< Joshua 1 >
1 And it was doon aftir the deeth of Moyses, seruaunt of the Lord, that the Lord spak to Josue, sone of Nun, the mynystre of Moyses, and seide to hym, Moises, my seruaunt, is deed;
Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
2 rise thou, and passe this Jordan, thou, and al the puple with thee, in to the lond which Y schal yyue to the sones of Israel.
“Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
3 Y schal yyue to you ech place which the step of youre foot schal trede, as Y spak to Moyses,
Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
4 fro the deseert and Liban til to the greet flood Eufrates; al the lond of Etheis, `til to the greet see ayens the goyng doun of the sunne, schal be youre terme.
kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
5 Noon schal mow ayenstonde you in alle the daies of thi lijf; as Y was with Moises, so Y schal be with thee; Y schal not leeue, nether Y schal forsake thee.
Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
6 Be thou coumfortid, and be thou strong; for thou schalt departe bi lot to this puple the lond, for which Y swoor to thi fadris, that Y schulde yyue it to hem.
Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
7 Therfor be thou coumfortid, and be thou ful strong, that thou kepe and do al the lawe, which Moyses, my seruaunt, comaundide to thee; bowe thou not fro it to the riyt side, ether to the left side, that thou vndirstonde alle thingis whiche thou doist.
Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
8 The book of this lawe departe not fro thi mouth, but thou schalt thenke therynne in daies and nyytis, that thou kepe and do alle thingis that ben writun therynne; thanne thou schalt dresse thi weie, and schalt vndirstonde it.
Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
9 Lo! Y comaunde to thee; be thou coumfortid, and be thou strong; nyle thou drede `withoutforth, and nyle thou drede withynne; for thi Lord God is with thee in alle thingis, to whiche thou goost.
Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
10 And Josue comaundide to the princis of the puple, and seide, Passe ye thoruy the myddis of the castels; and comaunde `ye to the puple, and seie ye, Make ye redi metis to you,
Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
11 for after the thridde dai ye schulen passe Jordan, and ye schulen entre to welde the lond, which youre Lord God schal yyue to you.
“Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
12 Also he seide to men of Ruben, and `to men of Gad, and to the half lynage of Manasses, Haue ye mynde of the word which Moises,
Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
13 the `seruaunt of the Lord, comaundide to you, and seide, Youre Lord God hath youe to you reste and al the lond;
“Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
14 youre wyues and youre sones and beestis schulen dwelle in the lond which Moises yaf to you biyende Jordan; but passe ye armed, `alle strong in hond, bifor youre britheren; and fiyte ye for hem,
Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
15 til the Lord yyue reste to youre britheren, as `he yaf also to you, and `til also thei welden the lond which youre Lord God schal yyue to hem; and so turne ye ayen in to the lond of youre possessioun, and ye schulen dwelle in that lond which Moises, `seruaunt of the Lord, yaf to you ouer Jordan, ayens the `rysyng of the sunne.
Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
16 And thei answeriden to Josue, and seiden, We schulen do alle thingis whiche thou comaundidist to vs, and we schulen go, whidir euer thou sendist vs;
Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
17 as we obeieden in alle thingis to Moises, so we schulen obeie also to thee; oneli thi Lord God be with thee, as he was with Moyses.
Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
18 Die he that ayenseith thi mouth, and obeieth not to alle thi wordis, whiche thou comaundist to hym; oneli be thou coumfortid, and do thou manli.
Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.