< Leviticus 15 >
1 And the Lord spak to Moises and Aaron, `and seide,
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
2 Speke ye to the sones of Israel, and seie ye to hem, A man that suffrith the rennyng out of seed, schal be vncleene;
“Waambie watu wa Israeli, na sema kwao, 'Wakati mtu yeyote kisonono kimemwathiri mwili wake unatoa ugiligili, anakuwa najisi.
3 and thanne he schal be demed to be suget to this vice, whanne bi alle momentis foul vmour `ethir moysture cleueth to his fleisch, and growith togidere.
Unajisi wake unatokana na athari ya kisonono. Iwe mwili wake unatoa ugiligili au umekoma, huo ni unajisi.”
4 Ech bed in which he slepith schal be vncleene, and where euer he sittith.
Kitanda chochote anachokilalia kitakuwa najisi, na kila kitu ambacho anakaa juu yake kitakuwa najisi.
5 If ony man touchith his bed, he schal waische his clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na awe amenajisika mpaka jioni.
6 If a man sittith where he satt, also thilke man schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vnclene `til to euentid.
Yeyote anayekaa katika kitu chochote ambacho mtu ambaye ameathiriwa na kisonono alikaa, mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
7 He that touchith hise fleischis, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Na yeyote anayegusa mwili wa ambaye ameathirika na kisonono lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na awe najisi hadi jioni.
8 If sich a man castith out spetyng on hym that is cleene, he schal waische his clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Kama mtu ambaye anaona majimaji kama hayo kwa mtu fulani ambaye ametakasika, ndipo mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na atakuwa najisi hata jioni.
9 The sadil on which he sittith,
Tandiko lolote ambalo ambaye anamajimaji ya kisonono atalikalia litakuwa najisi.
10 schal be vncleene; and ech man that touchith what euer thing is vndur hym that suffrith the fletyng out of seed, schal be defoulid `til to euentid. He that berith ony of these thingis, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Yeyote anayegusa kitu chochote kilichokuwa chini ya mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji; atanajisika mpaka jioni.
11 Ech man, whom he that is such touchith with hondis not waischun bifore, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Ambaye anamajimaji kama hayo akimgusa kabla kwanza ya kuosha kwa maji safi mikono yake, mtu aliyeguswa lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
12 `A vessel of erthe which he touchith, schal be brokun; but a `vessel of tre schal be waischun in watir.
Chungu chochote cha udongo ambacho ambaye anamajimaji kama hayo akigusa lazima kivunjwe, na kila chombo cha mti lazima kioshwe na maji safi.
13 If he that suffrith sich a passioun, is heelid, he schal noumbre seuene daies aftir his clensyng, and whanne the clothis and al `the bodi ben waischun in lyuynge watris, he schal be clene.
Wakati mwenye kisonono anapotakaswa katika kisonono chake, ndipo lazima ahesabu kwaajili yake siku saba kwaajili ya kutakasika kwake; ndipo afue nguo na aoshe mwili wake kwenye maji yatiririkayo. Ndipo atakuwa safi.
14 Forsothe in the eiytthe dai he schal take twei turtlis, ethir twei `briddis of a culuer, and he schal come in the `siyt of the Lord at the dore of tabernacle of witnessyng, and schal yyue tho to the preest;
Katika siku ya nane lazima achukue njiwa wawili au kinda mbili za njiwa na aje mbele za Yahwe pakuingilia kwenye hema ya mkutano; pale lazima atoe hao ndege kwa kuhani.
15 and the preest schal make oon for synne, and the tother in to brent sacrifice; and the preest schal preye for hym bifor the Lord, that he be clensid fro the fletyng out of his seed.
Lazima kuhani awatoe, moja kama sadaka ya dhambi na nyingine kama ya kuteketezwa, na kuhani lazima afanye upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe kwaajili ya kisonono chake.
16 A man fro whom the seed of letcherie, `ethir of fleischli couplyng, goith out, schal waische in watir al his bodi, and he schal be vncleene `til to euentid.
Kama mtu yeyote ametokwa na shahawa, ndipo lazima aoge mwili wake wote katika maji; atanajisika mpaka jioni.
17 He schal waische in watir the cloth `and skyn which he hath, and it schal be unclene `til to euentid.
Kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa lazama paoshwe kwa maji; itakuwa najisi mpaka jioni.
18 The womman with which he `is couplid fleischli, schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Na kama mwanamke na mwanaume watalala pamoja na kunakutokwa kwa shahawa kwenda kwa mwanamke, lazima wote wawili waoge katika maji; watakuwa najisi mpaka jioni.
