< Jude 1 >

1 Judas, the seruaunt of Jhesu Crist, and brother of James, to these that ben louyd, that ben in God the fadir, and to hem that ben clepid and kept of Jhesu Crist,
Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
2 mercy, and pees, and charite be fillid to you.
Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
3 Moost dere britheren, Y doynge al bisynesse to write to you of youre comyn helthe, hadde nede to write to you, and preye to striue strongli for the feith that is onys takun to seyntis.
Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
4 For summe vnfeithful men priueli entriden, that sum tyme weren bifore writun in to this dom, and ouerturnen the grace of oure God in to letcherie, and denyen hym that is oneli a Lord, oure Lord Jhesu Crist.
Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
5 But Y wole moneste you onys, that witen alle thingis, that Jhesus sauyde his puple fro the lond of Egipt, and the secunde tyme loste hem that bileueden not.
Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 And he reseruede vndur derknesse aungels, that kepten not her prinshod, but forsoken her hous, in to the dom of the greet God, in to euerlastynge bondis. (aïdios g126)
Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios g126)
7 As Sodom, and Gomorre, and the nyy coostid citees, that in lijk maner diden fornycacioun, and yeden awei aftir othir fleisch, and ben maad ensaumple, suffrynge peyne of euerelastinge fier. (aiōnios g166)
Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
8 In lijk maner also these that defoulen the fleisch, and dispisen lordschip, and blasfemen mageste.
Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
9 Whanne Myyhel, arkaungel, disputide with the deuel, and stroof of Moises bodi, he was not hardi to brynge in dom of blasfemye, but seide, The Lord comaunde to thee.
Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
10 But these men blasfemen, what euer thingis thei knowen not. For what euer thingis thei knowen kyndli as doumbe beestis, in these thei ben corupt.
Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
11 Wo to hem that wenten the weie of Caym, and that ben sched out bi errour of Balaam for mede, and perischiden in the ayenseiyng of Chore.
Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
12 These ben in her metis, feestynge togidere to filthe, with out drede fedinge hemsilf. These ben cloudis with out watir, that ben borun aboute of the wyndis; heruest trees with out fruyt, twies deed, drawun vp bi the roote;
Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
13 wawis of the woode see, fomynge out her confusiouns; errynge sterris, to whiche the tempest of derknessis is kept with outen ende. (aiōn g165)
Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn g165)
14 But Enoch, the seuenthe fro Adam, profeciede of these, and seide, Lo! the Lord cometh with hise hooli thousandis,
Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
15 to do dom ayens alle men, and to repreue alle vnfeithful men of alle the werkis of the wickidnesse of hem, bi whiche thei diden wickidli, and of alle the harde wordis, that wyckid synneris han spoke ayens God.
ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
16 These ben grutcheris ful of pleyntis, wandrynge aftir her desiris; and the mouth of hem spekith pride, worschipinge persoones, bi cause of wynnyng.
Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
17 And ye, moost dere britheren, be myndeful of the wordis, whiche ben bifor seid of apostlis of oure Lord Jhesu Crist; whiche seiden to you,
Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
18 that in the laste tymes ther schulen come gilours, wandringe aftir her owne desiris, not in pitee.
Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
19 These ben, whiche departen hemsilf, beestli men, not hauynge spirit.
Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
20 But ye, moost dere britheren, aboue bilde you silf on youre moost hooli feith, and preye ye in the Hooli Goost,
Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
21 and kepe you silf in the loue of God, and abide ye the merci of oure Lord Jhesu Crist in to lijf euerlastynge. (aiōnios g166)
Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios g166)
22 And repreue ye these men that ben demed,
Wahurumieni walio na mashaka;
23 but saue ye hem, and take ye hem fro the fier. And do ye merci to othere men, in the drede of God, and hate ye also thilke defoulid coote, which is fleischli.
wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
24 But to him that is miyti to kepe you with out synne, and to ordeyne bifore the siyt of his glorie you vnwemmed in ful out ioye, in the comynge of oure Lord Jhesu Crist, to God aloone oure sauyour,
Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
25 bi Jhesu Crist oure Lord, be glorie, and magnefiyng, empire, and power, bifore alle worldis, `and now and in to alle worldis of worldis. Amen. (aiōn g165)
kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn g165)

< Jude 1 >