< Judges 20 >

1 Therfor alle the sones of Israel yeden, and weren gaderid togidere as o man, fro Dan `til to Bersabee, and fro the lond of Galaad to the Lord in Maspha; and alle the `corneris of puplis;
Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 and alle the lynagis of Israel camen to gidere in to the chirche of `the puple of God, foure hundrid thousynde of `foot men fiyters.
Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
3 And it was not `hid fro the sones of Beniamyn, that the sones of Israel hadden stied in to Maspha. And the dekene, hosebonde of the `wijf that was slayn, was axid, `how so greet felonye was doon;
(Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
4 and he answeride, Y cam with my wijf in to Gabaa of Beniamyn, and Y turnede thidur.
Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
5 And lo! men of that citee cumpassiden in nyyt the hows, in which Y dwellide, and thei wolden sle me, and thei bitraueliden my wijf with vnbileueful woodnesse of letcherie; at the last sche was deed.
Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
6 And Y took, and Y kittide hir in to gobetis, and Y sente partis in to alle the termes of youre possessioun; for so greet felonye and so greuouse synne was neuere doon in Israel.
Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
7 Alle ye sones of Israel ben present; deme ye, what ye owen do.
Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
8 And al the puple stood, and answeride as bi word of o man, `that is acordyngli, with out ayenseiyng and with out delay, We schulen not go awei in to oure tabernaclis, nethir ony man schal entre in to his hows;
Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 but we schulen do this in comyn ayens Gabaa.
Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
10 `Ten men be chosun of an hundrid, of alle the lynagis of Israel, and an hundrid of a thousynde, and a thousynde of ten thousynde, that thei bere metis to the oost, and that we, fiytynge ayens Gabaa of Beniamyn, moun yelde to it `for the trespas that that it deserueth.
Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
11 And al the puple, `as o man, cam togidere to the citee bi the same thouyt and o counsel.
Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
12 And `thei senten messangeris to al the lynage of Beniamyn, `whiche messangeris seiden, Whi so greet felony is foundun in you?
Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
13 Bitake ye the men of Gabaa, that diden this wickidnesse, that thei die, and yuel be doon awey fro Israel. `Whiche nolden here the comaundement of her britheren, the sones of Israel,
Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
14 but of alle the citees, that weren of `her part, thei camen togidere in to Gabaa, to helpe hem, and to fiyte ayens al the puple of Israel.
Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
15 And fyue and twenti thousynde weren foundun of Beniamyn, of men drawynge out swerd, outakun the dwelleris of Gabaa,
Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
16 whiche weren seuen hundrid strongeste men, fiytynge so with the lefthond as with the riythond, and castynge so stoonus with slyngis at a certeyn thing, that thei myyten smyte also an heer, and the strook of the stoon schulde not be borun in to `the tother part.
Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
17 Also of the men of Israel, with out the sones of Beniamin, weren foundun foure hundrid thousynd `of men drawynge swerd and redi to batel.
Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
18 Whiche riseden and camen in to the hows of God, that is in Silo; and thei counceliden God, and seiden, Who schal be prince in oure oost of the batel ayens the sones of Beniamyn? To whiche the Lord answeride, Judas be youre duyk.
Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
19 And anoon the sones of Israel risiden eerli, and settiden tentis ayens Gabaa.
Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
20 And fro thennus thei yeden forth to batel ayens Beniamyn, and bigunnen to fiyte ayens `the citee.
Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
21 And the sones of Beniamyn yeden out of Gabaa, and killiden of the sones of Israel in that dai two and twenti thousynde of men.
Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
22 And eft the sones of Israel tristiden in strengthe and noumbre, and dressiden schiltrun, in the same place in which thei fouyten bifore;
Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
23 so netheles that thei stieden bifore, and wepten bifor the Lord `til to nyyt, and counseliden hym, and seiden, Owe Y go forth more to fiyte ayens the sones of Beniamyn, my britheren, ether nay? To whiche he answeride, Stie ye to hem, and bigynne ye batel.
Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
24 And whanne the sones of Israel hadden go forth to batel in the tother dai ayens Beniamyn,
Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
25 the sones of Beniamyn braken out of the yates of Gabaa, and camen to hem; and the sones of Beniamyn weren wood ayens hem bi so greet sleyng, that thei castiden doun eiytene thousynde of men drawynge swerd.
Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
26 Wherfor alle the sones of Israel camen in to the hows of God, and saten, and wepten bifore the Lord, and thei fastiden in that dai `til to euentid; and thei offeriden to the Lord brent sacrifices and pesible sacrifices,
Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
27 and axiden of her staat. In that tyme the arke of boond of pees of God was there in Silo;
Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
28 and Fynees, the sone of Eleazar, sone of Aaron, was souereyn of the hows. Therfor thei counseliden the Lord, and seiden, Owen we go out more to batel ayens the sones of Beniamyn, oure britheren, ethir reste? To whiche the Lord seide, Stie ye, for to morewe Y schal bytake hem in to youre hondis.
na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
29 And the sones of Israel settiden buyschementis bi the cumpas of the citee of Gabaa;
Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
30 and the thridde tyme as onys and tweis thei brouyten forth oost ayens Beniamyn.
Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
31 But also the sones of Beniamyn braken out of the citee booldli, and pursueden ferthere the aduersaryes fleynge, so that thei woundiden of hem, as in the firste dai and the secounde, and killiden bi twey paththis `the aduersaries turnynge backis; of whiche paththis oon was borun in to Bethel, the tother in to Gabaa. And thei castiden doun aboute thretti men;
Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
32 for thei gessiden to sle hem `bi customable maner; whiche `feyneden fliyt bi craft, and token counsel, that thei schulden drawe hem fro the citee, and that thei as fleynge schulden brynge to the forseid paththis.
Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
33 Therfor alle the sones of Israel risiden of her seetis, and settiden schiltrun in the place which is clepid Baalthamar. And the buschementis, that weren aboute the citee, bigunnen to opene hem silf litil and litil,
Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
34 and to go forth fro the west part of the citee. But also othere ten thousynde of men of al Israel excitiden the dwelleris of the cite to batels; and the batel was maad greuous ayens the sones of Beniamyn, and thei vndurstoden not, that perisching neiyede to hem on eche part.
Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
35 And the Lord smoot hem in the siyt of the sones of Israel, and `thei killiden of hem in that dai fyue and twenti thousynde and an hundrid men, alle the werryours and drawynge swerd.
Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
36 Sotheli the sones of Beniamyn bigunnen to fle, `whanne thei sien, that thei weren the lowere. And the sones of Israel sien this, and `yauen to hem place to fle, that thei schulden come to the buyschementis maad redi, whiche thei hadden set bisidis the citee.
Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
37 And whanne thei hadden rise sudenli fro hid places, and Beniamyn yaf backis to the sleeris, thei entriden in to the citee, and smytiden it by the scharpnesse of swerd.
Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
38 Sotheli the sones of Israel hadden youe a signe to hem whiche thei hadden set in buyschementis, that aftir that thei hadden take the citee, thei schulden kyndle fier, and that bi smook stiynge an hiy, thei schulden schewe the citee takun.
Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
39 And whanne the sones of Israel set in thilke batel sien this; for the sones of Beniamyn gessiden hem to fle, and thei sueden bisiliere, whanne thretti men of her oost weren slayn;
ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
40 and `the sones of Israel sien as a piler of smoke stie fro the citee; also Beniamyn bihelde bihynde, whanne he siy the citee takun, and flawmes borun in hiye,
Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
41 thei that feyneden fliyt bifore, `ayenstoden strongliere with face turned. And whanne the sones of Beniamyn hadden seyn this, thei weren turned in to fliyt,
Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
42 and thei bigunnen to go to the weie of deseert; while also aduersaries pursueden hem there, but also thei, that hadden brent the citee, camen ayens hem.
Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
43 And so it was doon, that thei weren slayn of enemyes on ech part, nether ony reste of men diynge was; and thei felden, and weren cast doun at the eest coost of the citee of Gabaa.
Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
44 Forsothe thei, that weren slayn in the same place, weren eiytene thousynde of `men, alle strongeste fiyteris.
Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
45 And whanne thei that leften of Beniamyn hadden seyn this, thei fledden in to wildirnesse, and thei yeden to the stoon, whos name is Remmon. And in that fliyt the sones of Israel yeden opynli, `and yeden in to dyuerse places, and killiden fyue thousynde men; and whanne thei yeden ferther, thei pursueden hem, and killiden also othere twei thousynde.
Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
46 And so it was doon, that alle that felden doun of Beniamyn in diuerse places, weren fyue and twenti thousynde, `fiyterys moost redi to batels.
Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
47 And so sixe hundrid men leften of al the noumbre of Beniamyn, that myyten ascape, and fle in to wildirnesse; and thei saten in the stoon of Remmon foure monethis.
Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
48 Forsothe the sones of Israel yeden out, and smytiden with swerd alle the remenauntis of the citee, fro men `til to werk beestis; and deuourynge flawme wastide alle the citees and townes of Beniamyn.
Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.

< Judges 20 >