19 A womman that suffrith the fletyng out of blood, whanne the moneth cometh ayen, schal be departid bi seuene daies; ech man that touchith hir schal be vncleene `til to euentid,
Mwanamke anapokuwa kwenye hedhi, ataendelea kunajisika kwa siku saba, na yeyote anayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 and the place in which sche slepith ether sittith in the daies of hir departyng, schal be defoulid.
Chochote anacholala juu yake wakati wa hedhi kitakuwa najisi; kila kitu ambacho anakalia kitakuwa pia najisi.
21 He that touchith her bed, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
22 Who euer touchith ony vessel on which sche sittith, he schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be defoulid `til to euentid.
Yeyote anayegusa chochote ambacho amekikalia lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo anakuwa najisi mpaka jioni.
Iwe juu ya kitanda au kitu chochote juu ya popote atakapokaa, kama akikigusa, mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
24 If a man is couplid fleischli with hir in the tyme of blood that renneth bi monethis, he schal be vncleene bi seuene daies, and ech bed in which he slepith schal be defoulid.
Kama mwanaume yeyote akilala naye, na unajisi wa mwanamke ukamgusa, atakuwa amenajisika siku saba. Kila kitanda ambacho anakilalia mwanaume huyo kitanajisika.
25 A womman that suffrith in many daies the `fletyng out of blood, not in the tyme of monethis, ethir which womman ceessith not to flete out blood aftir the blood of monethis, schal be vncleene as longe as sche `schal be suget to this passioun, as if sche is in the tyme of monethis.
Kama mwanamke ametokwa damu kwa siku nyingi ambayo siyo kipindi cha hedhi yake, au ikitoka zaidi ya kipindi chake cha hedhi, wakati wote wa siku za kunajisika, atakuwa kama alikuwa kwenye siku zake za hedhi. Yeye ni najisi.
26 Ech bed in which sche slepith, and `vessel in which sche sittith, schal be defoulid.
Kila kitanda anachokilalia wakati wote wa kutokwa damu itakuwa kwake sawa tu kama kitanda anacholalia wakati wa hedhi, na kila kitu ambacho anakalia kitakuwa najisi, kama tu unajisi wa hedhi yake.
27 Who euer touchith hir schal waische his clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
Na yeyote anayegusa kitu kati ya vitu hivyo atakuwa najisi; lazima yeye afue nguo zake na aoge mwenyewe kwenye maji, na atakuwa amenajisika mpaka jioni.
28 If the blood stondith, and ceessith to flete out, sche schal noumbre seuene daies of hir clensyng,
Lakini kama mwanamke ametakasika katika kutokwa na damu, ndipo atahesabu kwaajili yake siku saba, baada ya hizo atakuwa safi.
29 and in the eiytthe dai sche schal offre for hir silf to the preest twei turtlis, ethir twei `briddis of culueris, at the dore of the tabernacle of witnessyng;
Katika siku ya nane atachukua kwake njiwa wawili au kinda wawili wa njiwa na atawaleta kwa kuhani pakuingilia hema ya mkutano.
30 and the preest schal make oon for synne, and the tothir in to brent sacrifice; and the preest schal preye for hir bifor the Lord, and for the fletyng out of hir vnclennesse.
Huyo kuhani atatoa ndege mmoja kama sadaka ya dhambi na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa, na atafanya upatanisho kwaajili ya huyo mbele ya Yahwe kwaajili unajisi wa mwanamke atokwaye damu.
31 Therfor ye schulen teche the sones of Israel, that thei eschewe vnclennessis, and that thei die not for her filthis, whanne thei defoulen my tabernacle which is among hem.
Hivi ndivyo lazima uwatenge watu wa Israeli katika unajisi wao, hivyo hawatakufa tokana na unajisi wao, kwa kuchafua hema langu, ambapo naishi kati yao.
32 This is the lawe of hym that suffrith fletyng out of seed, and which is defoulid with fleischly couplyng,
Huu ndio utaratibu kwa kila ambaye anakisonono, kwaajili kila mwanaume ambaye shahawa yake inatoka na inamfanya kuwa najisi,
33 and of a womman which is departid in the tymes of monethis, ethir which flowith out in contynuel blood, and of the man that slepith with hir.
kwaajili ya mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha hedhi, kwaajili ya yeyote aliye na kisonono, awe mwanaume au mwanamke, na kwaajili ya yeyote anayelala na mwanamke najisi.