< Joshua 6 >

1 Forsothe Jerico was closid and wardid, for the drede of the sones of Israel, and no man durste entre, ethir go out.
Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
2 And the Lord seide to Josue, Lo! Y yaf in to thin hondis Jerico, and the king therof, and alle strong men.
Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
3 Alle ye fiyteris, cumpasse the citee onys bi the day; so ye schulen do in sixe daies.
Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
4 Forsothe in the seuenthe dai the preestis schulen take seuene clariouns, of whiche `the vss is in iubile; and thei schulen go bifor the arke of boond of pees; and seuen sithes ye schulen cumpasse the citee, and the preestis schulen trumpe with clariouns.
Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
5 And whanne the vois of the trumpe schal sowne lengere, and more bi whiles, and schal sowne in youre eeris, al the puple schal crie togidere with gretteste cry; and the wallis of the citee schulen falle alle doun, and alle men schulen entre bi the place, ayens which thei stonden.
Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
6 Therfor Josue, the sone of Nun, clepide preestis, and seide to hem, Take ye the ark of boond of pees, and seuene othere preestis take seuene clariouns of iubile yeeris, and go thei bifor the arke of the Lord.
Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
7 Also Josue seide to the puple, Go ye, and cumpasse ye the citee, and go ye armed bifor the arke of the Lord.
Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
8 And whanne Josue hadde endid the wordis, and seuene preestis trumpiden with seuen clariouns bifor the arke of boond of pees of the Lord,
Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
9 and al the puple armed yede bifore, the tothir comyn puple of fiyteris suede the arke, and alle thingis sowneden with clariouns.
Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
10 Sotheli Josue comaundide to the puple, and seide, Ye schulen not crye, nethir youre vois schal be herd, nethir ony word schal go out of youre mouth, til the dai come, in which Y schal seie to you, Crye ye, and make ye noyse.
Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
11 Therfor the arke of the Lord cumpasside the citee onys bi day, and turnede ayen in to the castels, and dwellide there.
Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
12 Therfor while Josue roos bi nyyt, preestis tooken the arke of the Lord;
Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
13 and seuene of the preestis token seuen clariouns, of whiche `the vss is in iubilee, and yeden bifor the arke of the Lord, `and yeden, and trumpiden; and the puple yede armed bifor hem. Sotheli the tother comyn puple suede the arke, and sownede with clariouns.
Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
14 And thei cumpassiden the citee in the secunde dai onys, and turneden ayen in to the castels; so thei dyden in sixe daies.
Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
15 Sotheli in the seuenthe dai thei risiden eerli, and cumpassiden the citee, as it was disposid, seuen sithis.
Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
16 And whanne in the seuenthe cumpas preestis sowneden with clariouns, Josue seide to al Israel, Crie ye, for the Lord hath bitake the citee to vs;
Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
17 and this citee be cursid, ethir distried, and alle thingis that ben therynne be halewid to the Lord. Raab the hoor aloone lyue, with alle men that ben with hir in the hows; for sche hidde the messangeris whiche we senten.
Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
18 Forsothe be ye war, lest ye touchen ony thing of these that ben comaundid to you, and ye ben gilti of trespassyng; and alle the castels of Israel be vndur synne, and be troblid.
Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
19 Sotheli what euer thing is of gold, and of siluer, and of brasun vessels, and of yrun, be halewid to the Lord, and be kept in hise tresoris.
Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
20 Therfor while al the puple criede, and the trumpis sowneden, aftir that the sowne sownede in the eeris of the multitude, the walles felden doun anoon; and ech man stiede bi the place that was ayens hym. And thei token the citee,
Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
21 and killiden alle thingis that weren therynne, fro man `til to womman, fro yong child `til to eld man; also thei smytiden bi the scharpnesse of swerd, oxun, and scheep, and assis.
Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
22 Forsothe Josue seide to twei men, that weren sent aspieris, Entre ye in to the hows of the womman hoore, and brynge ye forth hir, and alle thingis that ben herne, as ye maden stedfast to hir bi an ooth.
Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
23 And the yonge men entriden, and ledden out Raab, and her fadir, and modir, and britheren, and al the purtenaunce of houshold, and the kynrede `of hir; and maden to dwelle without the castels of Israel.
Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
24 Sotheli thei brenten the citee, and alle thingis that weren foundun therynne, without gold, and siluer, and brasun vesselis, and yrun, which thei halewiden in to the `treserie of the Lord.
Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
25 Sotheli Josue made Raab the hoore to lyue, and `the hows of hir fadir, and alle thingis that sche hadde; and thei dwelliden in the myddis of Israel, `til in to present dai; for sche hidde the messangeris, whiche he sente to asspie Jerico. In that tyme Josue preiede hertli,
Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
26 and seide, Cursid bifor the Lord be the man, that reisith and bildith the citee of Jerico! Leie he the foundementis therof in his firste gendrid sone, and putte he the yatis therof in the laste of fre children.
Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
27 Therfor the Lord was with Josue, and his name was pupplischid in ech lond.
Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.

< Joshua 6 >