< Joshua 22 >

1 In the same tyme Josue clepide men of Ruben, and men of Gad, and half the lynage of Manasses,
Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
2 and seide to hem, Ye han do alle thingis whiche Moises, `seruaunt of the Lord, comaundide to you, also ye obeieden to me in alle thingis;
Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
3 nether ye han lefte youre britheren in mych tyme til in to present dai, and ye kepten the comaundement of youre Lord God.
Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
4 Therfor for youre Lord God yaf reste and pees to youre britheren, as he bihiyte, turne ye ayen, and go ye in to youre tabernaclis, and in to the loond of youre possessioun, which lond Moyses, the `seruaunt of the Lord, yaf to you biyende Jordan;
Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
5 so onely that ye kepe bisili, and fille in werk the comaundement and lawe, `which lawe Moises, the `seruaunt of the Lord, comaundide to you; that ye loue youre Lord God, and go in alle hise weies, and kepe hise heestis, and cleue to hym and serue him in al youre herte, and in al youre soule.
Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
6 And Josue blesside hem, and lefte hem, whiche turneden ayen in to her tabernaclis.
Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
7 Sotheli Moyses hadde youe possessioun in Basan to the half lynage of Manasses; and therfor to the half lynage that lefte Josue yaf part among her othere britheren biyendis Jordan, at the west coost therof. And whanne Josue leet hem go in to her tabernaclis, and hadde blessid hem,
Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
8 he seyde to hem, With myche catel and richessis turne ye ayen to youre seetis; with siluer and gold, and bras, and yrun, and myche clothing; departe ye the prey of enemyes with youre britheren.
na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
9 And the sones of Ruben, and the sones of Gad, and `half the lynage of Manasses turneden ayen, and yeden fro the sones of Israel fro Silo, which is set in the lond of Canaan, that thei schulden entre in to Galaad, the lond of her possessioun, which thei gaten bi `comaundement of the Lord in the hond of Moises.
Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
10 And whanne thei hadden come to the litle hillis of Jordan, in to the lond of Canaan, thei bildiden bisidis Jordan an auter of greetnesse ouer comyn mesure.
Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
11 And whanne the sones of Israel hadden herd this, and certeyn messangeris hadden teld to hem, that the sones of Ruben, and of Gad, and the half lynage of Manasses hadden bildid an auter in the lond of Canaan, on the heepis of Jordan, ayens the sones of Israel,
Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
12 alle camen togidir in Silo, that thei schulden stie, and fiyte ayens hem.
Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
13 And in the meene tyme thei senten to hem in to the lond of Galaad, Fynees, preest,
Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
14 the sone of Eleazar, and ten princes with hym; of ech lynage o prince.
na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
15 Whiche camen to the sones of Ruben, and of Gad, and of the half lynage of Manasses, in to the lond of Galaad, and seiden to hem,
Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
16 Al the puple of the Lord sendith these thingis; What is this trespassyng? Whi han ye forsake the Lord God of Israel, and han bildid a cursid auter, and han go awei fro the worschiping of hym?
“Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
17 Whether it is litil to you that ye synneden in Belfegor, and the wem of this trespas dwellith in you til in to present dai, and many of the puple felden doun?
Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
18 And to day ye han forsake the Lord, and to morewe, that is, in tyme to comynge, the ire of hym schal be feers ayens al Israel.
Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
19 That if ye gessen, that the lond of youre possessioun is vncleene, passe to the lond, `in which the tabernacle of the Lord is, and dwelle ye among vs, oneli that ye go not awei fro the Lord, and fro oure felouschipe, bi an auter bildid outakun the auter of oure Lord God.
Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
20 Whether not Achar, the sone of Zare, passide the comaundement of the Lord, and his ire felde on al the puple of Israel? And he was o man; and we wolden that he aloone hadde perischid in his trespas.
Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
21 And the sones of Ruben, and of Gad, and of half the lynage of Manasses, answeriden to the princes of the message of Israel,
Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
22 The strongeste Lord God hym silf of Israel knowith, and Israel schal vndirstonde togidere; if we bildiden this auter for entent of trespassyng, `that is, of ydolatrye, he kepe not vs, but punysche in present time;
“Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
23 and if we diden bi that mynde, that we schulden putte theronne brent sacrifice, and sacrifice, and pesible sacrifices, he seke, and deme;
kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
24 and not more `bi that thouyt and tretyng that we seiden, Youre sones schulen seie `to morew to oure sones, What is to you and to the Lord God of Israel? Ye sones of Ruben,
La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
25 and ye sones of Gad, the Lord hath set a terme, the flood Jordan, bitwixe vs and you; and therfor ye han not part in the Lord; and bi this occasioun youre sones schulen turne awei oure sones fro the drede of the Lord. Therfor we gessiden betere,
Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
26 and seiden, Bilde we an auter to vs, not in to brent sacrifices, nethir to sacrifices to be offrid,
Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
27 but in to witnessyng bitwixe vs and you, and bitwixe oure children and youre generacioun, that we serue the Lord, and that it be of oure riyt to offre brent sacrifices, and sacrifices, and pesible sacrifices; and that youre sones seie not to morewe to oure sones, No part in the Lord is to you.
ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
28 And if `youre sones wolen seie this, `oure sones schulen answere hem, Lo! the auter of the Lord, which oure fadris maden, not in to brent sacrifices, nether in to sacrifice, but in to oure and your witnessing euerlastinge.
Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
29 Fer be this trespas fro vs, that we go awei fro the Lord, and forsake hise steppis, bi an auter bildid to brent sacrifices, and sacrifices, and sacrifices of preisyng to be offrid, outakun the auter of oure `Lord God, which is bildid bifore his tabernacle.
Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
30 And whanne these thingis weren herd, Fynees, preest, and the princes of message of Israel, that weren with hym, weren plesyd; and thei resseyueden gladli the wordis of the sones of Ruben, and of Gad, and of the half lynage of Manasses.
Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
31 And Finees, preest, the sone of Eleazar, seide to hem, Now we wyten, that the Lord is with you; for ye ben alien fro this trespassyng, and ye han delyuered the sones of Israel fro the hond, `that is, punyschyng, of the Lord.
Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
32 And Fynees turnede ayen with the princes fro the sones of Ruben and of Gad, fro the lond of Galaad to the coost of Canaan, to the sones of Israel; and he telde to hem.
Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
33 And the word pleside to alle men herynge; and the sones of Israel preisiden God, and seiden, that no more `thei schulden stie ayens hem, and fiyte, and do awei the lond of her possessioun.
Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
34 And the sones of Ruben and the sones of Gad clepiden the auter, which thei hadden bildid, Oure Witnessyng, that the Lord hym silf is God.
Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”

< Joshua 22 >