellyng of thingis, whiche ben fillid in vs,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 as thei that seyn atte the bigynnyng, and weren ministris of the word,
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 bitaken, it is seen also to me, hauynge alle thingis diligentli bi ordre, to write to thee,
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 thou best Theofile, that thou knowe the treuthe of tho wordis, of whiche thou art lerned.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 In the daies of Eroude, kyng of Judee, ther was a prest, Sakarie bi name, of the sorte of Abia, and his wijf was of the douytris of Aaron, and hir name was Elizabeth.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 And bothe weren iust bifor God, goynge in alle the maundementis and iustifiyngis of the Lord, withouten pleynt.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 And thei hadden no child, for Elizabeth was bareyn, and bothe weren of grete age in her daies.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it bifel, that whanne Zacarie schulde do the office of preesthod, in the ordre of his cours tofor God,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 aftir the custome of the preesthod, he wente forth bi lot, and entride in to the temple, to encense.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 And al the multitude of the puple was with outforth, and preiede in the our of encensyng.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 And an aungel of the Lord apperide to hym, and stood on the riythalf of the auter of encense.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 And Zacarie seynge was afraied, and drede fel vpon hym.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 And the aungel seide to hym, Zacarie, drede thou not; for thi preyer is herd, and Elizabeth, thi wijf, schal bere to thee a sone, and his name schal be clepid Joon.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 And ioye and gladyng schal be to thee; and many schulen `haue ioye in his natyuyte.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he schal be greet bifor the Lord, and he schal not drynke wyn and sidir, and he schal be fulfillid with the Hooli Goost yit of his modir wombe.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 And he schal conuerte many of the children of Israel to her Lord God;
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 and he schal go bifor hym in the spirit and the vertu of Helie; and he schal turne the hertis of the fadris in to the sones, and men out of bileue to the prudence of iust men, to make redi a perfit puple to the Lord.
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 And Zacarie seide to the aungel, Wherof schal Y wite this? for Y am eld, and my wijf hath gon fer in to hir daies.
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 And the aungel answeride, and seide to hym, For Y am Gabriel, that stonde niy bifor God; and Y am sent to thee to speke, and to euangelize to thee these thingis.
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 And lo! thou schalt be doumbe, and thou schalt not mow speke til in to the dai, in which these thingis schulen be don; for thou hast not bileued to my wordis, whiche schulen be fulfillid in her tyme.
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 And the puple was abidynge Zacarie, and thei wondriden, that he tariede in the temple.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 And he yede out, and myyte not speke to hem, and thei knewen that he hadde seyn a visioun in the temple. And he bikenyde to hem, and he dwellide stille doumbe.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 And it was don, whanne the daies of his office weren fulfillid, he wente in to his hous.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 And aftir these daies Elizabeth, his wijf, conseyuede, and hidde hir fyue monethis, and seide,
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 For so the Lord dide to me in the daies, in whiche he bihelde, to take awei my repreef among men.
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 But in the sixte moneth the aungel Gabriel was sent fro God in to a citee of Galilee, whos name was Nazareth,
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 to a maidyn, weddid to a man, whos name was Joseph, of the hous of Dauid; and the name of the maidun was Marie.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 And the aungel entride to hir, and seide, Heil, ful of grace; the Lord be with thee; blessid be thou among wymmen.
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 And whanne sche hadde herd, sche was troublid in his word, and thouyte what maner salutacioun this was.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 And the aungel seide to hir, Ne drede thou not, Marie, for thou hast foundun grace anentis God.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 Lo! thou schalt conceyue in wombe, and schalt bere a sone, and thou schalt clepe his name Jhesus.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 This schal be greet, and he schal be clepid the sone of the Hiyeste; and the Lord God schal yeue to hym the seete of Dauid, his fadir,
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and he schal regne in the hous of Jacob with outen ende, and of his rewme schal be noon ende. (aiōn g165)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 And Marie seide to the aungel, On what maner schal this thing be doon, for Y knowe not man?
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 And the aungel answeride, and seide to hir, The Hooly Goost schal come fro aboue in to thee, and the vertu of the Hiyeste schal ouerschadewe thee; and therfor that hooli thing that schal be borun of thee, schal be clepid the sone of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And lo! Elizabeth, thi cosyn, and sche also hath conceyued a sone in hir eelde, and this moneth is the sixte to hir that is clepid bareyn;
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 for euery word schal not be inpossible anentis God.
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 And Marie seide, Lo! the handmaydyn of the Lord; be it don to me aftir thi word. And the aungel departide fro hir.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 And Marie roos vp in tho daies, and wente with haaste in to the mounteyns, in to a citee of Judee.
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 And sche entride in to the hous of Zacarie, and grette Elizabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 And it was don, as Elizabeth herde the salutacioun of Marie, the yong child in hir wombe gladide. And Elizabeth was fulfillid with the Hooli Goost,
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and criede with a greet vois, and seide, Blessid be thou among wymmen, and blessid be the fruyt of thi wombe.
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 And whereof is this thing to me, that the modir of my Lord come to me?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For lo! as the voice of thi salutacioun was maad in myn eeris, the yong child gladide in ioye in my wombe.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessid be thou, that hast bileued, for thilke thingis that ben seid of the Lord to thee, schulen be parfitli don.
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 And Marie seide, Mi soule magnyfieth the Lord,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 and my spirit hath gladid in God, myn helthe.
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 For he hath biholdun the mekenesse of his handmaidun.
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 For lo! of this alle generaciouns schulen seie that Y am blessid. For he that is myyti hath don to me grete thingis, and his name is hooli.
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 And his mercy is fro kynrede in to kynredes, to men that dreden hym.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 He made myyt in his arme, he scaterede proude men with the thouyte of his herte.
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 He sette doun myyti men fro sete, and enhaunside meke men.
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 He hath fulfillid hungri men with goodis, and he hath left riche men voide.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He, hauynge mynde of his mercy, took Israel, his child;
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 as he hath spokun to oure fadris, to Abraham and to his seed, in to worldis. (aiōn g165)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
56 And Marie dwellide with hir, as it were thre monethis, and turnede ayen in to hir hous.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 But the tyme of beryng child was fulfillid to Elizabeth, and sche bare a sone.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 And the neiyboris and cosyns of hir herden, that the Lord hadde magnyfied his mercy with hir; and thei thankiden hym.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 And it was don in the eiyte dai, thei camen to circumcide the child; and thei clepiden hym Zacarie, bi the name of his fadir.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 And his moder answeride, and seide, Nay, but he schal be clepid Joon.
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 And thei seiden to hir, For no man is in thi kynrede, that is clepid this name.
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 And thei bikeneden to his fadir, what he wolde that he were clepid.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 And he axynge a poyntil, wroot, seiynge, Joon is his name.
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 And alle men wondriden. And anoon his mouth was openyd, and his tunge, and he spak, and blesside God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And drede was maad on alle her neiyboris, and alle these wordis weren pupplischid on alle the mounteyns of Judee.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 And alle men that herden puttiden in her herte, and seiden, What maner child schal this be? For the hoond of the Lord was with hym.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And Zacarie, his fadir, was fulfillid with the Hooli Goost, and prophesiede,
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 and seide, Blessid be the Lord God of Israel, for he hath visitid, and maad redempcioun of his puple.
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 And he hath rerid to vs an horn of heelthe in the hous of Dauid, his child.
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 As he spak bi the mouth of hise hooli prophetis, that weren fro the world. (aiōn g165)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
71 Helthe fro oure enemyes, and fro the hoond of alle men that hatiden vs.
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 To do merci with oure fadris, and to haue mynde of his hooli testament.
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 The greet ooth that he swoor to Abraham, oure fadir, to yyue hym silf to vs.
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 That we with out drede delyuered fro the hoond of oure enemyes,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 serue to hym, in hoolynesse and riytwisnesse bifor hym in alle oure daies.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 And thou, child, schalt be clepid the prophete of the Hiyest; for thou schalt go bifor the face of the Lord, to make redi hise weies.
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 To yyue scyence of helthe to his puple, in to remyssioun of her synnes;
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 bi the inwardnesse of the merci of oure God, in the whiche he spryngynge vp fro an hiy hath visitid vs.
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 To yyue liyt to hem that sitten in derknessis and in schadewe of deeth; to dresse oure feet in to the weie of pees.
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 And the child wexide, and was coumfortid in spirit, and was in desert placis `til to the dai of his schewing to Israel.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

< Luke 1 >